Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 3/15 kur. 3-4
  • Kile Ufalme wa Mungu Unachomaanisha kwa Wengi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kile Ufalme wa Mungu Unachomaanisha kwa Wengi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Ambayo Ufalme Umeonwa
  • Ufalme wa Mungu—Tumaini Peke Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kwa Nini Upendezwe na Ufalme wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Manabii Wawongo Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Ufalme Wa Mungu
    Amkeni!—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 3/15 kur. 3-4

Kile Ufalme wa Mungu Unachomaanisha kwa Wengi

YESU KRISTO mara nyingi alisema juu ya Ufalme wa Mungu. Kwa habari hiyo mwanahistoria H. G. Wells aliandika hivi: “Wenye kutokeza ni ule umashuhuri mwingi uliotolewa na Yesu kwa lile fundisho aliloita Ufalme wa Mbinguni, na jinsi kwa ulinganifu linavyokosa maana katika taratibu na mafundisho ya yaliyo mengi ya makanisa ya Kikristo. Fundisho la Ufalme wa Mbinguni, lililokuwa fundisho kuu la Yesu, na lenye kuwa na sehemu ndogo sana katika imani za Kikristo, kwa hakika ni mojawapo mafundisho yenye kuleta mabadiliko makubwa sana lililopata kuchochea na kubadili mawazo ya kibinadamu kwa wakati wowote.”

Ni kwa nini makanisa hayana mengi ya kusema juu ya Ufalme wa Mungu? Sababu moja yaweza kuwa kwamba hakuna uhakika juu ya Ufalme. Ni maoni gani ambayo yameshikiliwa kuhusu huo ufalme?

Jinsi Ambayo Ufalme Umeonwa

Wengine wameutambulisha Ufalme wa Mungu na Kanisa Katoliki. Baada ya maaskofu kumkubali Maliki Konstantino kuwa kiongozi wao kwenye lile Baraza la Nisea katika mwaka wa 325 W.K., kanisa lilijiingiza katika siasa, na watu waliambiwa kwamba Ufalme ulikuwa umekuja tayari. Encyclopædia Britannica hueleza kwamba kulingana na theolojia ya Augustino (354-430 W.K.), “Ufalme wa Mungu tayari umeanza katika ulimwengu huu kwa kuanzisha kwa kanisa” na “upo tayari katika sakramenti za kanisa.”

Wengine huona Ufalme wa Mungu kuwa mafanikio ya kibinadamu. Ensaiklopedia hiyo hiyo husema hivi: “Makanisa ya Mapinduzi Makubwa ya Kidini . . . punde baadaye yakawa makanisa ya kishirika ya eneo, ambayo nayo yalikomesha matazamio ya wakati wa mwisho” kuhusiana na kuja kwa Ufalme wa Mungu. H. G. Wells aliandika hivi: “Wanadamu waligeuza uhusisho wa maisha yao kutoka ufalme wa Mungu na udugu wa ainabinadamu wakauelekeza kwenye mambo yaliyoonekana kuwa ya kihalisi zaidi, Ufaransa na Uingereza, Urusi Mtakatifu, Hispania, Prushia . . . Hayo yalikuwa miungu ya Ulaya halisi na yenye uhai.”

Katika nyakati za ki-siku-hizi pia, Ufalme umefanywa kuwa wa kilimwengu. Encyclopædia Britannica hueleza hivi: “Iliyo tabia ni mtazamo wa msingi wa kwamba mwanadamu mwenyewe ndiye apaswa kutayarisha jamii kamilifu ya wakati ujao katika njia ya kufanyiza na ya kufanya tengenezo na kwamba uanzishaji wa kibinadamu unachukua mahali pa ‘kutumaini’ na ‘kungojea.’” Kwa habari ya “gospeli ya kijamii,” kitabu hicho hicho chaendelea hivi: “Harakati hiyo iliona ujumbe wa Kikristo kuhusu Ufalme wa Mungu kuwa hasa msukumo ili kutengeneza upya hali za kilimwengu za jamii katika maana ya maadili ya Ufalme wa Mungu.”

Wayahudi wengi pia wameona Ufalme kuwa mafanikio ya kibinadamu. Katika 1937 mkutano wa warabi wa Reform katika Columbus, Ohio, U.S.A., ulisema hivi: “Tunakuona kuwa kazi yetu ya kihistoria kushirikiana na wanadamu wote katika kusimamishwa kwa ufalme wa Mungu, wenye udugu wa ulimwengu wote mzima, haki, kweli na amani duniani. Huo ndio mradi wetu wa kimesiya.”

Maoni mengine yenye kushikiliwa na wengi ni kwamba Ufalme wa Mungu ni hali ya moyo wa mtu. Kwa mfano, katika United States, Mkusanyiko wa Baptisti ya Kusini wa 1925 ulitangaza rasmi hivi: “Ufalme wa Mungu ni utawala wa Mungu katika moyo na maisha ya mtu mmoja mmoja katika kila uhusiano wa kibinadamu, na katika kila namna na shirika la jamii lililopangwa kitengenezo. . . . Ufalme wa Mungu utakamilika wakati kila wazo na nia ya mwanadamu itakapoletwa ndani ya utumwa wa mapenzi ya Kristo.”

Kwa hiyo basi, je, kanisa ndilo Ufalme wa Mungu? Je, Ufalme huo utaletwa kupitia njia za kilimwengu? Huo ni hali ya moyo? Na Ufalme wa Mungu waweza kuwa na maana gani kwako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki