Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/90 kur. 1-2
  • Uwe Mwenye Bidii Katika Kueneza Ujumbe wa Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwenye Bidii Katika Kueneza Ujumbe wa Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ONYESHA BIDII KATIKA KUTOA BROSHUA
  • MADOKEZO YA KUTOA BROSHUA
  • Watu Wenye Juhudi ya Kazi Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Je, Una “Bidii kwa Ajili Ya Kazi Njema”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova
    Mwimbieni Yehova Sifa
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 8/90 kur. 1-2

Uwe Mwenye Bidii Katika Kueneza Ujumbe wa Ufalme

1 Yehova ni Mungu wa kazi njema, naye ni mwenye bidii katika kuitimiza. Kila jambo afanyalo ni kwa ajili ya wema wa wale wanaomtumikia. Yesu aliweka kielelezo chema katika kuiga bidii ya Babae. Katika pindi moja, bidii kwa ajili ya nyumba ya Yehova ilimumotisha aondoshe hekaluni wale waliokuwa wakiligeuza kuwa nyumba ya biashara. (Yn. 2:14-17) Sisi pia lazima tudhihirishe bidii katika utumishi wetu kwa Yehova Mungu endapo twataka kutambulishwa kuwa kikundi cha watu chenye “bidii kwa ajili ya kazi njema.”—Titus 2:14, NW.

2 Kazi njema za Wakristo hunufaisha wengine. Jambo lenye manufaa zaidi tunaloweza kufanyia mtu mwingine ni kumsaidia ajue na kutumikia Yehova. (Yn. 17:3) Sisi hutoa msaada huo kupitia kazi yetu yenye bidii ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi.

3 Bidii ni nini? Bidii ni ari. Bidii ya Kikristo hutokana na tamaa yenye juhudi ya kufanya yaliyo haki na yanayofaa. Neno la Kigiriki kwa “bidii” humaanisha “kuchemka.” Tukiwa wahudumu wa Mungu, twapaswa kuonyesha sifa hiyo tunapoeneza ujumbe wa Ufalme. Je! sisi ni wenye bidii katika huduma? Je! sisi tunafanya yote tuwezayo kuwasaidia wengine wajifunze juu ya makusudi ya Yehova?

ONYESHA BIDII KATIKA KUTOA BROSHUA

4 Katika mwezi wa Agosti, tutakuwa tena na pendeleo la kutoa broshua yoyote yenye kurasa 32 isipokuwa Shule na Mashahidi wa Yehova. Twaweza kutoa Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Should You Believe in the Trinity?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, au Serikali Itakayoleta Paradiso. Fanya matayarisho ya kutoa broshua yoyote inayoonekana kuwa yafaa kwa ajili ya eneo na pia kwa mtu unayekuta mlangoni.

5 Ili kuwa wenye bidii katika keneneza ujumbe wa Ufalme, twahitaji kuwa tayari vya kutosha. Je! sisi tumezoelena na Kichwa cha Mazungumzo cha wakati huu? Twaweza kuunganishaje Kichwa cha Mazungumzo na broshua tunayotoa? Ni mawazo gani hususa katika broshua tunayoweza kutaja? Tukichukua wakati kuzoeleana na broshua hizo tano na kujenga ndani ya akili zetu idili kwa ajili yazo, tutakuwa tayari kuzitoa kwa bidii kwa wale waliopo kwenye eneo.

MADOKEZO YA KUTOA BROSHUA

6 Baada ya kujitanguliza, huenda ukasema hivi: “Je! umepata kushangaa kama Mungu anahangaishwa na uovu katika ulimwengu leo? [Ruhusu itikio.] Biblia hueleza kwamba karibuni waovu wataangamizwa. [Soma Zaburi 92:7.] Kwa kuwa ndivyo ilivyo, twaweza kugeukia nani atupe uongozi na himaya ya kweli? [Soma Zaburi 145:20.] Kwa hiyo njia pekee yetu ya wokovu ni kupitia uhusiano pamoja na Muumba wetu, Yehova Mungu. Twahitaji kufikiria baraka ambazo ameahidi ainabinadamu wote watiifu.” Kisha waweza kufungua picha 49 katika broshua Maisha Duniani na kusoma maelezo ya picha hiyo, ukikazia baraka zilizotolewa kielezi. Au fungua ukurasa 29 katika broshua Serikali, na kuzungumza juu ya baraka zilizoelezwa hapo. Huenda wengine wakataka kutumia mafungu 49 na 50 katika broshua “Tazama!” ili kueleza ambayo Ufalme wa Mungu utafanyia ainabinadamu.

7 Kwa kuwa hizi ni nyakati zenye hatari, ujumbe tulio nao ni wenye uharaka. Kuna uhitaji kwetu kuwa wenye bidii katika kueneza ujumbe wa Ufalme, kutia moyo wengine wafahamikiane na Mungu na Neno lake. Kwa kueneza kwa bidii maarifa hayo yenye kutoa uhai, tunatoa uthibitisho wa ujitoaji kimungu wetu na upendo wetu kwa ajili ya Yehova. Jiulize mwenyewe: ‘Je! mimi nina bidii kwa ajili ya kazi njema? Je! tegemezo langu la utendaji wa kuhubiri laweza kuelezwa kuwa lenye ari na la nafsi yote?’ Majibu yetu yatatuambia mengi juu ya ilivyo bidii yetu. Kadiri tunavyoshiriki zaidi katika kueneza ujumbe wa Ufalme, ndivyo bidii yetu itakavyokuwa kubwa zaidi. Wengine wataona kwamba kweli kweli sisi ni watu wenye bidii kwa ajili ya kazi njema.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki