Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 5/8 uku. 11
  • Itikio kwa ”Mankind’s Search for God”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Itikio kwa ”Mankind’s Search for God”
  • Amkeni!—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utangulizi wa Kitabu Mankind’s Search for God
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Uhitaji wa Ainabinadamu wa Kutafuta-Tafuta Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kutolea Ushahidi “Watu wa Namna Zote”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • ‘Tamaa Inayochochea Moyo na Akili’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 5/8 uku. 11

Itikio kwa ”Mankind’s Search for God”

MOJAWAPO ya mambo makuu katika Mikusanyiko ya Wilaya ya “Lugha Iliyo Safi,” ambayo Mashahidi wa Yehova walikuwa nayo kuanzia katikati ya 1990 hadi mapema 1991, ilikuwa ni kitolewaji cha kitabu Mankind’s Search for God. Kinatoa maelezo mafupi yenye kueleweka juu ya asili, historia, na itikadi za dini kubwa-kubwa za ulimwengu, na kinaeleza jinsi Mungu wa kweli anavyoweza kupatikana. Wasomaji kuzunguka ulimwengu wameitikiaje?

“Pongezi yangu ya moyoni kwa kitabu Mankind’s Search for God,” akasema E. G., kutoka Ujerumani, asiye Shahidi. “Uchunguzi huo na ulio wa ndani kwa dini za watu mmoja mmoja ni wenye kutazamisha sana na hufanya kusoma kusisimue. Zaidi ya hilo, kitabu hicho hakipungukiwi katika mambo yanayotumika—ni kinyume kabisa cha hilo. Naweza kutoa pendekezo tu kwamba watu wachunguze dini yao kwa msingi wa kitabu hiki.”

Msomaji kutoka Flushing, New York, U. S. A., aliandika: “Mimi ni Mwislamu, na Al-Islaam ni dini yangu. Nakithamini kitabu chenu kipya Mankind’s Search for God. Nathamini hasa habari mliyo nayo kuhusu dini yangu.”

Katika Uholanzi, A. v. D., mwenye umri wa miaka 17, aliangusha nakala ya kitabu kwa mwanafunzi mwenzi, ambaye alikitumia kutayarishia mgawo wa shule. Mwalimu alitaka kujua chanzo cha habari ya msichana huyo. Alipokiona kitabu hicho, aliagiza nakala tatu. A. v. D. aendelea: “Siku iliyofuata nilimpa mwalimu vitabu vitatu vipya, ambavyo alivionyesha kwa walimu wengine mara moja. Muda mfupi baadaye, akaniambia, ‘Ni sawa. Nina ruhusa kutoka kwa wasimamizi wa shule ya kuagiza vitabu 35.’”

Kutoka British Columbia, Kanada, wenzi wawili waliandika, “mankind’s Search for God kingeweza kuathiri watu zaidi kutoka tamaduni nyingi kuliko vile kichapo kingine chochote cha Watch Tower kimefanya hapo awali.”

Kutoka Le Havre, Ufaransa, M. H. aliandika: “Ni lazima niseme kwamba kitabu hiki kilipita kabisa matazamio yangu; kiko wazi sana, ni sahihi, na kinapendeza macho. Maridadi!”

H.  W. W. kutoka Texas, U. S. A., aliandika: “Kitabu hiki kilikuwa chenye kupendeza na chenye kuvuta fikira sana, hata singeweza kukiweka chini. Nilijipata nikikisoma hadi usiku sana. Aina ya uandikaji wake ni bora. Kitabu hicho kinazungumzia itikadi za watu wengine kwa njia ya kiasi na yenye staha, huku kikiwatia moyo waendelee kumtafuta Mungu wa kweli, Yehova. Na maneno yacho yanasemwa kwa njia ya kuvutia sana mtu binafsi, kana kwamba mtu yuko kando yako akifanya mazungumzo nawe.”

Wenzi wa ndoa kutoka Panama, G. na S., walisema: “Watu wenye kuongea Kihispania wanakikubali kitabu kwa utayari. Wanasisimuliwa na picha zenye rangi za mahekalu na sanamu.”

D. M., baharia wa Wanajeshi wa bahari katika U. S. aliandika: “Nilikutana na mwanamke siku moja ambaye alisema, ‘Unataka kitabu cha kiroho?’ nami nikasema, ‘Ndiyo,’ bila kujua kilikuwa kitabu cha aina gani. Kwa mshangao wangu kilikuwa kitabu ambacho kwa muda fulani nilikuwa nimekuwa nikikitafuta.”

Profesa ambaye amefundisha juu ya dini katika chuo kikuu cha Amerika aliandika: “Maelezo yaliyo wazi na usahihi wa ujumla wa mafundisho ya dini mbalimbali ni yenye kuvutia. Kutajwa kwa waandishi wengi wenye kutambuliwa kunaonyesha wazi kwamba mtungaji anajua habari za uanachuo na wakati huu na matumizi yazo. Kina unyofu kamili na mambo hayasemwi kwa kufichafichwa.”

Msichana mchanga, N. Y., aliandika kutoka Jiji la Nagoya, Japan: “Nina umri wa miaka 12 na najifunza historia shuleni. Kitabu hiki kinashughulika na dini za Kijapani kwa undani. Pia, nilifurahia kusoma juu ya mizungu na upashanaji habari na roho waovu katika sura ya 4 na ‘Kumrudia Mungu wa Kweli’ katika sura ya 15.”

Barua nyingine nyingi zenye uthamini zimepokewa kutoka Argentina, Colombia, Uingereza, Puerto Riko, na Uhispania na nchi nyingine pia. ‹cThis last sentence left out on purpose.c›

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki