Wimbo 31
Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova
1. Kwa nyumba ya Mungu Yesu
Alitia bidii.
Iliwaka ndani yake,
Kafunua uovu.
Alihubiri wokovu,
Kweli akatangaza.
Kwa jina la Baba yake
Bidii ikamula.
2. Wafuasi na mitume
Walitia bidii.
Kwayo roho takatifu
Makundi yakakua!
Daima wakahubiri,
Watu nyumba kwa nyumba.
Wakatangaza wokovu
Wakisema tubuni.
3. Na leo twaona watu
Walio na bidii,
Roho yao haizimwi
Na ulimwengu ’bovu.
Wahimizwa na Yehova;
Wajitoa kwa moyo.
Wanahubiri Ufalme,
Wanatia bidii.