Je! Wewe Utakuwa Shahidi kwa Ajili ya Yule Mungu wa Kweli?
“‘Ninyi ni mashahidi wangu mimi,’ ndio usemi wa Yehova, ‘na mimi ni Mungu.’”—ISAYA 43:12. NW
1. Kwa sababu gani inatupasa sisi tuheshimu yule Mungu wa kweli?
MUDA mfupi kabla Yesu hajafa, yeye ‘aliinua macho yake kuyaelekeza mbinguni’ ili asali. Yeye alimwita yule Mmoja ambaye yeye alikuwa akisali kwake kuwa “yule Mungu wa kweli mmoja tu.” (Yohana 17:1, 3, NW) Kulingana na kufikiri kuzuri, kunaweza kuwa na Mungu mmoja tu anayeishi aliye wa kweli, yule Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima, yule Muumba. Kwa kuwa sisi ni wadeni kwa yule Mungu wa kweli kwa sababu ya kuwako kwetu, inatupasa sisi tumtolee yeye ile heshima ambayo yeye anastahili. Kama Ufunuo 4:11, NW unavyoeleza jambo hilo: “Wewe unastahili, Yehova, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na uwezo, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vikawako, na vikaumbwa.”
2. (a) Ni jambo gani lililo la kiakili kuitikadi juu ya yule Mungu wa kweli? (b) Ni jinsi gani yeye anavyowasiliana pamoja na wale ambao wanataka kuabudu yeye?
2 Lingekuwa jambo la kiakili kutazamia kwamba yule Mungu wa kweli hangeendelea kuachilia milele zile hali mbaya ambazo zimeharibu sura ya uumbaji wake wa kidunia. Na lingekuwa pia jambo la kiakili kuitikadi kwamba yeye angeendelea kuwapa habari waabudu wake juu ya mambo atakayofanya na mambo ambayo yeye anataka wao wafanye kabla yeye hajatekeleza hukumu zake. (Amosi 3:7) Ni jinsi gani yeye anavyowasiliana na watafutaji ukweli? Yeye anatumia wanadamu wenye nia wawe wanenaji wake. ‘“Ninyi ni mashahidi wangu,’ ndio usemi wa Yehova . . . ‘Kabla yangu mimi kulikuwa hakuna Mungu aliyeumbika, na baada yangu mimi hakuna aliyeendelea kuwako. Mimi—mimi ni Yehova, na kando yangu mimi hakuna mwokozi.’ “(Isaya 43:10, 11, NW) Lakini ni jinsi gani mtu anavyoweza kutambua wale ambao yule Mungu wa kweli anatumia kuwa mashahidi wake? Ni jinsi gani wao, na ujumbe wao, wanatofautiana na waabudu wa miungu mingine?
Mwito wa Ushindani kwa Miungu Mingine
3. Ni mwito wa ushindani gani ambao Yehova anatokeza kwa miungu mingine yote?
3 Yehova alivuvia Isaya pumzi ya kuandika katika kumbukumbu huu mwito wa ushindani kwa miungu mingine yote: “Ni nani aliye miongoni mwao [ile miungu ya mataifa na jamii za watu] ambaye anaweza kueleza jambo hilo [unabii sahihi]? Au je! wao wanaweza kusababisha sisi tusikie hata yale mambo ya kwanza [ambayo yatatukia katika wakati ujao]? Acheni wao [wakiwa miungu] watokeze mashahidi wao, kwamba wao [wakiwa miungu] wapate kutangazwa uadilifu, au acheni wao [zile jamii za watu wa mataifa] wasikie na kusema, ‘Huo ndio ule ukweli!’” (Isaya 43:9, NW) Hivyo Yehova anaitolea mwito wa ushindani miungu yote ambayo watu wanaabudu ithibitishe kwamba hiyo ni miungu. Mashahidi wayo wanapaswa kutokeza ushuhuda kwamba miungu yao inategemeka na inastahili kuabudiwa.
4. Ni jinsi gani sisi tunajua kwamba ile miungu ya mataifa ya kale ilikuwa isiyo na thamani?
4 Lakini ni nini ambacho miungu hiyo na waabudu wayo wametokeza? Je! wao wametuongoza sisi kwenye amani, ufanisi, afya, na maisha halisi? Historia inashuhudiza kwamba ile miungu mingi ya mataifa ya kale ilithibitika kuwa isiyo na thamani na hoi kwa kukosa nguvu. Hiyo hata haikuweza kubaki ikiwa vyombo vya ibada, kwa kuwa haipo leo. Ile miungu mingi ya Misri wa kale, Ashuru, Babuloni, Umedi-Uajemi, Ugiriki, Roma, na mataifa mengine ilithibitika kuwa ya bandia. Hiyo imo tu katika vitabu vya historia au katika majumba ya kuhifadhia vitu vya kihistoria ambamo sanamu zayo ni vyombo tu vya kutazamwa na watu wakiuliza hivyo ni vitu gani.
5. Ni jambo gani ambalo huenda sisi tukauliza juu ya ile miungu ya nyakati za ki-siku-hizi?
5 Hata hivyo, je! ile miungu ya ki-siku-hizi na waabudu wayo imezidi kwa njia yo yote ile miungu ya kale? Dini ya Kihindu peke yayo ina mamilioni ya miungu. Wabuddha, Wakatoliki, Wakonfyushiasi, Wayahudi, Waislamu, Waprotestanti, Washinto, Watao, na wengine wengi wana miungu yao wenyewe. Katika Afrika, Esia, na kwingineko, kani za maumbile, wanyama, na vyombo fulani-fulani vinaabudiwa kuwa miungu. Utukuzo wa taifa na ufuatiaji wa vitu vya kimwili, na hata uwenyewe wa mtu, yamekuwa miungu, katika maana ya kwamba hayo ndiyo mambo ambayo watu wengi wanajitolea kwa bidii iliyo nyingi zaidi. Ni njia ipi ya ibada ambayo kwa kweli inawakilisha yule mmoja ambaye anatangaza: “Mimi ni Yehova, na hakuna mmoja mwingine ye yote. Isipokuwa mimi hakuna Mungu”?—Isaya 45 5, NW.
“Mtawatambua kwa Matunda Yao”
6. Ni jinsi gani sisi tunavyoweza kupambanua kati y: ibada ya kweli na ibada-bandia?
6 Yesu aliweka kawaida inayotegemeka ya kutambulia ukweli au ubandia kwa mintarafu ya dini. Yeye alisema: “Mtawatambua kwa matunda yao. . . . Kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya . . . kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.” (Mathayo 7:16-19) Hivyo, ili kuamua yule Mungu wa kweli ni nani kutoka kati ya wale bandia, na waabudu wa kweli kutoka wale walio bandia, sisi tunahitaji kuchunguza mambo ambayo wao wanazaa. Je! matunda yao ni “mazuri,” au ni “mabaya”?
7. Historia ya karne hii inatuambia sisi nini juu ya dini za ulimwengu huu?
7 Mathalani, ni ipi kati ya dini za ulimwengu ambayo imesimamisha kwa imara amani halisi miongoni mwa washikani wayo duniani pote? Kwa uhakika, washiriki wa ile dini ya kweli, ndugu za kiroho, hawapaswi kuwa wakiuana mmoja na mwingine. Lakini watu milioni mia moja wameuawa katika vile vita vya karne hii ya 20, na vita vyote hivyo vimeungwa mkono na zile dini za ulimwengu huu. Kama tokeo, watu wa kidini wameua watu wengine wa kidini. Katika sehemu kubwa ya wakati huo, wao wameua watu wa dini yao wenyewe. Wakatoliki wameua Wakatoliki, Waprotestanti wameua Waprotestanti, Waislamu wameua Waislamu, na wale wa dini nyinginezo wamefuata mwendo uo huo.
8. Wenye kutazama wanaeleza jinsi gani juu ya kushindwa kwa kidini katika wakati wetu?
8 Katika makala moja ya mhariri yenye kichwa “Ile Jeuri Ambayo Imefanywa Katika Jina la Mungu,” Mike Royko alisema hivi juu ya dini hizi za ulimwengu, kana kwamba anaambia Mungu: “Wao wanaonyesha bidii yao ya kujitolea wewe kwa kuuana mmoja na mwingine kwa mamia. Mimi nadhani wao wanafikiri kwamba ikiwa upande mmoja unaweza kufutilia mbali ule upande mwingine, hiyo itathibitisha kwamba njia yao ya kukuabudu wewe ndiyo sahihi.” Yeye alisema kwamba ingawa yule papa anajionyesha mwenyewe kuwa mwanamume mwenye amani, “wafuasi wake wamejulikana kumwaga mamilioni kadha ya galani za damu wakati hasira zao zinapopanda juu.” Pia, wakati Carter aliyekuwa Rais wa United States alipoonelea kwamba “ulimwengu umepatwa na kichaa,” yeye alisema: “Usadikisho wa kidini wenye kina kirefu, ambao unapasa kufunganisha watu pamoja katika upendo, mara nyingi unaonekana kuwa sehemu ya kichaa hicho na uuaji huo.”
9. Kwa sababu gani haipasi sisi kufuata “miungu isiyo na thamani”?
9 Tunda hilo baya ndicho kinyume cha tunda ambalo lazima lizaliwe na wale ambao wanaabudu yule Mungu wa kweli. (Wagalatia 5:19-23) Kwa sababu hiyo, wale ambao wanaunga mkono dini na falsafa zenye kupigana vita ni sehemu ya ibada-bandia kwa uhakika ule ule walivyokuwa sehemu ya ibada-bandia Wamisri wa kale, Waashuru, Wababuloni, na wengine ambao walitegemea “miungu isiyo na thamani ambayo ni isiyosema.” (Habakuki 2:18, NW) Na sawa na vile neno la kiunabii la yule Mungu wa kweli lilivyotimizwa juu ya ibada-bandia ya kale, hivyo ndivyo itakavyokuwa katika wakati wetu: “Ile miungu yenyewe isiyo na thamani itapitilia mbali kabisa.” (Isaya 2:18, NW) Linastahili itibari onyo lake yeye: “Msijigeuze wenyewe kuelekea miungu isiyo na thamani.” —Walawi 19:4, NW.
Ni Nani Ambao Wanatoa Ushuhuda kwa Ajili ya Yehova?
10. Je! washikani wa dini za ulimwengu huu ni mashahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli?
10 Shahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli anapaswa kuwa mmoja ambaye anahimili ushuhuda juu ya Yeye. Je! wale washikani wa dini za ulimwengu huu wanahimili ushuhuda huo? Ni mara nyingi jinsi gani watu wa dini hizo wanasema na wewe juu ya ibada yao? Ni wakati gani wao wametembelea nyumbani kwako wewe kuhimili ushuhuda juu ya mungu wao? Ule mwito wa ushindani ambao yule Mungu wa kweli ametokeza kwa miungu bandia kwamba itokeze mashahidi unapita bila kusikizwa. Watu wa dini za ulimwengu huu hawahimili ushuhuda huo. Wao hawawezi kukuambia wewe yule Mungu wa kweli ni nani au makusudi yake ni nini. Viongozi wao wa kidini wameshindwa kuwafundisha ule ukweli. “Hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.”—Mathayo 15:14.
11. Ni nani peke yao ambao wanatoa ushuhuda kwa lile jina la yule Mungu wa kweli?
11 Ni akina nani walio na nia ya kudhabihu wakati, mali zao za kimwili, hata maisha zao, ili kutoa ushuhuda kwa ajili ya yule Mungu wa kweli? Ni akina nani ambao wanaambia watu kwamba yule Mungu wa kweli anatangaza: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu”? (Isaya 42:8, NW) Ni akina nani ambao wanafundisha kwamba “wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiwe yule Uliye Juu Zaidi juu ya dunia yote”? (Zaburi 83:18, NW) Katika wakati wake, Yesu angeweza kusema kwa yule Mungu wa kweli hivi: “Jina lako nimewadhihirishia.” (Yohana 17:6) Katika wakati wetu, ni Mashahidi wa Yehova peke yao ambao wanaweza kusema hivyo. Linafaa kama nini jina lao—Mashahidi wa Yehova!
Kutoa Ushuhuda Juu ya Ule Ufalme
12. Ni fundisho gani muhimu ambalo lazima mashahidi wa kweli wawe wakiambia wengine?
12 Zaidi ya kujulisha jina la yule Mungu wa kweli, ni nini, hasa, mashahidi wake wangekuwa wakisema juu ya makusudi yake? Yesu aliweka kielelezo kwa kufundisha wafuasi wake kusali kwa yule Mungu wa kweli hivi: “Ufalme wako uje.” (Mathayo 6:10, NW) Ufalme wa kimbingu wa Mungu ni ile serikali ambayo hatimaye itatawala dunia nzima. (Danieli 2:44) Hiyo ilikuwa ndicho kichwa cha fundisho la Yesu. (Mathayo 4:23) Kwa sababu ule Ufalme ndio utatuzi wa pekee kwa taabu za aina ya wanadamu, yeye alihimiza hivi: “Endeleeni, basi kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.”—Mathayo 6:33, NW.
13. (a) Mambo ya uhakika yanaonyesha nini juu ya kule kuhubiri kwa Mashahidi wa Yehova kuhusu Ufalme wa Mungu? (b) Ni jinsi gani kule kuhubiriwa kwa Ufalme ni ithibati ya kwamba Yehova ndiye yule Mungu wa peke yake wa unabii wa kweli?
13 Ni akina nani leo ambao wanahimili ushuhuda kwa ajili ya Ufalme wa Mungu? Profesa C. S. Braden, mwanafunzi mwenye kuchunguza sana dini za ulimwengu, alisema: “Mashahidi wa Yehova wameifunika kihalisi dunia kwa ushuhuda wao. . . . Inaweza kusemwa kikweli kwamba hakuna kikundi kimoja cha kidini katika ulimwengu ambacho kimeonyesha juhudi na udumifu mwingi zaidi katika jaribio la kueneza zile habari njema za ule Ufalme kuliko Mashahidi wa Yehova.” Lakini yeye aliandika hilo karibu miaka 40 iliyopita! Leo ushuhuda mkubwa zaidi wa Ufalme unatimizwa, kwa maana sasa kuna Mashahidi mara kumi zaidi ya waliokuwako wakati huo! Wapatao milioni tatu na nusu wa hao, katika makundi zaidi ya 54,900 duniani pote, wanatoa ushuhuda kwa ajili ya ule Ufalme, na hesabu zao zinakua kwa haraka sana. Tunda zuri hilo ni ithibati ya kwamba Yehova ndiye yule Mungu wa unabii wa kweli. Ndiye yeye ambaye alivuvia Mwana wake, Yesu, pumzi ya kutabiri kuhusu wakati wetu hivi: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.”—Mathayo 24:14; Yohana 8:28, NW.
Kuiga Upendo wa Mungu
14. Ni sifa gani ambayo lazima mashahidi wa Mungu wa kweli waige, na inamaanisha nini ikiwa wao hawaigi sifa hiyo?
14 Wale mashahidi wa kweli wa Mungu lazima waige sifa yake iliyo ya mbele zaidi ya zote —upendo. “Yeye ambaye hapendi hajaja kujua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8, NW) Kwa kweli, “watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni dhahiri kwa jambo hili: Kila mmoja ambaye haendelei na uadilifu hawi na asili pamoja na Mungu, wala yeye ambaye hapendi ndugu yake. . . . sisi tunapaswa kuwa na upendo kwa mmoja na mwingine; si kama Kaini, ambaye alikuwa na asili pamoja na yule mmoja mwovu na akachinja ndugu yake.”—1 Yohana 3:10-12, NW.
15. Kwa sababu gani sisi tunaweza kusema kwamba Mashahidi wa Yehova wanadhihirisha upendo halisi?
15 Mashahidi wa Yehova peke yao ndio walio na aina hiyo ya upendo. Wao hawajiweki chini ya mwongozo wa ile miungu ya vita, utukuzo wa taifa, na ukabila. Wao hawaungi mkono vita vyo vyote vya ulimwengu huu na kwa hiyo wao hawamo kamwe katika hali ambamo wangeunga mkono kule kuua ndugu zao za kiroho katika sehemu nyingine za ulimwengu. Wao, kama Yesu alivyosema, “si sehemu ya ulimwengu” na ‘wameweka chini ule upanga.’—Yohana 17:14; Mathayo 26:52, NW.
16. Ni jinsi gani wengine wanavyosaidia kutambulisha wale mashahidi wa kweli wa Mungu?
16 Uchunguzi mmoja wenye kichwa “Mengi Zaidi Juu ya Kutetea Haki ya Jeuri” ulisema: “Mashahidi wa Yehova wamedumisha bila ugeugeu msimamo wao wa ‘kutokuwamo kwa Kikristo’ kusiko na jeuri . . . Msimamo wao unaoendelea dhidi ya utumishi wa kitaifa wa namna yo yote, wa kivita au wa kiraia, na katao lao kuheshimu vitu vinavyofananisha utambulishi wa kitaifa limetokeza vipindi vya mnyanyaso, kufungwa gerezani, na kutendwa fujo na watu wenye ghasia katika nchi nyingi . . . Hata hivyo, Mashahidi hawajajibu kamwe kwa jeuri.” O Tempo, karatasi-habari ya Brazili, ilisema hivi juu yao: “Ingawa kuna dini nyingi zinazojisingizia-singizia kwa propaganda zao katika sehemu zote za dunia, hakuna hata moja juu ya uso wa dunia leo ambayo inaonyesha upendo uo huo.” Upendo huo halisi, Yesu alitangaza, unatambulisha wale mashahidi wa kweli wa Mungu. “Kwa hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa ninyi mnao upendo miongoni mwa ninyi wenyewe.”—Yohana 13:35, NW.
Mnyanyaso Waongeza Ushuhuda
17, 18. Ni kielelezo gani cha hivi majuzi kinachoonyesha jinsi mnyanyaso unavyoweza kuongezea ushuhuda wa Ufalme?
17 Mnyanyaso unaweza hata kutokeza ushuhuda mpana zaidi wa Ufalme. Mathalani, katika India kuna Mashahidi wa Yehova wapatao 8,000 tu. Hata hivyo, hivi majuzi jina na makusudi ya Yehova yalivumishwa kwa mweneo mkubwa katika nchi hiyo na jambo ambalo watoto Mashahidi 11 walifanya katika kuiga Wakristo wa karne ya kwanza ambao walisema hivi kwa mahakama moja: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29, NW) Watoto hao wa India walikuwa wameondoshwa shuleni kwa kutoimba ule wimbo wa kitaifa. Lakini Mahakama Kubwa Zaidi ya India ilikata maneno, kama ilivyoripotiwa katika Deccan Herald ya Bangalore, kwamba “hamna wajibu katika nchi hii wa kuimba ule Wimbo wa Kitaifa.” Mahakama hiyo iliona kwamba watoto hao “walikuwa wameonyesha staha inayofaa” na kwamba kutoimba kwao ‘hakukufikia kwa njia yo yote kuwa ukosefu wa kujitiisha chini ya wakubwa.’ Mahakama iliagiza kwamba watoto hao wakubaliwe tena shuleni.
18 Karatasi-habari iyo hiyo ilionelea pia: “Watoto hao walikataa kuimba ule Wimbo wa Kitaifa kwa sababu Mashahidi wa Yehova wanajifikiria wenyewe kuwa Wakristo na wenye bidii ya kujitolea kabisa kabisa ule Ufalme wa Mungu. . . . Wao basi hawashiriki katika utendaji wo wote wa kisiasa wa Serikali.” Pia, The Telegraph ya Kalikata iliripoti hivi: “Ile hatua ya watoto-shule imeingiza pia ndani ya nuru ya kuonekana na watu wote . . . Mashahidi wa Yehova, hao ambao sana sana walikuwa wamebaki wakiwa katika hali ya kufichika katika nchi yetu mpaka hivi majuzi.” Ndiyo, ‘habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa kwa ushuhuda kwa mataifa yote’ kabla ya ule mwisho kuja.—Mathayo 24:14, NW.
Kukusanywa Ndani kwa Mashahidi kwa Ajili ya Yule Mungu wa Kweli
19. Watu wenye mioyo minyofu wanahitaji kufanya nini ikiwa wao wanataka kuabudu yule Mungu wa kweli?
19 Leo, yule Mungu wa kweli, Yehova, anafanya watu wake wahimili ushuhuda kwa enzi kuu na makusudi yake. Wakati wao wanapotangaza ujumbe wake kwa kani iliyo kubwa hata zaidi, yeye anakusanya hesabu zinazoongezeka za watu wenye mioyo minyofu kutoka mataifa yote waingie katika ushirika pamoja na waabudu wake. (Isaya 2:2-4) Wao wanaachilia mbali miungu-bandia yao na kugeukia ile ibada ya yule Mungu wa kweli, sawa na vile wale ambao walitaka kuabudu Yehova walivyofunguliwa kutoka utekwa kwa Babuloni wa kale, ambako ile ibada ya miungu-bandia ilitapakaa. —Isaya 43:14.
20, 21. Kwa sababu gani ni jambo la haraka kuachilia mbali miungu-bandia sasa na kutokuwa wafuasi-wasimama-kando tu?
20 Je! wewe utakuwa shahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli? Je! wewe utachukua msimamo wako kwa ajili ya ibada ya kweli na kuepuka kushiriki ile hatia ya damu na ulaumifu wa ulimwengu huu na miungu-bandia yao? Neno la Mungu linahimiza hivi: “Endeni nje kutoka kwa mwanamke huyo [ibada-bandia ya Kibabuloni], watu wangu, ikiwa ninyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika dhambi zake yeye, na ikiwa ninyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake yeye.” (Ufunuo 18:4, NW) Ndiyo, ‘enda nje,’ chukua hatua kabla haijawa kuchelewa mno! Usiwe kama yule mwanamume ambaye, wakati alipoulizwa na gazeti moja la Kikatoliki juu ya dini anayopendelea zaidi, alisema: “Mimi nadhani mimi ni Mfuasi Msimama-Kando wa Yehova. Mimi ninaitikadi mambo mengi sana ambayo Mashahidi wa Yehova wanaitikadi—lakini mimi sitaki kuhusika ndani.”
21 Hata hivyo, karibuni kila mtu aliye duniani atahusika ndani wakati Yehova atakapofisha ile miungu-bandia ya ulimwengu huu na waabudu wayo: “Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu.” (Yeremia 10:11) Wakati huo hakutakuwa na wafuasi-wasimama-kando. Kutakuwa tu na wale walio na wale wasio mashahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli. (Mathayo 24:37-39; 2 Petro 2:5; Ufunuo 7:9-15) Je! wewe utakuwa shahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli? Inakupasa wewe uwe, kwa maana “yule Mungu wa kweli ni Mungu wa vitendo vya kuokoa kwa ajili yetu; na ni za Yehova yule Bwana mwenye Enzi Kuu zile njia za kutoka kwenye kifo.”—Zaburi 68:20, NW.
Maswali ya Kupitia
◻ Ni mwito wa ushindani gani ambao yule Mungu wa kweli anatokeza kwa miungu-bandia?
◻ Ni kwa kawaida gani yenye kutegemeka sisi tunaweza kupambanua kati ya ibada ya kweli na ibada-bandia?
◻ Ni tunda gani ambalo linaonyesha ile miungu ya ulimwengu huu kuwa isiyo na thamani kama ilivyokuwa ile ya kale?
◻ Ni tunda gani nzuri ambalo lazima mashahidi kwa ajili ya yule Mungu wa kweli wawe wanazaa, na ni nani ambaye anadhihirisha tunda hilo?
◻ Kwa sababu gani ni jambo la haraka kuchukua hatua sasa ya kuachilia mbali ibada-bandia?
[Picha katika ukurasa wa 16]
Ile miungu isiyo na thamani ya mataifa ya kale imekoma kuwako isiwe vyombo vya kuabudiwa
[Picha katika ukurasa wa 17]
Katika karne yetu watu wapatao milioni mia moja wameuawa katika vita vyenye kuungwa mkono na dini za ulimwengu huu
[Credit Line]
U.S. Army photo
[Picha katika ukurasa wa 18]
Yesu alisema kwamba mashahidi wa kweli wangejulikana kwa upendo ambao wao wanao miongoni mwao wenyewe