Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 4/1 kur. 6-8
  • Je! “Utaratibu wa Ulimwengu Mpya” wa Mwanadamu U Karibu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! “Utaratibu wa Ulimwengu Mpya” wa Mwanadamu U Karibu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utumwa kwa dhambi na Kifo
  • Matumizi Mabaya ya Hiari
  • ‘Mwanadamu Hawezi Kuelekeza Hatua Zake’
  • Nani Ajuaye Vizuri Zaidi?
  • Watu Huru Lakini Wanaotakwa Watoe Hesabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Usikose Kusudi la Uhuru wa Kupewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Jinsi ya Kupata Uhuru wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Uhuru Unaofurahiwa na Waabudu wa Yehova
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 4/1 kur. 6-8

Je! “Utaratibu wa Ulimwengu Mpya” wa Mwanadamu U Karibu?

1. Tamaa ya uhuru zaidi wa kisiasa imeonyeshwaje katika miaka ya karibuni?

LEO, mamilioni ya watu wamo utumwani mwa dini bandia, na huchagua kuendelea kukaa hivyo. Wakati ule ule watu zaidi na zaidi wanadai uhuru wa kisiasa. Matukio yasiyo ya kawaida ya miaka michache iliyopita katika Ulaya ya Mashariki na kwingineko huonyesha kwamba watu wanataka namna za serikali zilizo huru zaidi. Kama tokeo, wengi wanasema kwamba enzi mpya ya uhuru imekaribia. Rais wa United States aliiita “utaratibu wa ulimwengu mpya.” Kweli kweli, viongozi wa ulimwengu kila mahali walikuwa wakisema kwamba Vita Baridi na shindano la silaha vilikuwa vimekwisha na kwamba enzi mpya ya amani ilikuwa imepambazuka kwa ajili ya wanadamu.—Linganisha 1 Wathesalonike 5:3.

2, 3. Ni hali gani huzuia uhuru wa kweli?

2 Lakini, hata kama jitihada za kibinadamu zingetokeza silaha chache zaidi na namna za utawala zenye uhuru zaidi, je! kweli kungekuwako uhuru wa kweli? Sivyo, kwa sababu ya matatizo yenye kushtua yaliyo katika mataifa yote, kutia na yale ya kidemokrasia, ambako hesabu ya maskini huongezeka na mamilioni hung’ang’ana ili wastahimili kiuchumi. Ripoti ya Umoja wa Mataifa hutaarifu kwamba ijapokuwa maendeleo katika sayansi na tiba, kila siku ulimwenguni pote wastani wa watoto 40,000 hufa kutokana na ugonjwa unaoletwa na ukosefu wa chakula chenye kulisha mwili au maradhi yanayoweza kuzuiliwa. Stadi katika uwanja huu alisema hivi: “Umaskini unapata tabia ambazo zinatisha kweli kweli wakati ujao wa binadamu.”

3 Kwa kuongezea, watu wengi zaidi kuliko walivyopata kuwako wanataabishwa na uhalifu ambao unakuwa wenye ukatili zaidi. Chuki za kisiasa, kijamii, na kidini zinagawanya nchi mbalimbali. Katika mahali pengine pengine hali haitofautiani sana na ile iliyotabiriwa kwenye Zekaria 14:13, isemapo kwamba watu ‘wangekuwa wenye kuvurugika na kuogopa sana hivi kwamba kila mtu atakamata mtu aliye karibu naye na kumshambulia.’ (Today’s English Version) Matumizi mabaya ya dawa za kulevya na magonjwa yenye kuambukia kingono yanaenea duniani pote. Mamilioni ya watu wameambukiwa na UKIMWI; katika United States pekee, watu zaidi ya 120,000 tayari wameuawa nao.

Utumwa kwa dhambi na Kifo

4, 5. Bila kujali uhuru mbalimbali ulioko leo, ni utumwa wa namna gani unaonasa kila mtu?

4 Hata hivyo, hata kama hakukuwa na yoyote ya hali hizo mbaya, bado watu hawangekuwa na uhuru wa kweli. Bado wote wangekuwa katika utumwa. Kwa nini iko hivyo? Tutoe mfano: Vipi kama mtawala fulani mwenye kutumia nguvu mwenye mamlaka peke yake angemfanya kila mtu duniani kuwa mtumwa na kuwaua wote? Kwa kweli, hilo ndilo ambalo limepata jamii nzima ya kibinadamu tangu wazazi wetu wa kwanza walipomwasi Mungu wakawa watumwa wa utawala wenye uonevu wa Ibilisi.—2 Wakoritho 4:4.

5 Mungu alipoumba wanadamu, yeye alikusudia waishi duniani milele katika ukamilifu, katika paradiso, kama vile Mwanzo sura ya 1 na ya 2 huonyesha. Lakini kwa sababu ya uasi wa babu wetu wa kale Adamu dhidi ya Mungu, sisi sote tuko chini ya hukumu ya kifo tangu wakati tunapochukuliwa mimba: “Kama kwa mtu mmoja [Adamu, kichwa cha familia ya wanadamu] dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” Kama isemavyo Biblia, ‘mauti ikatawala ikiwa mfalme.’ (Warumi 5:12, 14) Hivyo, bila kujali ni uhuru mwingi kadiri gani huenda sisi binafsi tukawa nao, sisi sote tumo utumwani mwa dhambi na kifo.

6. Kwa nini kumekuwa maendeleo kidogo tu katika muda wa kuishi tangu Zaburi 90:10 iandikwe?

6 Na zaidi, maisha tuliyo nayo sasa ni mafupi sana. Hata kwa wale waliojaliwa, ni makumi machache tu; kwa wale wasiojaliwa sana, miaka michache tu au punde kuliko hiyo. Na uchunguzi mpya wasema hivi: “Sayansi na tiba vimesukuma muda wa kuishi wa wanadamu kufikia kikomo chao cha kiasili.” Hiyo ni kwa sababu kutokamilika na kifo vimekazwa ndani ya mfumo wetu kwa kurithi likiwa tokeo la dhambi ya Adamu. Ni huzuni kama nini kwamba tukiishi kufikia miaka 70 au 80, wakati twapaswa kuwa tukiwa wenye hekima zaidi na kuweza kufurahia maisha zaidi, miili yetu huharibika nao mwisho wetu wawa mavumbi!—Zaburi 90:10.

7. Kwa nini wanadamu hawawezi kuwa chanzo cha uhuru mbalimbali wa kweli tunaotaka na kuhitaji?

7 Ni utawala wa kibinadamu wa aina ipi unaoweza kuzuia utumwa huo kwa dhambi na kifo? Hakuna hata mmoja! Hakuna wakuu wa serikali, wanasayansi, au madaktari kokote wanaoweza kutuweka huru na laana za magonjwa, uzee, na kifo, wala hakuna wowote wawezao kumaliza ukosefu wa usalama, ukosefu wa haki, uhalifu, njaa, na umaskini. (Zaburi 89:48) Hata wanadamu wawe wenye nia njema kadiri gani, haiwezekani wao kuwa chanzo cha uhuru mbalimbali wa kweli tunaotaka na kuhitaji.—Zaburi 146:3.

Matumizi Mabaya ya Hiari

8, 9. Ni nini kilicholeta aina ya kibinadamu katika hali yayo iliyopo yenye kuhuzunisha?

8 Familia ya kibinadamu imo katika hali hii yenye kuhuzunisha kwa sababu Adamu na Hawa walitumia vibaya hiari yao. Petro wa Kwanza 2:16 husema, kulingana na tafsiri ya The Jerusalem Bible: “Jiendesheni kama watu huru, na msitumie kamwe uhuru wenu kama udhuru wa uovu.” Hilo huonyesha wazi kwamba Mungu hakukusudia uhuru wa mwanadamu usiwe na mipaka. Ulipaswa kutumiwa ndani ya mipaka ya sheria za Mungu, ambazo zilikuwa adilifu na zingenufaisha kila mtu. Na mipaka hiyo ilikuwa mipana vya kutosha kuruhusu uhuru mwingi wa uchaguzi wa kibinafsi, hivi kwamba utawala wa Mungu haungepata kamwe kuwa wenye uonevu.—Kumbukumbu la Torati 32:4.

9 Hata hivyo, wazazi wetu wa kwanza walichagua kujiamulia wenyewe yaliyofaa na yasiyofaa. Kwa kuwa waliondoka kimakusudi ndani ya utawala wa Mungu, yeye aliwaondolea utegemezo wake. (Mwanzo 3:17-19) Hivyo wakawa wasiokamilika, tokeo likiwa magonjwa na kifo. Badala ya uhuru, wanadamu wakaingia katika utumwa wa dhambi na kifo. Pia walipata kuwa chini ya tamaa zenye ubinafsi za watawala wa kibinadamu wasiokamilika na, mara nyingi, walio wakatili.—Kumbukumbu la Torati 32:5.

10. Yehova ameshughulikiaje mambo kwa upendo?

10 Mungu ameruhusu wanadamu wafanye jaribio hili la ule unaodhaniwa kuwa uhuru kamili kwa kipindi tu cha wakati chenye mpaka. Yeye alijua kwamba matokeo yangeonyesha pasipo shaka yoyote kwamba utawala wa kibinadamu bila kumtegemea Mungu haungeweza kufanikiwa. Kwa kuwa hiari, ikitumiwa ifaavyo, ni hazina kubwa sana, Mungu katika upendo wake aliruhusu kwa muda mfupi yale ambayo yametukia badala ya kuondoa zawadi ya hiari.

‘Mwanadamu Hawezi Kuelekeza Hatua Zake’

11. Historia imeungaje mkono usahihi wa Biblia?

11 Matukio ya historia yameonyesha usahihi wa Yeremia sura ya 10, mstari wa 23 na wa 24, isemayo: “Kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. Ee BWANA [Yehova, NW], unirudi.” Historia imeonyesha pia usahihi wa Mhubiri 8:9, ambao hujulisha wazi hivi: ‘Mtu ana mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasara yake.’ Ni kweli kama nini! Familia ya kibinadamu imepatwa na msiba mmoja baada ya mwingine, na mwisho wao wote ukiwa kaburi. Mtume Paulo alieleza hali hiyo barabara aliposema, kama ilivyoonyeshwa kwenye Warumi 8:22: “Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” Naam, uhuru wa kujitegemea bila sheria za Mungu umemaanisha msiba.

12. Vyanzo vya ulimwengu vyasema nini juu ya uhuru kamili?

12 Kitabu Inqusition and Liberty kilieleza uhuru kwa njia hii: “Uhuru wa kujitegemea, wenyewe, si sifa ya wema: Si jambo la kujivunia bila kuelezwa zaidi. Kwa kweli, huenda ukawa tu mojayapo zile namna potovu zaidi za ubinafsi . . . Mwanadamu si kiumbe mwenye hali ya kujitegemea kabisa, na hawezi hata kujitahidi kuwa hivyo bila kufanya upumbavu.” Na Prince Philip wa Uingereza alisema wakati mmoja hivi: “Uhuru wa kujitosheleza kila tamaa na silika ya ubinafsi huenda ukavutia, lakini maono hufundisha mara nyingi sana kwamba, uhuru bila kujizuia . . . na mwenendo bila kufikiria wengine ndiyo njia hakika zaidi ya kuharibu ubora wa maisha ya jamii yoyote ile, hata utajiri wayo uweje.”

Nani Ajuaye Vizuri Zaidi?

13, 14. Ni nani pekee awezaye kuandaa uhuru wa kweli kwa familia ya kibinadamu?

13 Ni nani ajuaye vizuri zaidi jinsi makao yapasavyo kupangwa—ni wazazi wenye upendo, wenye uwezo, na wenye ujuzi au ni watoto wachanga? Jibu ni wazi. Hali kadhalika, Muumba wa wanadamu, Baba yetu wa kimbingu ajua kilicho bora kwetu. Yeye ajua jinsi jamii ya kibinadamu yapaswa kupangwa vizuri na kutawalwa. Ajua jinsi hiari yapasa kuongozwa ili kuleta manufaa za uhuru wa kweli kwa kila mtu. Ni Mungu mwenye uweza wote pekee, Yehova, ajuaye jinsi ya kuondoa familia ya kibinadamu katika utumwa wayo na kuandaa uhuru wa kweli kwa wote.—Isaya 48:17-19.

14 Katika Neno lake, kwenye Warumi 8:21, Yehova atoa ahadi hii yenye kutumainisha: “Kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.” Naam, Mungu aahidi kuikomboa kabisa familia ya kibinadamu katika hali yayo ya sasa yenye huzuni. Makala ifuatayo itazungumzia jinsi hilo litakavyotukia.

Wewe Ungejibuje?

(Kupitia kurasa 3 hadi 8)

◻ Kwa nini wanadamu huthamini sana uhuru?

◻ Wanadamu wametiwa utumwani katika njia zipi muda wote wa historia?

◻ Ni kwa nini Yehova ameruhusu utumizi mbaya wa hiari kwa muda mrefu kadiri hiyo?

◻ Ni nani pekee awezaye kuleta uhuru wa kweli kwa wanadamu wote, na kwa nini?

[Picha katika ukurasa wa 7]

Muda wa kuishi wa wanadamu uko kama vile ilivyotaarifiwa miaka 3,500 iliyopita katika Zaburi 90:10

[Hisani]

Kwa Hisani ya The British Museum

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki