Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 6/15 kur. 25-26
  • ‘Tamaa Inayochochea Moyo na Akili’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Tamaa Inayochochea Moyo na Akili’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sayansi Inayoeleweka
  • Kumjua Muumba Vizuri Zaidi
  • Muumba Wetu Mtukufu Hutujali!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Kitabu Kipya Chawasisimua Mamilioni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Muumba Wako—Jifunze Jinsi Alivyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • ‘Sijapata Kusoma Cho Chote Kinachofanana Nacho’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 6/15 kur. 25-26

‘Tamaa Inayochochea Moyo na Akili’

“Hata sina maneno ya kuelezea shangwe na msisimuko ninaozidi kupata ninapoendelea kufurahia kusoma kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Kinakuza tamaa ndani ya mtu—naam, uhitaji—wa kujua mengi zaidi. Asanteni kwa kuwasha tamaa inayochochea moyo wangu na akili yangu.”

HIVYO ndivyo mmoja wa Mashahidi wa Yehova wa North Carolina, Marekani, alivyohisi kuhusu kitabu kilichotolewa na Watch Tower Society kwenye Mikusanyiko ya Wilaya ya “Njia ya Mungu ya Maisha” katika kipindi cha 1998/1999. Hata kama huna kitabu hicho, tafadhali ona jinsi wengine wanavyoeleza.

Siku kadhaa baada ya kupokea kitabu hicho kwenye mkusanyiko wa San Diego, California, Marekani, mtu mmoja aliandika: “Naona kitabu hiki ni chenye kuimarisha imani sana. Kinafanya nithamini sana kazi za uumbaji za Yehova. Nimefikia ukurasa wa 98, na naogopa nisifikie mwisho! Kinaridhisha jinsi hiyo.”

Mwanamke mmoja wa nchi za Mashariki aliandika: “Msemaji wa mkusanyiko alitumia maneno ‘kitabu cha kipekee,’ na maneno hayo kwa kweli yanafafanua yaliyomo. Sehemu yenye kutokeza ni kwamba kitabu hiki hakimsukumi msomaji aamini kuna Mungu, bali kinataja tu mambo ya hakika.”

Mambo ya hakika yanatia ndani uvumbuzi wa kisayansi wenye kuvutia kuhusu ulimwengu wetu, uhai, na sisi. Jambo hilo lilivutia wengi. “Hata nashindwa kueleza jinsi ambavyo kitabu hiki kimenigusa moyo sana,” mwanamke mmoja wa California akaandika. “Nilishindwa kuacha kukisoma kwa kuwa kila ukurasa ulifafanua uvumbuzi zaidi kuhusu ulimwengu wetu na maisha yenyewe. Nilijifunza mengi sana! Nitathamini kitabu hiki kidogo na kukionyesha watu wengi kadiri iwezekanavyo.”

Sehemu iliyowafurahisha wengi ni jinsi kitabu hiki kinavyotoa muhtasari wa Biblia, kikikazia utu wa Muumba. “Muhtasari wa Biblia, ambao umetolewa katika sehemu ya mwisho-mwisho ya kitabu hicho, ni mmojawapo wa mihtasari bora ambayo nimepata kusoma,” ndivyo wengi waelezavyo. Punde tu baada ya mkusanyiko mmoja uliofanywa mapema jijini New York, Marekani, mwanamke mwingine aliandika hivi: “Ni lazima kitabu hiki kipya kiwe kichapo chenye kunasa akili zaidi ambacho mmepata kuchapa. Nilifurahia sana uthibitisho wa kisayansi kwamba kuna Muumba. Muhtasari mfupi wenyewe wa Biblia watosha kuelezea mambo yanayotajwa na kuchochea mtu aendelee kusoma.”

Sayansi Inayoeleweka

Habari za kisayansi zilizo katika sura za mwanzo huenda zikaonekana kuwa ngumu sana, lakini yafuatayo ni maelezo ya wengi.

Mtu mmoja wa Kanada aliandika: “Ni tofauti kama nini na vitabu vya kiufundi ambavyo watungaji wake hujaribu kutuvutia kwa kutumia maneno makubwa-makubwa. Uandishi wenu ni wenye kutokeza kwa kufanya tuweze kuelewa kwa urahisi habari za fizikia, kemia, DNA, kromosomu, na kadhalika. Laiti mngaliandika vitabu vya mafundisho vinavyotumiwa kwenye vyuo vikuu ambavyo nilitumia miaka mingi iliyopita!”

Profesa wa fizikia wa chuo kikuu aliandika: “Kinaeleza masuala yanayohusika kwa njia ya wazi bila kuingilia mno mambo madogo-madogo ya kiufundi. Kitabu hiki kinasababu pamoja na msomaji na kunukuu wanasayansi wengi mashuhuri. Hiki ni kitabu ambacho ‘ni lazima kisomwe’ na mtu yeyote ambaye anapenda kujua chanzo cha ulimwengu na uhai, awe mwanasayansi au mtu wa kawaida.”

Mwanamke mmoja mchanga ambaye anafanya mtaala wa uuguzi alisema hivi: “Sikuamini nilipofungua sura ya 4 na kusoma nukuu ya kitabu ambacho tunatumia darasani! Nilimpa profesa wetu kitabu hicho nikamwambia kwamba najua angefurahia habari zake. Nikamwonyesha ukurasa wa 54 kuhusu ubongo. Alisoma kimoyomoyo kisha akasema, ‘Kinapendeza! Nitakisoma.’”

Mbunge mmoja nchini Ubelgiji aliandika hivi: “Kilichonivutia na kunipendeza ni maelezo ya kisayansi ambayo yanakazia kwamba sayansi ya kisasa haipingi dokezo la Biblia la kwamba kuna Mungu mmoja, bali zinakubaliana. Huo ni mtazamo muhimu sana.”

Kumjua Muumba Vizuri Zaidi

Kitabu hicho kilisaidia watu katika nchi nyingi kumjua Mungu vizuri zaidi na kufanya wahisi kuwa karibu zaidi naye. Msomaji mmoja katika Fukuoka City, nchini Japani, alisema: “Ni kana kwamba kwa mara ya kwanza Yehova alifafanuliwa vizuri zaidi. Kitabu hiki kinasadikisha sana. Nilipata kumjua Yehova kwa njia ambayo sikuwa nimewazia kamwe.” Mtu mmoja wa El Salvador aliandika: “Mnaeleza wazi jinsi Mungu alivyo mwenye huruma, asiye mwepesi wa hasira, na mwingi wa rehema. Kwa kweli, hayo ndiyo mambo tunayohitaji hasa ili tuweze kuwa karibu zaidi na yeye na Mwana wake. Ndicho kitabu cha kwanza kinachofafanua hisia za Yehova na hisia za kibinadamu za Mwana wake, Yesu.” Na msomaji mmoja nchini Zambia alisema: “Nilianza kumwona Yehova kwa njia tofauti kabisa.”

Basi inaeleweka kwamba Mashahidi wa Yehova wamesisimuka kuhusu kuwaonyesha wengine kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Mwanamke mmoja alisema: “Nilipokuwa nikimaliza kusoma sura ya 10 [“Ikiwa Muumba Anajali, Mbona Wanadamu Wanateseka Sana?”], nilishtuka nimesema kwa sauti, ‘Hiki ndicho kitabu hasa tunachohitaji Japani!’ Ningependa nifahamu vizuri habari iliyo kwenye sura hii na kuitumia zaidi na zaidi katika huduma ya shambani.” Mwanamke mwingine anajifunza Biblia na msichana mmoja aliyelelewa kwenye hekalu ambako babake alikuwa kuhani. “Imekuwa vigumu sana kwake kukubali wazo la kwamba kuna Muumba. Kitabu hiki hakisisitizi mambo, lakini kina mambo ya hakika, basi nafikiri kwamba hata Wabudha wanaweza kukisoma bila kusita. Kinatufanya tuhisi hata zaidi upendo wa Yehova.”

Uchanganuzi ufuatao ulitoka Uingereza: “Nimetoka tu kumaliza kusoma kitabu cha Muumba na ninataka kuanza kukisoma tena. Ni kitabu kizuri kama nini! Mtu yuampenda tu Yehova akikisoma. Nimempa jirani yangu kitabu kimoja, ambaye baada ya kusoma sura mbili tu alisema: ‘Siwezi kuacha kukisoma, kinasisimua sana.’ Nina hakika kitawasaidia watu wapate kumjua Muumba wetu Mtukufu na kumpenda.”

Mtu mmoja wa Maryland, Marekani, alisema: “Kwa kweli kimechochea hali yangu ya kiroho! Napangia kuwapa watu wote ninaoshughulika nao kikazi kitabu hiki. Nyakati nyingine mimi huona ugumu wa kuanza kutolea ushahidi watu kama hao wenye shughuli nyingi na wenye elimu. Nikiwa na kitabu hiki sasa nitapata njia nzuri na yenye kuvutia ya kuwafikia watu.”

Kwa wazi, kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? kitagusa mioyo ya watu duniani pote.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 25]

Picha ya jalada juu, Eagle Nebula: J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki