Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 1/1 uku. 3
  • Umwabudu Mungu Yupi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Umwabudu Mungu Yupi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kutokea kwa Miungu Bandia
  • Kesi ya Mahakama ya Ulimwengu Wote Mzima Ambayo Inakuhusisha Wewe Ndani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Je! Wewe Utakuwa Shahidi kwa Ajili ya Yule Mungu wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Je, Kuna Mungu Mmoja Tu wa Kweli?
    Amkeni!—2006
  • Ni Mungu Yupi Ambaye Wewe Unapaswa Kuabudu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 1/1 uku. 3

Umwabudu Mungu Yupi?

TOFAUTI na wanyama, sisi binadamu tuna uwezo wa kuabudu. Hiyo ni sehemu ya sifa zetu tangu tunapozaliwa. Pia tuna ufahamu wa kiadili, dhamiri yenye kutuongoza kuhusu lililo jema na lililo baya. Katika njia mbalimbali sisi sote hufuata dhamiri hiyo, na katika kufanya hivyo, wengi humtegemea mungu au miungu fulani ili kupata mwongozo.

Muda wa karne moja au mbili zilizopita, wataalamu fulani wa kilimwengu wamebisha kuwapo kwa Mungu na Muumba mweza yote. Katika 1844, Karl Marx alitangaza dini kuwa “kasumba ya watu.” Baadaye, Charles Darwin alitokeza nadharia ya mageuzi. Kisha kukaja yale mapinduzi ya Bolshevik. Katika Ulaya Mashariki kutoamini kuna Mungu kukawa sera rasmi ya serikali, na ilidaiwa kwamba dini ingefifia na kizazi cha 1917. Lakini wale wasioamini kuna Mungu hawakuweza kubadili jinsi wanadamu walivyoumbwa. Hiyo inashuhudiwa na kurudi kwa dini katika Ulaya Mashariki wakati huu.

Hata hivyo, kama Biblia isemavyo, wako wengi “waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi.” (1 Wakorintho 8:5) Muda wa enzi zote zilizopita ainabinadamu imeabudu miungu wengi sana. Kumekuwa miungu wa uzazi, wa upendo, wa vita, na wa divai na karamu za mashindano ya ulevi na ulafi. Katika dini ya Kihindu pekee, hesabu ya miungu imefika mamilioni.

Miungu wa utatu wamesitawi katika Babuloni, Ashuru, na Misri, na pia katika nchi za Kibuddha. Jumuiya ya Wakristo pia ina Utatu wayo “mtakatifu.” Uislamu, unaokataa Utatu, hauna “mungu yeyote ila Allah.” Isitoshe, hata wale wanaodhihaki wazo la kuwapo kwa Mungu mweza yote asiyeonekana, wana miungu yao wenyewe. Kwa mfano, kwenye Wafilipi 3:19, Biblia husema juu ya wanadamu wanaonaswa katika ufuatiaji vitu vya kimwili: “Mungu wao ni tumbo.”

Watu walio wengi huabudu mungu au miungu wa nchi au jamii ambayo katika hiyo walipata kuzaliwa. Hilo latokeza maswali. Je! namna zote za ibada huongoza mahali pamoja—kama barabara kwenda hadi kilele cha milima? Au nyingi za barabara za kiroho za dini huongoza kwenye msiba—kama vijia viendavyo hadi genge? Je! kuna njia nyingine zinazofaa za kuabudu au kuna moja tu? Je! kuna miungu wengi wenye kustahili sifa au kuna Mungu Mweza Yote mmoja tu anayestahili ujitoaji na ibada yetu ya pekee?

Kutokea kwa Miungu Bandia

Maswali yaliyo juu hustahili uchunguzi wetu wa karibu. Kwa nini? Kwa sababu habari sahihi juu ya dini iliyoandikwa zamani zaidi ya zote, Biblia, hueleza jinsi mungu bandia, akitenda kazi kupitia nyoka, alivyoshawishi babu zetu wa kwanza waingie katika mwendo wa maafa. Tunapatwa na matokeo yenye kusononesha ya hila yake hadi leo. (Mwanzo 3:1-13, 16-19; Zaburi 51:5) Yesu “Mwana wa Mungu,” alisema juu ya mungu huyo mwasi akiwa “mkuu wa ulimwengu huu.” Mmoja wa mitume wa Yesu alimwita “mungu wa dunia hii.” (Yohana 1:34; 12:31; 16:11; 2 Wakorintho 4:4) Kwenye Ufunuo sura 12, mstari 9, anaelezwa kuwa “nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote.” Milki ya ulimwengu ya dini bandia imo chini ya udhibiti wa Shetani.

Shetani ni mdanganyi mkuu. (1 Timotheo 2:14) Yeye hutumia kwa hila tamaa ya kuabudu ambayo ainabinadamu imezaliwa nayo kwa kuendeleza aina nyingi za miungu—roho za mababu, sanamu, picha takatifu, Sanamu za Mariamu. Yeye hata hutegemeza ibada za miungu za kibinadamu, kama vile watawala wenye uwezo, majemadari washindi, na watu mashuhuri wa sinema au michezo. (Matendo 12:21-23) Twafanya vema kujilinda na hayo, kuazimia kumtafuta na kumwabudu Mungu wa kweli tu, ambaye kwa kweli “hawi mbali na kila mmoja wetu.”—Matendo 17:27.

Basi, ni nani huyo Mungu wa pekee ambaye twapaswa kumwabudu? Miaka 3,000 hivi iliyopita, mtunga zaburi wa Biblia alimweleza akiwa “Aliye juu . . . , Mwenyezi . . . , Mungu wangu nitakayemtumaini,” na akamwita kwa jina lake tukufu—“BWANA [Yehova, NW].” (Zaburi 91:1, 2) Mapema zaidi, Musa alikuwa amesema hivi juu yake: “BWANA [Yehova, NW], Mungu wetu, BWANA [Yehova, NW] ndiye mmoja.” (Kumbukumbu la Torati 6:4) Na nabii Isaya alimnukuu Mungu mwenyewe akisema: “Mimi ni BWANA [Yehova, NW]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.”—Isaya 42:8.

Yehova Mungu akusudia kuondolea jina lake suto lote ambalo mungu bandia Shetani ameliwekea. Alionyesha jinsi angefanya hivyo katika mwaka wa 1513 K.W.K., wakati alipomtumia nabii wake Musa kukomboa watu wa Israeli kutoka kwa uonevu wa Kimisri. Katika pindi hiyo, Mungu aliunganisha jina lake Yehova na maneno haya: “Nitathibitika kuwa kile ambacho nitathibitika kuwa.” (Kutoka 3:14, 15, NW) Yeye angejitetea mwenyewe dhidi ya Farao wa Misri, lakini kwanza alimwambia yule mtawala mwovu hivi: “Nilikusimamisha wewe kwa sababu ii hii, ili nikuonyeshe uweza wangu, tena kwamba jina langu litangazwe katika dunia yote.”—Kutoka 9:16.

Hali iko vivyo hivyo leo. Kama Farao wa zamani, mungu wa ulimwengu huu, Shetani, humpinga Yehova Mungu na kupiga vita ya kiroho kwa hila dhidi ya wale wanadamu wanaopenda uadilifu na kweli. (Waefeso 6:11, 12, 18) Mara nyingine tena, Mungu amekusudia kutukuza jina lake akikabili upinzani wa Shetani. Hata hivyo, kabla ya kuonyesha nguvu zake kwa kumharibu Shetani na kazi zake zote, Yehova atuma waabudu wake watangaze jina Lake katika dunia yote. Huko kutoa ushahidi kwa jina lake ni sehemu muhimu ya ibada ya kweli.

Kwa kufaa, Mungu mwenyewe amesema kwamba waabudu hao wangekuwa mashahidi wake, Mashahidi wa Yehova, “watu wale niliojiumbia nafsi yangu, ili wazitangaze sifa zangu.” (Isaya 43:10-12, 21) Wanatangazaje sifa za Yehova? Wanahubiri na kufundisha peupe na kutoka nyumba kwa nyumba, wakitangaza rasmi habari njema kwamba Ufalme wa Yehova, unaotawalwa na Mwana wake, Yesu Kristo, utaleta mibaraka ya milele kwa ainabinadamu tiifu kwenye dunia hii. Hivyo, wanamwabudu Mungu bila ‘kuacha,’ kama Wakristo wa kweli katika karne ya kwanza walivyofanya. (Matendo 5:42; 20:20, 21) Je! wameonea shangwe baraka ya kimungu katika kufanya hivyo? Kurasa zifuatazo zitajibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki