Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 4/15 kur. 14-20
  • Wewe Utaiga Rehema Ya Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wewe Utaiga Rehema Ya Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Haki ya Kimungu Yatekelezwa
  • Haki Ikisawazishwa na Rehema
  • Hangaiko kwa Kilichopotezwa
  • Shangilio la Kimbingu—Juu ya Nini?
  • Toba na Rehema Katika Kitendo
  • Yehova—Chanzo cha Haki na Uadilifu wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Mwige Yehova—Dhihirisha Haki na Uadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Haki Karibuni kwa Ajili ya Mataifa Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kushangilia Mtenda Dhambi Anapotubu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 4/15 kur. 14-20

Wewe Utaiga Rehema Ya Mungu?

“Mfuateni [mwigeni, NW] Mungu, kama watoto wanaopendwa.”—WAEFESO 5:1.

1. Ni kwa nini kuwaiga wengine kunapasa kuwa hangaiko kwa sisi sote?

WATU walio wengi huwaiga wengine kwa mazuri au kwa mabaya. Wale tunaowazunguka, na ambao huenda tukawaiga, wanaweza kutuathiri kwa kadiri kubwa. Mwandikaji wa Mithali 13:20 aliyepuliziwa roho alionya hivi: “Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; bali rafiki wa wapumbavu ataumia.” Basi, kwa sababu nzuri, Neno la Mungu linasema hivi: “Usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu.”—3 Yohana 11.

2. Tunatakiwa tumwige nani, na katika njia zipi?

2 Tuna mifano mizuri sana ya wanaume na wanawake ambao tunaweza kuiga. (1 Wakorintho 4:16; 11:1; Wafilipi 3:17) Hata hivyo, wa kwanza apaswaye kuigwa nasi ni Mungu. Katika Waefeso 4:31–5:2, baada ya kuonyesha tabia na mazoea ambayo tunapaswa kuepuka, mtume Paulo alihimiza kwamba tuwe ‘wenye huruma, tukisameheana.’ Hiyo iliongoza kwenye himizo lililo kubwa: “Hivyo mfuateni [mwigeni, NW] Mungu, kama watoto wanaopendwa; mkaenende katika upendo.”

3, 4. Mungu aliandaa maelezo gani juu yake mwenyewe, na kwa nini tunapaswa kukaza fikira juu ya kuwa kwake Mungu mwenye haki?

3 Njia na sifa za Mungu tunazopaswa kuziiga ni zipi? Kuna sehemu nyingi za utu na matendo yake, kama inavyoonwa kutokana na jinsi alivyojieleza kwa Musa: “BWANA [Yehova, NW], Mungu mwingi wa huruma [rehema, NW], mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma [fadhili zenye upendo, NW] watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao.”—Kutoka 34:6, 7.

4 Kwa kuwa Yehova “huzipenda haki [uadilifu, NW] na hukumu [haki, NW],” sisi tunashurutishwa kujua na kuiga upande huu wa utu wake. (Zaburi 33:5; 37:28) Yeye ndiye Muumba, na pia Hakimu na Mfanya-Sheria wa ainabinadamu aliye mkuu, kwa hiyo huonyesha haki kuelekea wote. (Isaya 33:22) Hiyo inaonyeshwa wazi katika njia ambayo alitaka haki na kuifanya itekelezwe miongoni mwa watu wake Waisraeli na baadaye katika kundi la Kikristo.

Haki ya Kimungu Yatekelezwa

5, 6. Haki ilionyeshwaje katika shughuli za Mungu pamoja na Israeli?

5 Alipokuwa akichagua Waisraeli kuwa watu wake, Mungu aliuliza kama ‘wangetii sauti yake kweli kweli, na kulishika agano lake.’ Walipokuwa wamekusanyika chini ya Mlima Sinai, walijibu hivi: “Hayo yote aliyoyasema BWANA [Yehova, NW] tutayatenda.” (Kutoka 19:3-8) Ni daraka lenye uzito kama nini! Kwa njia ya malaika, Mungu aliwapa Waisraeli amri 600 hivi, ambazo wao wakiwa taifa lililojiweka wakfu kwake, walikuwa na daraka la kuzishika. Vipi ikiwa mtu hangefanya hivyo? Mwenye maarifa katika Sheria ya Mungu alieleza hivi: “Lile neno lililonenwa na malaika lilikuwa imara, na kila kosa na uasi ulipata ujira wa haki.”—Waebrania 2:2.

6 Ndiyo, Mwisraeli ambaye hangetii alipata “ujira wa haki,” si hukumu ya kibinadamu yenye upungufu, bali hukumu kutoka kwa Muumba wetu. Mungu aliweka masharti ya adhabu za aina mbalimbali kwa ajili ya kuvunja sheria. Adhabu iliyokuwa yenye uzito sana ilikuwa ya ‘kukatiliwa mbali,’ au kuuawa. Hiyo ilitumika katika mivunjo mizito ya sheria, kama ibada-sanamu, uzinzi, kufanya ngono na watu wa ukoo, kufanya ngono na wanyama, kufanya ngono ya jinsia moja, kutoa watoto kuwa dhabihu, kuua, na utumizi mbaya wa damu. (Walawi 17:14; 18:6-17, 21-29) Tena, Mwisraeli yeyote ambaye alivunja sheria yoyote ya kimungu kwa kusudi, bila kutubu, ‘angekatiliwa mbali.’ (Hesabu 4:15, 18; 15:30, 31) Haki hiyo ya kimungu ilipotekelezwa, matokeo yangeweza kuonwa na wazao wa mtenda mabaya vile vile.

7. Baadhi ya matokeo ya kutekelezwa kwa haki miongoni mwa watu wa kale wa Mungu yalikuwa gani?

7 Adhabu kama hizo zilikazia uzito wa kuvunja sheria ya kimungu. Kwa mfano, ikiwa mwana alikuja kuwa mlevi na mlafi, alitakiwa aletwe mbele ya mahakimu waliokomaa. Ikiwa walipata kwamba alikuwa mtenda mabaya wa kusudi, asiyetubu, wazazi wangeshiriki katika kutekeleza haki. (Kumbukumbu 21:18-21) Wale walio wazazi miongoni mwetu wanaweza kujua kwamba haikuwa rahisi kufanya hivyo. Hata hivyo Mungu alijua kwamba hiyo ilihitajiwa ili uovu usienee miongoni mwa waabudu wa kweli. (Ezekieli 33:17-19) Hiyo ilipangwa na Yule ambaye inaweza kusema hivi juu yake: “Njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili.”—Kumbukumbu 32:4.

8. Haki ilitiaje alama shughuli za Mungu pamoja na kundi la Kikristo?

8 Baada ya karne nyingi Mungu alikataa taifa la Israeli na akachagua kundi la Kikristo. Lakini Yehova hakubadilika. Bado alishikamana na haki na angeweza kuelezwa kuwa “moto ulao.” (Waebrania 12:29; Luka 18:7, 8) Kwa hiyo aliendelea kuwa na uandalizi wa kutia hofu ya kimungu katika kundi zima kwa kuwaondoa watenda mabaya. Wakristo waliojiweka wakfu ambao walikuja kuwa watenda mabaya wasiotubu walitakiwa watengwe na ushirika.

9. Kutenga na ushirika ni nini, nako kunatimiza nini?

9 Ni nini inatiwa ndani katika kutenga na ushirika? Tunapata funzo la jambo hilo katika jinsi tatizo lilivyoshughulikiwa katika karne ya kwanza. Mkristo katika Korintho aliingia katika ukosefu wa adili pamoja na mke wa baba yake na hakutubu, kwa hiyo Paulo aliagiza kwamba aondolewe kutoka kundi hilo. Hiyo ilipasa ifanywe ili kulinda usafi wa watu wa Mungu, kwa ajili “chachu kidogo hulichachusha donge zima.” Kumwondoa kungezuia uovu wake usiaibishe Mungu na watu Wake pia. Nidhamu kali ya kutengwa na ushirika huenda pia ikamshtua ili apate akili tena na kutia ndani yake na ya kundi hofu ya Mungu ipasayo.—1 Wakorintho 5:1-13; Linganisha Kumbukumbu 17:2, 12, 13.

10. Mtu anapotengwa na ushirika watumishi wa Mungu wanatakiwa waitikieje?

10 Amri ya kimungu ni kwamba mwovu akiondolewa, ni lazima Wakristo ‘wasichangamane kabisa na yeye, hata wasile naye.’a Hivyo, yeye amekatiliwa mbali na ushirika, kutia ndani na utendaji wa kijamii, pamoja na waaminifu washikamanifu ambao huheshimu na hutaka kutembea kulingana na sheria ya Mungu. Wengine wao huenda wakawa watu wa ukoo nje ya familia ya karibu, si sehemu ya watu wa nyumba iyo hiyo. Huenda ikawa vigumu kwa watu wa ukoo huo kutumia amri hii ya kimungu, hata jinsi isivyokuwa rahisi kwa wazazi Waebrania chini ya Sheria ya Kimusa kushiriki katika kumwua mwana mwovu. Hata hivyo, amri ya Mungu iko wazi; hivyo tunaweza kuwa na uhakika kwamba kutenga na ushirika ni jambo la haki.—1 Wakorintho 5:1, 6-8, 11; Tito 3:10, 11; 2 Yohana 9-11; Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1982, kurasa 18-24; Aprili 15, 1988, kurasa 28-31.

11. Sehemu tofauti-tofauti za utu wa Mungu zingekuja kuonyeshwaje kuhusiana na kutenga na ushirika?

11 Hata hivyo, kumbuka kwamba Mungu wetu si mwenye haki tu; yeye pia ni “mwingi wa rehema [fadhili zenye upendo, NW], mwenye kusamehe uovu na makosa.” (Hesabu 14:18) Neno lake linaonyesha wazi kwamba mtu aliyetengwa na ushirika anaweza kutubu, akitafuta msamaha wa kimungu. Halafu nini? Waangalizi wenye ujuzi wangekutana naye ili kuamua kwa sala na kwa uangalifu kama anatoa ushuhuda wa kuwa na toba juu ya kitendo kibaya kilichoongoza kwenye kutengwa kwake na ushirika. (Linganisha Matendo 26:20.) Ikiwa ndivyo, aweza kurudishwa kundini, kama vile 2 Wakorintho 2:6-11 inavyoonyesha ilitokea kwa yule mwanamume katika Korintho. Hata hivyo, wengine ambao wameondolewa wamekuwa mbali na tengenezo la Mungu kwa miaka mingi, kwa hiyo je! kuna jambo lolote ambalo linaweza kufanywa ili kuwasaidia waione njia ya kurudi?

Haki Ikisawazishwa na Rehema

12, 13. Kwa nini kuiga kwetu Mungu kunapasa kutia ndani zaidi ya kuonyesha haki yake?

12 Mambo yaliyotangulia yameshughulika hasa na upande mmoja wa sifa za Mungu, jinsi ilivyotajwa katika Kutoka 34:6, 7. Hata hivyo, mistari hiyo inaorodhesha mengi zaidi ya haki ya Mungu, na wale ambao wanataka kumwiga hawakazii kutekeleza haki tu. Ikiwa ulikuwa unatengeneza mfano wa hekalu lililojengwa na Solomoni, je, ungejifunza juu ya moja tu ya nguzo zalo? (1 Wafalme 7:15-22) Sivyo, kwa kuwa hiyo haingekupa hata kidogo, picha iliyosawazika ya umbo wala kazi ya hekalu. Vivyo hivyo, ikiwa tunatamani kumwiga Mungu, tunahitaji kuiga pia njia na sifa zake nyingine, kama vile kuwa kwake “mwingi wa huruma [rehema, NW], mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma [fadhili zenye upendo, NW] watu elfu elfu, mwenye kusamehe.”

13 Rehema na msamaha ni sifa za msingi za Mungu, vile tunavyoona kutokana na jinsi alivyoshughulika pamoja na Israeli. Mungu wa haki hakuwaondolea adhabu kwa ajili ya kosa la kurudiwa-rudiwa, hata hivyo alionyesha rehema na msamaha wa kutosha. “Alimjulisha Musa njia zake, wana wa Israeli matendo yake. BWANA [Yehova, NW] amejaa huruma [rehema, NW] na neema, haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili [fadhili zenye upendo, NW]. Yeye hatateta sikuzote, wala hatashika hasira yake milele.” (Zaburi 103:7-9; 106:43-46) Ndiyo, mtazamo wa shughuli zake mamia ya miaka yaliyopita unathibitisha maneno hayo kuwa ya kweli.—Zaburi 86:15; 145:8, 9; Mika 7:18, 19.

14. Yesu alionyeshaje kwamba aliiga rehema ya Mungu?

14 Kwa kuwa Yesu Kristo “ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake,” tungetazamia kwamba angeonyesha rehema na utayari huo huo wa kusamehe. (Waebrania 1:3) Alifanya hivyo, kama vile matendo yake kuwaelekea wengine yanavyoonyesha. (Mathayo 20:30-34) Alikazia rehema kwa maneno yake tunayosoma katika Luka sura ya 15. Vielezi vitatu vilivyopo vinathibitisha kwamba Yesu alimwiga Yehova, na vinaandaa mafunzo ya maana kwetu.

Hangaiko kwa Kilichopotezwa

15, 16. Ni nini kilimchochea Yesu kutoa vielezi vilivyo katika Luka 15?

15 Vielezi hivyo vinashuhudia upendezi wa Mungu wenye rehema katika watenda dhambi, vikituonyesha picha inayopatana kwa ajili yetu kuiga. Angalia vikao vya vielezi hivi: “Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. Mafarisayo na waandishi wakanung’unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao.”—Luka 15:1, 2.

16 Wote waliohusika walikuwa Wayahudi. Mafarisayo na waandishi walijivunia kushikilia kwao sana Sheria ya Kimusa kwa kudhania tu, namna ya uadilifu wenye kujihesabia haki. Hata hivyo, Mungu hakukubali uadilifu huo wa mtu kujitangaza binafsi. (Luka 16:15) Kwa wazi, watoza ushuru waliotajwa walikuwa Wayahudi ambao walikusanya kodi kwa ajili ya Roma. Kwa sababu wengi wao walitoza fedha zilizozidi kutoka kwa Wayahudi wenzao, watoza ushuru walikuwa kikundi kilichodharauliwa. (Luka 19:2, 8) Waliwekwa kikundi kimoja na “wenye dhambi,” ambacho kilikuwa ni kutia ndani watu wenye kukosa maadili, hata makahaba. (Luka 5:27-32; Mathayo 21:32) Lakini Yesu aliwauliza viongozi wa kidini wenye kulalamika:

17. Kielezi cha Yesu cha kwanza katika Luka 15 kilikuwa nini?

17 “Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi. Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.” Viongozi wa kidini wangeweza kufahamu mfano huo, kwa ajili kondoo na wachungaji walikuwa mwono wa kikawaida. Kwa kuhangaishwa, mchungaji aliacha kondoo 99 kulisha katika malisho ambayo walizoea huku akienda kutafuta-tafuta aliyepotea. Akifuliza mpaka akampata, alimbeba kwa wororo kondoo yule mwenye kuogopa akamrudisha kwenye kundi.—Luka 15:4-7.

18. Ni nini kilichotokeza kushangilia, jinsi inavyokaziwa katika kielezi cha Yesu cha pili katika Luka 15?

18 Yesu aliongeza kielezi hiki cha pili: “Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi [drakma, NW] kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi [drakma, NW] ile iliyonipotea. Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.” (Luka 15:8-10) Thamani ya drakma hiyo ilikuwa karibu mshahara wa siku moja wa mfanya kazi wa kibarua. Sarafu ya mwanamke huyo huenda ikawa ilikuwa mali ya urithi isiyoweza kutolewa wala kuuzwa, au huenda ikawa ilikuwa kifungu kimoja kilichofanyizwa kuwa kito. Wakati ilipopotea, alitafuta kwa bidii ili apate sarafu hiyo, halafu yeye na rafiki zake wanawake wakashangilia. Hiyo inatuambia jambo gani juu ya Mungu?

Shangilio la Kimbingu—Juu ya Nini?

19, 20. Vielezi vya kwanza viwili vya Yesu katika Luka 15 vilikuwa juu ya nani hasa, na vilikazia jambo gani?

19 Vielezi viwili hivyo vilikuwa itikio la uchambuzi kwa Yesu, ambaye miezi kadhaa ya mapema alikuwa amejitambulisha kuwa “mchungaji mwema” ambaye angetoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo zake. (Yohana 10:11-15) Hata hivyo, vielezi hivyo havikuwa juu ya Yesu hasa. Masomo ambayo waandishi na Mafarisayo walihitaji kujifunza yalikazia mwelekeo na njia za Mungu. Hivyo, Yesu alisema kwamba kuna shangwe mbinguni juu ya mtenda dhambi anayetubu. Wanadini hao walidai kwamba walimtumikia Yehova, hata hivyo hawakuwa wakimwiga. Kwa upande mwingine njia zenye rehema za Yesu, ziliwakilisha mapenzi ya Baba yake.—Luka 18:10-14; Yohana 8:28, 29; 12:47-50; 14:7-11.

20 Ikiwa moja kati ya mia ilikuwa msingi wa shangwe, sarafu moja kati ya kumi ilikuwa hivyo hata zaidi. Hata leo, tunaweza kuona maono ya moyoni ya wanawake waliokuwa wanashangilia kupata ile sarafu! Hapa pia, somo lakazia mbingu, kwa kuwa “malaika wa Mungu” wanashangilia pamoja na Yehova “kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.” Angalia neno hilo la mwisho, “atubuye.” Vielezi hivyo vilikuwa juu ya watenda dhambi ambao wanatubu. Na unaweza kuona kwamba vyote viwili vilikazia jinsi inavyofaa kuwa na shangwe juu ya kutubu kwao.

21. Tunapaswa kujifunza nini kutokana na vielezi vya Yesu katika Luka 15?

21 Wale viongozi wa kidini walioongozwa vibaya ambao walijivuna juu ya kushikilia Sheria kijuujuu tu walikosa kuona Mungu kuwa “mwingi wa huruma [rehema, NW], mwenye fadhili, . . . mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi.” (Kutoka 34:6, 7) Kama wangalikuwa wakiiga sehemu hiyo ya njia na utu wa Mungu, wangalithamini rehema ya Yesu kuwaelekea watenda dhambi ambao walitubu. Ni jinsi gani na sisi? Je, tunafikiria sana somo hilo na kulitumia? Basi, angalia kielezi cha Yesu cha tatu.

Toba na Rehema Katika Kitendo

22. Kwa ufupi, Yesu alitoa kielezi kipi cha tatu katika Luka 15?

22 Mara nyingi hicho kimeitwa kielezi cha mwana mpotevu. Hata hivyo, katika kukisoma huenda ukaona ni kwa nini wengine hukiona kuwa mfano wa upendo wa baba. Kinasema juu ya mwana mchanga zaidi katika familia, ambaye atwaa urithi wake kutoka kwa baba yake. (Linganisha Kumbukumbu 21:17.) Mwana huyo aondoka kwenda nchi ya mbali, ambapo atapanya mali yake yote katika ufasiki, alazimika kuanza kazi ya kuchunga nguruwe, na hata ashushwa kwenye hali ya kutamani chakula cha nguruwe. Hatimaye apata akili tena na aamua kurudi nyumbani, ili tu aweze kumfanyia baba yake kazi akiwa mfanya kazi ya kibarua aliyeajiriwa. Akaribiapo nyumbani, baba yake achukua hatua chanya (nzuri) ya kumkaribisha, hata kuwa na karamu. Kaka yake, ambaye alikuwa amebaki nyumbani akifanya kazi, achukizwa na rehema ambayo imeonyeshwa. Lakini baba asema kwamba wanapaswa kushangilia kwa sababu mwana aliyekuwa mfu sasa yu hai.—Luka 15:11-32.

23. Tunapaswa kujifunza nini kutokana na kielezi cha mwana mpotevu?

23 Huenda ikawa waandishi na Mafarisayo fulani waliona kwamba walikuwa wakifananishwa na mwana mkubwa zaidi, tofauti na watenda dhambi ambao walikuwa kama mwana mchanga zaidi. Hata hivyo, je, walipata jambo la maana lenye kutokeza la kielezi hicho, na sisi je? Kinakazia sifa yenye kutokeza ya Baba yetu wa kimbingu mwenye rehema, utayari wake kusamehe kwa msingi wa kutubu na kugeuka kwa moyoni kwa mtenda dhambi. Hiyo ingalipasa kuwasukuma wasikilizaji kuitikia kwa shangwe kufidiwa kwa watenda dhambi wenye kutubu. Hivyo ndivyo Yehova huona mambo na jinsi anavyotenda, na wale ambao humwiga hufanya vivyo hivyo.—Isaya 1:16, 17; 55:6, 7.

24, 25. Ni njia zipi za Mungu ambazo tunapaswa kuwa tukitafuta kuiga?

24 Kwa wazi, haki hutia alama njia zote za Mungu, kwa hiyo wale ambao wanataka kumwiga Yehova huthamini na kufuatia haki. Hata hivyo, Mungu wetu hachochewi na haki iliyowaziwa tu au yenye ugumu usiobadilika. Rehema na upendo zake ni kubwa. Anaonyesha hivyo kwa utayari wa kusamehe kwa msingi wa toba ya kweli. Basi, inafaa kwamba Paulo alilinganisha kusamehe kwetu na kuiga kwetu Mungu: “Mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi. Hivyo mfuateni [mwigeni, NW] Mungu, kama watoto wanaopendwa; mkaenende katika upendo.”—Waefeso 4:32–5:2.

25 Wakristo wa kweli wamejaribu kwa muda mrefu kuiga haki ya Yehova na pia rehema yake na utayari wake wa kusamehe. Tunapokuja kumjua zaidi, inapasa kuwa rahisi zaidi kwetu kumwiga katika njia hizo. Lakini, tungeweza kutumiaje hilo kuelekea mtu ambaye amepokea nidhamu kali kihaki kwa sababu alifuatia mwendo wa dhambi? Na tuone.

[Maelezo ya Chini]

a “Kuondoa ndani ya shirika katika maana yayo ya kawaida ni kitendo cha kusudi ambacho kwacho kikundi kinawanyima wale ambao kwa wakati mmoja walikuwa washirika wenye sifa nzuri, mapendeleo ya ushirika wacho. . . . Katika wakati wa Kikristo kuondoa ndani ya ushirika kulikuja kurejezea tendo la kutohusisha ndani ambalo kwalo jamii ya kidini inawanyima watenda mabaya sakramenti, ibada za kikundi, na labda mwungano wa kijamii wa aina yoyote.”—The International Standard Bible Encyclopedia.

Umejifunza Nini?

◻ Haki ya Mungu ilionyeshwaje katika kundi la Israeli na katika kundi la Kikristo?

◻ Ni kwa sababu gani tuiige rehema ya Mungu, kuongezea na haki yake?

◻ Ni nini ilitokeza vile vielezi vitatu katika Luka sura ya 15, na vinapasa kutufunza jambo gani?

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Tambarare ya er-Raha mbele ya Mlima Sinai (mandhari-nyuma kushoto)

[Hisani]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 15]

Garo Nalbandian

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 18]

Garo Nalbandian

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki