Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Januari 1
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 15: “Hubiri kwa Ufahamu Wenye Kina.” Zungumzia mambo makuu, na uwe na wonyesho wa utoaji mmoja au mbili. Julisha kutaniko ni vitabu gani vya zamani vilivyo akibani wakati huu.
Dak 20: Kupanga Fursa za Kutoa Ushahidi. Mara nyingi wengi wetu huwa na fursa za kusafiri nazo fursa nzuri za kutoa ushahidi wa vivi hivi hutokea. Ukitumia kitabu Kiongozi cha Shule, kurasa 80-82, mafungu 11-16, pitia madokezo ya jinsi ya kuanzisha mazungumzo na watu usiowafahamu. Onyesha jinsi kujitayarisha mapema husaidia kupata matokeo mazuri. Panga uwe na wahubiri watatu tofauti watoe wonyesho wa jinsi ya kuanzisha mazungumzo na mtumishi wa kituo cha petroli, abiria akiwa ndani ya usafiri wa umma, na mtu anayesimama katika foleni sokoni au dukani. Kumbusha wahubiri waweke rekodi za wale wanaoonyesha kupendezwa na wapange mtu fulani awatembelee baadaye.
Wimbo 28 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 8
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Toa pongezi inayofaa kwa tegemezo la kifedha la kwenu na la kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri habari njema.
Dak 15: Thamani Ilindayo ya Kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Mzee azungumza na kutaniko umaana wa kila mmoja kujaza ifaavyo kadi yake ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia na kuibeba kila nyakati na uhitaji wa watoto kuwa na Kadi ya Utambulishi sikuzote. Kama vile kichwa cha kadi hiyo kinavyodokeza, huandaa taarifa ya mapema juu ya jambo linalotakikana (au lisilotakikana) kuhusu utunzaji wa kitiba. Kwa nini jambo hili hufanywa kila mwaka? Kadi ya karibuni ni yenye kusadikisha zaidi kuliko ile inayoweza kuonwa kuwa ya zamani au isiyoonyesha tena masadikisho ya mtu. Hati hiyo hukusemea ikiwa huwezi kusema wewe mwenyewe. Kadi zitatolewa usiku huu. Zapaswa kujazwa kwa uangalifu nyumbani, lakini hazipaswi kutiwa sahihi. Kama vile imekuwa ikifanywa kwa miaka miwili iliyopita, kutia sahihi na kushuhudiwa kutafanywa mahali pa Funzo la Kitabu la Kutaniko, chini ya usimamizi wa viongozi wa funzo la kitabu. Wale wanaotia sahihi wakiwa mashahidi wanapaswa kwa kweli kuona mwenye kadi akitia sahihi hati hiyo. Hili litafanywa baada ya funzo la kitabu katika juma la Januari 15. (Ona ukurasa wa 2 wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1994 kwa habari zaidi juu ya utaratibu huu. Ona pia barua ya Oktoba 15, 1991.) Wahubiri wote waliobatizwa wanaweza kujaza kadi yao ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Kwa kugeuza usemi ulio katika kadi hii kulingana na hali zao na masadikisho yao wenyewe, wahubiri wasiobatizwa wanaweza kuandika mwelekezo wao wenyewe. Wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wajaze Kadi ya Utambulishi.
Dak 20: “Iweni Watendaji—Si Wasikiaji Tu.” Maswali na majibu. Kadiri wakati uruhusuvyo, zungumzia umaana wa utii, kwa kutegemea kitabu Insight, Buku la 2, ukurasa wa 521, mafungu 1 na 2.
Wimbo 70 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 15
Dak 12: Matangazo ya kwenu. Zungumza kifupi juu ya tatizo linaloongezeka la wasiokuwepo nyumbani. Tia moyo wahubiri wakomboe wakati kwa kuchukua hatua ya kwanza kuwafikia watu ambao huenda wakawa wanapita, wanasimama kwenye kijia, au wanaoketi kwenye magari.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. (Au “Linda Hisi Yako ya Uharaka,” hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1995, kurasa 25-28.)
Dak 18: “Rudi Ili Kuokoa Wengine.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa. Pendekeza mradi wa kuanzisha mafunzo katika kitabu kipya, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 22
Dak 5: Matangazo ya kwenu.
Dak 20: “Nufaika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996—Sehemu ya 1.” Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa shule. Pitia mielekezo inayotolewa kwa ajili ya migawo ya wanafunzi katika maagizo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, iliyotokea kwenye Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1995.
Dak 20: “Sema kwa Ujasiri.” Hotuba na mazungumzo yashughulikiwe na mzee. Pitia mipango ya utumishi wa Jumapili ya kwenu. Toa pongezi kwa uungaji-mkono mzuri, na utoe madokezo panapohitaji kufanyiwa maendeleo.
Wimbo 92 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 29
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.”
Dak 15: Kutoa Ushahidi Wakati wa Halihewa Mbaya. Wengi hulazimika kukabiliana na baridi, au mvua wakati wa majira ya mvua nyingi. Wengine hulazimika kukabiliana na hali ya anga yenye joto zaidi. Kikundi cha wahubiri watatu au wanne wazungumza jinsi wanavyoweza kudumisha ushiriki mzuri katika huduma ijapokuwa halihewa hiyo. Makutaniko mengi huhubiri maeneo ya mashambani wakati wa miezi ya ukavu, wakikazia maeneo ya jiji kubwa, mjini au sokoni wakati wa majira ya mvua nyingi, na kupanga mikutano ya utumishi katika eneo ili kupunguza kusafiri kwingi. Wengine huhifadhi majengo yenye vyumba mbalimbali kwa ajili ya siku zilizo mbaya. Katizeni mahubiri ya nyumba kwa nyumba kwa kufanya ziara za kurudia. Vaeni nguo zifaazo ili kuwa na joto na ukavu. Tumia simu panapowezekana au uandikaji wa barua inapokuwa si jambo la hekima kwenda nje. Zungumza mawazo yoyote mengine ambayo umeona yakiwa yenye kutumika katika eneo lako.
Dak 20: Toa Kitabu Upeo wa Ufunuo Wakati wa Februari. Eleza kwa nini kitabu cha Ufunuo kilionwa kuwa fumbo tusiloweza kulielewa kwa muda mrefu. Pitia mafungu 6 hadi 9 kwenye ukurasa wa 8, ukionyesha kwa nini kitabu hiki chahitajiwa. Tia moyo wahubiri wafikirie mawazo haya ili kwamba wawe na msingi wa mambo ya kuzungumza milangoni. Rejeza kwenye “Muundo wa Kitabu cha Ufunuo” kwenye kurasa 98-99, na uonyeshe jinsi habari hii inavyoweza kutumiwa ili kutoa maoni ya ujumla juu ya kitabu cha Ufunuo. Elekeza uangalifu kwenye picha zenye kusisimua zilizo katika sehemu ya ndani ya majalada ya mbele na nyuma na jinsi zinavyoweza kutumiwa ili kuanzisha mazungumzo. Wakumbushe wote wachukue nakala za kutumia katika utumishi mwisho-juma huu.
Wimbo 143 na sala ya kumalizia.