Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 12/1 kur. 5-6
  • Ni Nani Aliye na Upendeleo wa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Aliye na Upendeleo wa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Viwango vya Mungu vya Juu Zaidi
  • Twaweza Kupata Upendeleo wa Mungu
  • Wewe Hupendelea Watu wa Aina Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Je, Mungu Hupendelea Mataifa Fulani?
    Amkeni!—2005
  • Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Tumaini Lako—Je, Ni Mungu au Mali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 12/1 kur. 5-6

Ni Nani Aliye na Upendeleo wa Mungu?

Sisi sote twataka kupendwa na wenzetu. Tamaa yenye nguvu zaidi ya Mkristo ni kupata upendeleo wa Mungu. Inataarifiwa hivi juu ya Yehova Mungu kwenye Zaburi 84:11, New World Translation: “Upendeleo na utukufu ndivyo yeye hutoa. Yehova mwenyewe hatazuia chochote chema kutoka kwa wale wanaotembea katika hali isiyo na hitilafu.” Wakati wa kuzaliwa kwa Yesu, kilio chenye shangwe cha malaika wa kimbingu kiliahidi “amani duniani kwa wanaume ambao yeye hupendelea!”—Luka 2:14, Moffatt.

Lakini Mungu hupendelea nani? Je! viwango vya Mungu ni sawa na vile vya mwanadamu? Kwa kueleweka, haviko sawa, kama vile ilivyoonyeshwa na yale yaliyozungumziwa katika makala inayotangulia. Kwa kweli, kwa kuwa Wakristo wanaonywa kwa upole ‘wawe wenye kumwiga Mungu,’ kila mmoja wetu aweza kwa kufaa kuuliza, Je! mimi huonyesha upendeleo kwa wale ambao Mungu huonyesha upendeleo, au ninaelekea kufuata viwango vya kilimwengu katika kukadiria kwangu watu? (Waefeso 5:1) Ili kupata upendeleo na kibali cha Yehova, ni lazima tuwe waangalifu kuona mambo jinsi anavyoyaona.

Viwango vya Mungu vya Juu Zaidi

“Mungu hapendelei upande mmoja,” akasema mtume Petro, “bali katika kila taifa mtu ambaye huhofu yeye na kufanya uadilifu anakubalika kwake.” Zaidi ya hayo, mtume Paulo alishuhudia kwamba Mungu “alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika [mtu] mmoja.” (Matendo 10:34, 35, NW; 17:26) Kwa hiyo, ni jambo lifaalo tu kukata maneno kwamba sifa zao za kimwili ziwe ni nini, wanadamu wote wako sawa machoni pa Mungu. Hali ikiwa hivyo, lisingekuwa jambo lifaalo kwa Mkristo kupendelea mtu fulani mno kwa sababu tu mtu huyo atoka mkoa fulani au ni mwenye ngozi ya rangi fulani au ni wa taifa jingine. Bali, angefanya vema kufuata Kielelezo chake, Yesu Kristo, ambaye kuhusu yeye hata maadui walikiri kwamba hakuonyesha kupendelea upande mmoja.—Mathayo 22:16.

Usemi wa Kiingereza “skin-deep” (kina cha ngozi) hutumiwa nyakati nyingine kueleza kitu chenye kina kidogo au kisicho na maana. Rangi ya ngozi ni hivyo tu; kina kidogo tu. Rangi ya ngozi ya mtu haionyeshi kwa njia yoyote utu au sifa za kindani. Kwa habari ya kuchagua ni watu gani tutashiriki nao, kula nao, au kusalimiana nao kwa mkono, kwa hakika hatupaswi kutazama hasa rangi ya ngozi. Kumbuka, yule mwanamwali aliyetunga baadhi ya mashairi mazuri na ya kimahaba zaidi yaliyopata kuandikwa wakati wowote alisema hivi juu yake mwenyewe: “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, . . . ni mweusi-mweusi, kwa sababu jua limeniunguza.” (Wimbo Ulio Bora 1:5, 6) Wala taifa wala rangi haifanyizi msingi ufaao wa kuonyesha upendeleo. La maana zaidi ni kama mtu anamhofu Mungu na kufanya uadilifu.

Mungu huhisije juu ya kuwa na utajiri wa kimwili? Kati ya watu wote ambao Mungu hupenda na kupendelea, Mwana wake, Yesu Kristo, ndiye wa kwanza. Hata hivyo, alipokuwa duniani, Yesu hakuwa na “pa kulaza kichwa chake.” (Mathayo 8:20) Hakuwa na mali yenye shamba, nyumba, migunda, miti ya matunda, au wanyama. Hata hivyo, Yehova alimheshimu na kumkweza kwenye cheo kilicho juu ya kila mtu mwingineye yote katika ulimwengu wote mzima ila Mungu mwenyewe.—Wafilipi 2:9.

Yesu Kristo alipata upendeleo wa Mungu kwa sababu alikuwa tajiri si wa mali za kimwili bali wa matendo mema. (Linganisha 1 Timotheo 6:17, 18.) Aliwaonya wafuasi wake kwa upole: “Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi.” (Mathayo 6:19, 20) Hivyo, badala ya kuonyesha upendeleo kwa wale walio matajiri wa mali za kilimwengu tu, Wakristo hawataonyesha ubaguzi wowote kwa msingi wa mali za kimwili. Watawatafuta wale walio matajiri kuelekea Mungu haidhuru kama wao ni matajiri au maskini katika njia ya kimwili. Usisahau kamwe kwamba ‘Mungu aliwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme.’ (Yakobo 2:5) Ukidumisha maoni ya Mungu, hutanaswa kamwe na lile zoea la kawaida la kupendelea au kujaribu kupata upendeleo wa wale walio matajiri kimwili.

Kwa habari ya elimu, Biblia huonyesha wazi kwamba Mungu hutuhimiza tutafute maarifa na hekima na kwamba Yesu Kristo alikuwa ndiye mwalimu mkuu zaidi aliyepata kuitembea dunia. (Mithali 4:7; Mathayo 7:29; Yohana 7:46) Lakini si hekima au elimu ya kilimwengu inayopata upendeleo wa Mungu. Kinyume cha hiyo, Paulo atuambia kwamba “si wengi wenye hekima ya mwilini, . . . walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima.”—1 Wakorintho 1:26, 27.

Mungu hupendelea wale wenye kuelimishwa vema, si katika masomo ya kilimwengu yanayofundishwa katika taasisi za masomo ya juu zaidi, bali katika ile “lugha iliyo safi” ya kweli kama ipatikanavyo katika Neno lake, Biblia. (Sefania 3:9) Kwa kweli, Yehova mwenyewe anawafundisha watu wake leo kupitia programu ya kielimu inayoenea hadi kona za mbali za dunia. Kama vile ilivyotabiriwa na nabii Isaya, watu wa mataifa yote wanaitikia kwa kusema: “Njoni, twende juu mlimani kwa BWANA [Yehova, NW], nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake.” Kwa hiyo, badala ya kutukuza elimu ya kilimwengu, Wakristo watawatafuta wale wanaothibitisha kwa maneno na matendo yao kwamba kwa kweli wao ni ‘watu waliofundishwa na Yehova.’ Kwa kufanya hivyo, watafurahia ‘wingi wa amani’ ambao Mungu hutoa.—Isaya 2:3; 54:13.

Twaweza Kupata Upendeleo wa Mungu

Naam, viwango vya Mungu vya kuwapa wengine upendeleo ni tofauti kabisa na vile vya mwanadamu. Hata hivyo, ni lazima tujitahidi kuongozwa na njia zake ikiwa tunataka kupata upendeleo machoni pake. Hiyo inamaanisha kwamba ni lazima tujifunze kuwaona wengine kulingana na maoni ya Mungu na si kulingana na viwango vya kibinadamu, jinsi ambavyo huenda vikaathiriwa na ubinafsi na ubaguzi. Twaweza kufanyaje hilo?

Yehova Mungu huchunguza moyo wa mtu na hupendelea wale wanaoonyesha sifa kama vile upendo, wema, fadhili, na ustahimilivu. Tunapaswa kufanya vivyo hivyo. (1 Samweli 16:7; Wagalatia 5:22, 23) Kwa kadiri tuwezavyo tukiwa wanadamu, tunahitaji kuchunguza mtu wa kindani, na si rangi ya ngozi yake au malezi yake ya kikabila. Badala ya kuwatafuta wale walio matajiri wa vitu vya kimwili, twafanya vema kukumbuka maoni ya Mungu juu ya mali na kujitahidi ‘kuwa matajiri kwa kutenda mema, kuwa tayari kutoa mali zetu, kushirikiana na wengine kwa moyo.’ (1 Timotheo 6:18) Ili kupata upendeleo wa Mungu, ni lazima tuendelee kutafuta maarifa sahihi ya Mungu na Mwana wake, Yesu Kristo, kuwa wenye kuelimishwa vema katika lugha iliyo safi ya kweli. (Yohana 17:3, 17) Kwa kufanya hivyo, sisi pia tutakuwa miongoni mwa wale ambao Mungu hupendelea.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki