Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 11/15 uku. 7
  • Msalaba —Kifananisho cha Ukristo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msalaba —Kifananisho cha Ukristo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Kweli Yesu Alikufa Juu ya Msalaba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Msalaba Katika Ibada?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii Msalaba Katika Ibada?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Maana ya Kumpenda Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 11/15 uku. 7

Msalaba —Kifananisho cha Ukristo?

KWA karne nyingi watu wengi sana wamekubali msalaba kuwa kifananisho cha Ukristo. Lakini ni hivyo kweli? Wengi ambao wameamini hivyo kwa moyo mweupe hushangaa sana kujifunza kwamba msalaba si jambo lililomo katika Jumuiya ya Wakristo peke yake. Kinyume cha hilo, umetumiwa sana katika dini zisizo za Kikristo kotekote ulimwenguni.

Kwa mfano, katika miaka ya mapema ya 1500, Hernán Cortés na jeshi lake la “Kikristo” walipojitayarisha kushambulia Milki ya Azteki, walibeba mabango yaliyopiga mbiu, “Acheni tufuate ishara ya Msalaba Mtakatifu katika imani ya kweli, kwani chini ya ishara hiyo tutashinda.” Ni lazima walishangaa kupata kwamba adui zao wapagani waliheshimu msalaba uliofanana na wao wenyewe. Kitabu Great Religions of the World husema: “Cortés na wafuasi wake waligutushwa sana na dhabihu za kibinadamu za Waazteki na ile iliyoonekana kama miigo ya Ukristo ya kishetani: . . . kuheshimu vifananisho vilivyo kama msalaba vya vijimungu vya upepo na mvua.”

Katika makala ya mhariri katika gazeti la habari La Nación, mwandikaji José Alberto Furke aonyesha kwamba katika nusu ya pili ya karne ya 18, “ubishi mkali na wenye kusisimua [ulianza] miongoni mwa waanthropolojia [wenye kuchunguza sayansi ya wanadamu] na waakiolojia juu ya vyanzo na maana ya ishara zenye umbo la msalaba” ambazo walikuwa wakipata katika sehemu kubwa ya Amerika ya Kati na Kusini. Yaonekana wengine walitaka sana kulinda cheo cha msalaba kikiwa kifananisho cha “Kikristo” peke yake hivi kwamba walitokeza nadharia kwamba nchi hizo za Amerika zilikuwa zimeenezewa evanjeli kwa njia fulani kabla ya safari mashuhuri ya Kolumbus! Wazo hilo lisilo halisi lilihitaji kukataliwa mbali kuwa bila msingi wowote.

Baadaye, uvumbuzi mwingi zaidi kuhusu habari hiyo ulikomesha ubishi huo. Furke asema hivi: “Katika kitabu kilichotangazwa kwa chapa katika 1893 na Taasisi ya Smithsonia, ilithibitishwa kwamba msalaba ulikuwa tayari ukiheshimiwa . . . muda mrefu kabla ya kuwasili kwa Wazungu wa kwanza katika Amerika Kaskazini, jambo linalothibitisha nadharia . . . ya kwamba kifananisho hicho kilitokea katika jumuiya zote kikiwa sehemu ya ibada ya kidhehebu ya kani zinazotokeza uhai.”

Biblia huonyesha kwamba Yesu hakuuawa juu ya msalaba wa kimapokeo hata kidogo, bali, juu ya mti sahili, au stau·rosʹ. Neno hilo la Kigiriki, linalotokea kwenye Mathayo 27:40, humaanisha boriti au nguzo iliyonyooka, kama zile zilizotumiwa katika kujenga misingi. Kwa hiyo, msalaba haukuwakilisha kamwe Ukristo wa kweli. Yesu Kristo alitambulisha kifananisho au “alama,” ya Ukristo wa kweli alipowaambia wafuasi wake hivi: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.”—Yohana 13:35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki