Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 7/1 kur. 20-23
  • ‘Kuishi kwa Kukaribisha Akilini Siku ya Yehova’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kuishi kwa Kukaribisha Akilini Siku ya Yehova’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utumishi wa Betheli
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Barabarani
  • Napata Mwenzi
  • Kuwa Shahidi wa Baraka ya Yehova
  • Kutazamia Siku ya Yehova Bado
  • Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Mambo Niliyotimiza Katika Utumishi wa Wakati Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Maisha Yenye Kuthawabisha Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maisha Yangu Katika Tengenezo la Yehova Lenye Kuelekezwa kwa Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 7/1 kur. 20-23

‘Kuishi kwa Kukaribisha Akilini Siku ya Yehova’

KAMA ILIVYOSIMULIWA NA LYLE REUSCH

KUTOKANA na kumbukumbu langu la mapema zaidi, maisha yetu ya familia yalizungukia imani imara katikaulimwengu mpya wenye uadilifu unaokuja. Mamangu na Babangu walikuwa wanatusomea sisi watoto kutoka katika Biblia juu ya “mbingu mpya na dunia mpya”na juu ya‘ng’ombe na dubu wakilisha pamoja, simba akila majani kama ng’ombe,na mtoto mdogo akiwaongoza.’ Waliifanya iwe halisi sana,hivi kwamba nilijiwazmwenyewe kuwa huyo mtoto mdogo.—2 Petro 3:11-13, HNWW; Isaya 11:6-9, UV. KUTOKANA na kumbukumbu langu la mapema zaidi, maisha ya familia yetu yalizungukia imani imara katika ulimwengu mpya wenye uadilifu unaokuja. Mamangu na Babangu walikuwa wanatusomea sisi watoto kutoka katika Biblia juu ya “mbingu mpya na dunia mpya” na juu ya ‘ng’ombe na dubu wakilisha pamoja, simba akila majani kama ng’ombe, na mtoto mdogo akiwaongoza.’ Waliifanya iwe halisi sana, hivi kwamba nilijiwaza mwenyewe kuwa huyo mtoto mdogo.—2 Petro 3:11-13, HNWW; Isaya 11:6-9, UV.

Katika miaka ya 1890 babu yangu, August Reusch, alijifunza kweli za msingi za Biblia kupitia kuandikiana barua na Charles T. Russel. Alihubiri sana sehemu ya kwao katika Eneo la Kaskazini-Magharibi mwa Kanada, sasa Yorkton, Saskatchewan. Tena na tena aliwashauri wana wake hivi: “Vijana, iweni waangalifu kuhusu 1914!” Kusadikishwa kwamba siku ya Yehova ilikuwa karibu kulimtia moyo baba yangu maono ya uharaka yaliyoendelea muda wa maisha yake yote nayo imekuwa njia ya maisha kwangu.

Mama na Baba walikuwa mfano bora wa ukaribishaji-wageni. Kikundi cha funzo la Biblia cha Saskatoon, Saskatchewan, Eklesia (Kundi) ya Wanafunzi wa Biblia kilikutana kwa ukawaida nyumbani mwetu. Wahudumu wasafirio (waliokuwa wakiitwa mapilgrimu) mara nyingi walikaa nyumbani mwetu. Ndugu yangu, Verne, na dada yangu, Vera, nami tulifaidika kiroho. Wakati wote kulikuwako maono ya uhalisi juu ya ujumbe wa Ufalme na uhitaji wa uharaka wa kuambia wengine juu yao. (Mathayo 24:14) Sikuwa nimeng’amua kwamba katika miaka ijayo ningekuwa nikitumia sehemu kubwa ya maisha yangu nikiendelea na kazi ya mapilgrimu hao kwa kutumikia nikiwa mwangalizi asafiriye wa Mashahidi wa Yehova.

Katika 1927, Baba alihamisha familia kwenda Berkeley, California. Halafu, wakati wa upeo wa upungufu wa kifedha katika 1933, nilihitimu shule ya sekondari. Ndugu yangu, Verne, nami tulijiona kuwa wenye pendeleo kupata kazi katika kiwanda cha Kampuni ya Gari Aina ya Ford katika Richmond, California. Hata hivyo, siku moja katika masika ya 1935, nilifikiria hivi: ‘Ikiwa ni lazima nifanye kazi kwa bidii, ingefaa zaidi ikiwa ningefanya kazi kwa bidii kwa jambo linalostahili.’ Siku hiyo nilijiuzulu, na siku ifuatayo niliandikia makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova, katika Brooklyn, New York, ili kupata fomu ya kuomba kutumikia Betheli. Baada ya kuhudhuria mkusanyiko wenye kusisimua katika Washington, D. C., katika Juni 1935, nilikubaliwa katika utumishi wa Betheli.

Utumishi wa Betheli

Msimamizi wa kiwanda, Nathan Knorr, alinipa kazi katika kudumisha jengo. Mimi pekee ndiye niliyekuwa katika idara hiyo. Nikiwa kijana wa miaka 20, nilijisikia kuwa mtu wa maana sana. Niliweza kuzunguka-zunguka nilivyopenda katika kiwanda hicho, na hakuna yeyote aliyesaili juu ya kile nilichokuwa nikifanya. Ndugu Knorr alithamini jinsi nilivyokuwa nikifanya kazi yangu, lakini alitambua tatizo la mwelekeo wangu. Aliendelea kujitahidi kunipa mwongozo niweze kusitawisha unyenyekevu.

Hata hivyo, ilikuwa muda fulani, kabla ya mimi kung’amua kwamba Ndugu Knorr alikuwa akijaribu kweli kweli kunisaidia. Kwa hiyo niliomba radhi kwa mwelekeo wangu nami nikaonyesha azimio la kufanya vizuri zaidi. Huo ulikuwa mwanzo wa uhusiano mrefu wenye uchangamfu pamoja na Ndugu Knorr, ambaye katika Januari 1942 akawa msimamizi wa tatu wa Watch Tower Society.

Zaidi ya kufanya kazi ya kudumisha, niliji-funza jinsi ya kuendesha mashine katika sehemu ya kuunganisha vitabu au kusaidia kuziendesha. Baada ya muda fulani nilifanya kazi ya ofisi, kuandika, na kupeleka maagizo ya kazi katika kiwanda. Misimu ya masika na kiangazi cha 1943 ilikuwa hasa nyakati za shughuli na za kusisimua. Ulimwengu ulikuwa kati ya Vita ya Ulimwengu 2, na Mashahidi wa Yehova walivumilia kuudhiwa, kukamatwa, na hukumu za kuwekwa gerezani na aina zote za kushtakiwa isivyo haki. Katika 1940 Mahakama Kuu Zaidi ya U.S. ilikuwa imeamuru kwamba shule zingeweza kushurutisha wanafunzi kusalimu bendera. Hiyo ilichochea wimbi la jeuri katika majimbo 44 kati ya 48 yaliyokuwapo. Watoto wa Mashahidi walifukuzwa kutoka shule, wazazi walikamatwa, na watu wenye ghasia walifukuza Mashahidi nje ya mji. Watu mmoja mmoja walipigwa risasi, wengine walipakwa lami na kuwekwa manyoya.

Mashahidi wa Yehova waliposhindana katika mahakama mbalimbali, karatasi nyingi zenye maamrisho ya mahakama, miswada ya kesi kutoka kwa mwanasheria, na hati zilizotolewa na wafanyakazi wa mambo ya kisheria wa Sosaiti zilipitia dawati langu ili zichapishwe. Sisi sote tulifanya kazi saa nyingi za ziada ili kutimiza kazi kwa wakati uliohitajiwa. Hukumu za Mahakama Kuu Zaidi zilizotokea katika Mei na Juni ya 1943—wakati kesi 12 kati ya 13 zilipoamuliwa kwa upande wa Mashahidi wa Yehova—zimekuja kuwa sehemu ya rekodi za matukio ya kila mwaka ya historia ya kisheria. Ninashukuru kuwa nimejionea jinsi Yehova alivyofungua njia katika kutetea habari njema na kuzithibitisha kisheria.—Wafilipi 1:7.

Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Katika njia fulani siku hizo hatukutayarishwa vizuri ili kutimiza kazi kubwa sana iliyotabiriwa kwenye Mathayo 24:14, yaani, ‘kuhubiri habari njema ya ufalme katika ulimwengu wote kabla ya mwisho kuja.’ Ndugu Knorr, akiwa msimamizi wa Sosaiti, aliona uhitaji wa programu ya kielimu. Pamoja na washiriki wa kiume wengine wa familia ya Betheli, nilipata mwaliko kujiandikisha katika “Masomo ya Maendeleo Katika Huduma ya Kitheokrasi.” Hiyo hatimaye ikawa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ambayo imekuwa yenye kutenda kazi katika makundi ya Mashahidi wa Yehova tangu 1943.

Tulikutana katika chumba cha mkutano cha familia ya Betheli Jumatatu jioni, Februari 16, 1942, na Ndugu Knorr akatoa hotuba ya maagizo ya kwanza. Habari yake ilikuwa “Hati-Mkono za Biblia.” Ndugu T. J. Sullivan alikuwa mwangalizi wa shule naye akatupa shauri ili kutusaidia tufanye maendeleo. Baada ya wakati fulani nilipewa mgawo huo wa kuwa mwangalizi wa shule, ambao niliuona kuwa pendeleo. Lakini kwa mara nyingine ilikuwa wakati wa nidhamu.

Nilikuwa nimekuwa mwenye kuchambua mno na kukosa heshima katika kumshauri ndugu mwenye umri mkubwa, kwa hiyo Ndugu Knorr akaniambia kwa uwazi: “Hakuna yeyote anayethamini unapotumia kifua hapa.” Alipokuwa ameeleza jambo hilo waziwazi na masikio yangu yakaiva vya kutosha kwa ajili ya aibu, macho makubwa yenye rangi ya kahawia ya Ndugu Knorr yakawa yenye upole. Kwa sauti ya upole, alisoma Zaburi 141:5: “Acha mwadilifu anipige kwa nguvu; litakuwa tendo la fadhili: na acha anikaripie; yatakuwa mafuta bora, ambayo hayatavunja kichwa changu.” (King James Version) Nimetumia andiko hilo mara nyingi wakati limekuwa daraka langu kutoa shauri la kusahihisha kwa wengine.

Kabla ya mwanzo wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, wachache wetu walikuwa na pendeleo la kuhutubu sana peupe. Ndugu Rutherford alipokufa, Ndugu Knorr alifanya bidii ili kusitawisha uwezo wake wa kusema. Chumba changu cha Betheli kilikuwa chini ya chake moja kwa moja, nami niliweza kumsikia akijizoeza hotuba yake. Kwa dazani halisi za nyakati, alisoma kwa sauti kubwa hotuba “Amani—Je! Inaweza Kudumu?” ambayo alitoa kwenye mkusanyiko wa Cleveland katika 1942.

Barabarani

Nilipokuwa nimetumikia Betheli miaka 13, Ndugu Knorr alinipa mgawo kutumikia shambani nikiwa mwangalizi wa wilaya. Alipokuwa ananiambia kwa ufupi juu ya mgawo wangu mpya, alisema hivi: “Lyle, sasa una nafasi ya kujionea moja kwa moja jinsi Yehova anavyoshughulika na watu wake.” Nikikumbuka hayo na nikiwa na masanduku mawili mikononi, siku ya Mei 15, 1948 nilianza kazi-maisha yangu nikiwa mwangalizi asafiriye. Kabla ya kuanza kazi ya wilaya, nilitumikia nikiwa mwangalizi wa mzunguko kwa miezi michache.

Shirika au kundi la kwanza, nililotumikia lilikuwa moja dogo lililokuwa la mashambani katika Waseca, Minnesota. Nilikuwa nimeandika mapema kwa Dick Cain, mtumishi wa shirika (kama vile mwangalizi-msimamizi alivyokuwa akiitwa wakati huo) anilaki kwenye gari-moshi. Alikuwa painia wa pekee, na ili kupunguza gharama, alikuwa tu amehama chumba chake cha kupanga, alipokuwa akikaa wakati wa kipupwe, akaingia chumba chake cha kiangazi, yaani hema. Hata hivyo, Mei katika Minnesota si wakati wa kiangazi barabara! Usiku huo, nikiwa natetemeka hemani, nilishangaa kama njia hiyo ya maisha ilinifaa. Nilipata homa kali ambayo iliendelea kwa majuma kadhaa, lakini niliendelea kuishi.

Wakati wa miaka hiyo ya mapema nilipokuwa nikizuru makundi na mizunguko tofauti, nilikaa katika nyumba za akina ndugu, na kuishi kwa vitu vilivyokuwa ndani ya sanduku langu tu. Nililala mahali pa namna zote, kutia na kulala kwenye sakafu jikoni, juu ya viti virefu vya sebule, katika vyumba vya orofa ya juu zaidi vyenye joto bila kupishwa kwa hewa safi. Nyakati nyingine nilikaa katika makao ambapo mshiriki wa familia alipinga imani zetu. Katika Wisconsin mume mmoja asiyeamini alinikodolea macho juma zima nilipokuwa nikija na kwenda. Alipokuja nyumbani usiku mmoja akiwa amelewa, nikamsikia akitisha “kumpiga huyo jamaa fulani,” nilikata kauli kwamba ilikuwa wakati wa kuondoka. Lakina maono magumu yalikuwa machache kwa ulinganifu na yaliongeza usisimuko katika mgawo wangu. Yalikuwa mambo ya kuleta ucheshi baadaye.

Napata Mwenzi

Nakumbuka vizuri. Kwenye kusanyiko la mzunguko katika Tiffin, Ohio, nilikutana na kibibi mrembo, mwenye macho ya kahawia, Leona Ehrman, wa kutoka Fort Wayne, Indiana. Yeye pia alikuwa amelelewa katika imani ya Kikristo na alikuwa amekuwa painia mwaminifu kwa miaka kadhaa. Kusafiri daima hakukufaa uchumba, lakini tulipashana habari kwa kuandikiana barua. Halafu katika 1952, niliuliza, “Je! utafanya?” naye akasema, “Ndiyo, nitafanya!” basi tukafanya. Tukafanya ndoa. Mara nyingi tumeulizwa kwa nini hatukutulia kuwa na makao na familia, lakini sisi husema kwamba tunayo familia—akina ndugu, akina dada, akina baba, na akina mama katika majimbo 44 hivi ambapo tumetumikia.—Marko 10:29, 30.

Wengine wameuliza, ‘Je! hamjapata kuchoka na kuhisi kama kutaka kuacha?’ Ndiyo, zaidi ya mara moja. Lakini kati yetu wawili, mmoja akishuka moyo mwingine humtia moyo. Wakati mmoja hata nilimwandikia ndugu yangu Verne, nikimwuliza juu ya uwezekano wa kufanya kazi pamoja naye katika biashara yake ya kupaka rangi. Alijibu kwamba alikuwa ametazamia jambo hilo mara nyingi kwa sababu tulikuwa wenzi wa karibu sana tulipokuwa tukikua. Hata hivyo, alinishauri nifikirie uamuzi wangu kwa uangalifu. Halafu nikakumbuka maneno ya Ndugu Knorr aliyorudia mara nyingi kwa washiriki wa familia ya Betheli: “Haihitaji bidii nyingi kuacha; inahitaji moyo mkuu na ushikamanifu wa maadili kuushikilia mgawo wako.” Hilo lilikuwa shauri zuri bado.

Hakuna mwangalizi yeyote aliyeoa ambaye angeweza kuushikilia mgawo wake kwa muda mrefu bila mke aliye mshikamanifu na mwenye kuunga mkono, kama vile Leona amethibitika kuwa kwangu. Utu wake wenye ujoto, wa upendo na mtazamo wake ulio mchangamfu daima katika makundi umemfanya apendwe na maelfu. Sichoki kamwe kumwambia kadiri ninavyompenda. Hilo, nina uhakika, linamsaidia kuishikilia kazi pia.

Kuwa Shahidi wa Baraka ya Yehova

Kazi kuu ya mwangalizi wa wilaya yahusu hasa kusanyiko la mzunguko, ambapo anatumikia kila juma akiwa mwenyekiti, msemaji kwa watu wote, na mwangalizi wa shule. Baraka ya Yehova juu ya mpango huu inathibitika kutokana na uhakika wa kwamba kati ya mamia ya makusanyiko ya mzunguko ambayo nimesimamia, hakuna hata moja lililokosa kufanywa. Ni kweli, mengine yalisumbuliwa, lakina hakuna hata moja lililofutwa.

Katika Wooster, Ohio, katika masika ya 1950, nilipokuwa nikitangaza wimbo wa kufunga kipindi cha Jumamosi usiku, kikundi cha wapinzani wenye ghasia zaidi ya elfu moja walikusanyika nje ya jumba la michezo ambapo kusanyiko lilikuwa likifanywa. Watu hao wenye ghasia walikuwa wameleta sanduku za mayai yaliyooza kututupia tulipokuwa tukiondoka. Kwa hiyo tuliamua hali na kuendeleza programu kwa nyimbo, mambo yaliyoonwa, na hotuba zisizotayarishwa mapema. Mashahidi wale 800 walibaki watulivu na wenye subira.

Saa 8:00  ya usiku, hali ya anga ilikuwa baridi sana. Kana kwamba kutayarisha kuondoka, wakaribishaji walitoa mabomba ya kuzimia moto na kuanza kuoshea mbali mayai yaliyokuwa yameanguka mbele ya mahali pa kutembea. Watu wenye ghasia wakakusanyika tena, wakitoka kwenye ujoto wa kituo cha basi kilichokuwa karibu. Lakini tendo la wakaribishaji hao lilielekeza kando fikira za watu hao, nasi tukaachilia wasikilizaji waondoke kimya kupitia mlango wa kuondokea wa nyuma. Wote walifikia magari yao salama. Kusumbuliwa na watu wenye ghasia kulitukia kwenye makusanyiko mengine ya Ohio, katika Canton, Defiance, na Chillicothe. Lakini ghasia ya watu wenye jeuri ilikuwa ikififia, na maamuzi ya Mahakama Kuu Zaidi ya U.S. yakiwa yanatuunga mkono yalianza kuwa na matokeo kwa walioasi sheria.

Baada ya wakati matatizo ya afya yakalazimisha badiliko. Kwa hiyo katika miaka ya katikati ya 1970, Sosaiti kwa fadhili ilinipa mgawo kutumikia nikiwa mwangalizi wa mzunguko katika eneo la kusini mwa California ambamo makundi yako karibu karibu, na vifaa vya kutunza afya vinapatikana kwa urahisi. Wakati wajibu mbalimbali wa mwangalizi wa wilaya unapohusisha kusafiri zaidi na kutunza na kusimamia mizunguko mingi, wajibu mbalimbali wa mwangalizi wa mzunguko unahusisha kupanga makusanyiko ya mzunguko na kugawa na kujizoeza sehemu za programu. Kuongezea hayo, Shule za Utumishi wa Painia zinahitaji kupangwa na kutumikiwa. Kwa hiyo kazi ya waangalizi wasafirio, iwe ya wilaya au ya mzunguko, ni kazi ya wakati wote, njia ya maisha yenye thawabu.

Kutazamia Siku ya Yehova Bado

Kutokana na kumbukumbu yangu ya mapema zaidi ya miaka zaidi ya 70 iliyopita, sikuzote nimehisi maoni ya uharaka. Sikuzote katika fikira zangu, Har–Magedoni imekuwa kesho kutwa. (Ufunuo 16:14, 16) Kama baba yangu, na baba yake kabla ya yeye, nimeishi maisha yangu kama mtume alivyohimiza, “kukaribisha akilini kuwapo kwa siku ya Yehova.” Sikuzote nimeuona ulimwengu mpya ulioahidiwa kuwa wa ‘hakika ingawa haujaonwa.’—2 Petro 3:11, 12, NW; Waebrania 11:1, NW.

Tazamio hilo lililosisitizwa kwangu kutoka uchanga litatimilizwa karibuni. “Ng’ombe na dubu watalisha pamoja,” “simba atakula majani kama ng’ombe,” na “mtoto mdogo atawaongoza.” (Isaya 11:6-9) Ahadi kama hizo zenye kuchangamsha moyo zinathibitishwa na maneno ya Yesu kwa Yohana kwenye Ufunuo 21:5: “Yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.”

[Picha of Lyle and Leona Reusch katika ukurasa wa 23]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki