Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 4/15 kur. 4-6
  • Mateso ya Milele—Kwa Nini ni Fundisho Linalofadhaisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mateso ya Milele—Kwa Nini ni Fundisho Linalofadhaisha?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Madokezo ya Kiadili
  • Helo na Haki
  • Kulitetea Fundisho Hilo
  • Helo—Mateso ya Milele au Kaburi la Ujumla?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Watu Wanauonaje Moto wa Mateso Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Fundisho Lililoenea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Moto wa Mateso Ni Halisi? Kuzimu Ni Wapi Kulingana na Biblia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 4/15 kur. 4-6

Mateso ya Milele—Kwa Nini ni Fundisho Linalofadhaisha?

“Nasikia kwamba mlimwondosha Pasta wenu. Tatizo lilikuwa nini?”

“Alikuwa akituambia sikuzote kwamba sote tunaenda helo.”

“Pasta mpya anasema nini?”

“Pasta mpya husema kwamba tunaenda helo, pia.”

“Kwa hiyo tofauti ni nini?”

“Tofauti ni kwamba yule pasta wa zamani aliposema hivyo, alisikika kana kwamba alifurahia jambo hilo; lakini huyo mpya anaposema hivyo, anasikika kana kwamba anaumia sana moyoni.”

HADITHI hiyo ikiwa imesimuliwa katika kitabu chenye vielezi, huonyesha kwa njia yayo yenyewe kwamba walimu wengi wa Biblia, pamoja na wahudhuriaji-kanisa, hawana starehe na fundisho la helo. Kwa kuhusisha mambo mengi zaidi, hadithi hiyo huhakikisha pia yale ambayo yule mwanatheolojia wa Kanada Clark H. Pinnock alisema: “Miongoni mwa habari zote za theolojia ambazo zimetatiza dhamiri ya kibinadamu kwa muda wa karne ambazo zimepita, nadhani ni chache tu ambazo zingeweza kuwa zimesababisha wasiwasi mkubwa zaidi kuliko ule ufasiri wa helo uliokubaliwa wa kuwa adhabu ya milele yenye kuhisiwa mwilini na nafsini.”

Madokezo ya Kiadili

Kwa hiyo, kwa nini wengi hufadhaishwa na zile mandhari za moto unaowaka zinazotolewa na Jumuiya ya Wakristo? (Ona kisanduku.) Profesa Pinnock asema hivi: “Wazo la kwamba kiumbe chenye ufahamu chapaswa kupatwa na mateso ya kimwili na ya kiakili kupitia wakati usio na mwisho linafadhaisha sana, na lile wazo la kwamba [mateso] hayo yanaamriwa kimungu linaudhi sadikisho langu kuhusu upendo wa Mungu.”

Naam, fundisho la mateso ya milele hutokeza tatizo la kiadili. Kwa mfano, Wakristo wenye mioyo myeupe hufikiria yale maswali yaliyotokezwa na mwanatheolojia mmoja Roma Katoliki Hans Küng: “Je! Mungu mwenye upendo angeweza . . . kutazama kwa umilele wote mateso ya kimwili na ya kiakili ya viumbe vyake yasiyo na mwisho, yasiyo na tumaini, yasiyo na huruma, yasiyo na upendo?” Küng aendelea hivi: “Je! yeye ni mdai mwenye moyo mgumu? . . . Tungefikiri nini juu ya mwanadamu ambaye angeridhisha tamaa yake ya kulipiza kisasi kwa njia isiyotulizika wala kutosheleka?”a Kwa kweli, Mungu anayetuambia katika Biblia kwamba tunapaswa kuwapenda maadui wetu angewezaje kutamani kuwatesa maadui wake kwa umilele? (1 Yohana 4:8-10) Haishangazi kwamba, watu fulani hukata maneno kwamba asili ya helo haipatani hata kidogo na asili ya Mungu, kwamba fundisho hilo halipatani na maoni ya kiadili.

Waamini wengine wengi hujaribu kutuliza dhamiri yao kwa kuepuka maswali hayo. Lakini Kuyapuuza maswali hayo hakufanyi kufadhaika huko kutoweke. Kwa hiyo acha tukabili suala hilo. Ni nini madokezo ya kiadili yanayohusiana na fundisho hilo? Katika Criswell Theological Review, Profesa Pinnock aandika hivi: “Mateso ya milele hayavumiliki kwa maoni ya kiadili kwa sababu yanamwonyesha Mungu kuwa dubwana lenye hamu ya kumwaga damu linalodumisha Auschwitz [kambi ya mateso] ya milele kwa majeruhi ambao yeye hata hawaruhusu wafe.” Yeye auliza hivi: “Mtu yeyote mwenye huruma anaweza kukaaje akiwa mtulivu akifikiria wazo kama hilo [lile fundisho la helo la kimapokeo]? . . . Wakristo wanaweza kuonyeshaje kiabudiwa chenye ukatili na kisasi cha jinsi hiyo?”

Akionyesha ule uvutano mwovu ambao huenda ikawa fundisho hilo limekuwa nao juu ya mwenendo wa wanadamu, Pinnock aeleza hivi: “Hata najiuliza ni ukatili gani mbalimbali ambao umetendwa na wale ambao wameamini katika Mungu anayetesa maadui wake?” Yeye amalizia hivi: “Je! hilo si wazo linalofadhaisha zaidi ambalo lahitaji kuchunguzwa tena?” Naam, ikiwa Mungu anahesabiwa ukatili wa jinsi hiyo, haishangazi kwamba wahudhuriaji-kanisa ambao ni wepesi wa kuona mambo yasiyofaa wanachunguza tena moto wa helo. Nao wanaona nini? Tatizo jingine linalokabili lile wazo la mateso ya milele.

Helo na Haki

Wengi wanoachunguza lile fundisho la helo la kimapokeo huona kwamba linaonekana kumwonyesha Mungu kuwa mwenye kutenda bila haki, kwa hiyo linaudhi hisi yao ya asili juu ya haki. Katika njia gani?

Waweza kupata jibu moja kwa kulinganisha fundisho la mateso ya milele na kiwango kimoja cha haki kilichopewa na Mungu: “Jicho kwa jicho, jino kwa jino.” (Kutoka 21:24) Ili kutoa hoja, tumia ile sheria ya kimungu iliyotolewa kwa Israeli wa kale, sheria ya malipo yaleyale, kuhusu lile fundisho la moto wa helo. Waelekea kufikia mkataa gani? Kwamba ni wale watenda dhambi tu ambao wamesababisha mateso ya milele ndio wanaostahili mateso ya milele yaleyale pia—mateso ya milele kwa mateso ya milele. Lakini kwa kuwa wanadamu (hata wawe waovu jinsi gani) wanaweza tu kusababisha mateso yenye kikomo, kuwahukumia mateso ya milele kunatokeza hali isiyosawazika kati ya uhalifu wao na ile adhabu isiyo na kikomo ya moto wa helo.

Kusema sahili, adhabu hiyo ingekuwa kali mno. Ingepita kwa mbali “jicho kwa jicho, na jino kwa jino.” Inapokumbukwa kwamba mafundisho ya Yesu yalipunguza wazo la kisasi, waweza kukubali kwamba Wakristo wa kweli wangeliona kuwa jambo gumu sana kuona haki katika mateso ya milele.—Mathayo 5:38, 39; Warumi 12:17.

Kulitetea Fundisho Hilo

Hata hivyo, waamini wengi wanaendelea kujaribu kulitetea fundisho hilo. Jinsi gani? Mbuni vitabu mmoja Mwingereza Clive S. Lewis huwanenea watetezi wengi wa fundisho hilo katika kitabu chake The Problem of Pain: “Hakuna fundisho ambalo ningeondoa kwa moyo wa kupenda kutoka kwa Ukristo kuliko hili, ikiwa ningalikuwa na uwezo wa kufanya hivyo. Lakini lina utegemezo kamili wa Andiko na, hasa, wa maneno ya Bwana Yetu mwenyewe.” Hivyo, wenye kuliunga mkono huungama kwamba mateso ya milele ni jambo lenye kufadhaisha, lakini wakati uo huo, wao huona fundisho hilo kuwa la lazima kwa sababu wanahisi kwamba Biblia hulifundisha. Mwanatheolojia Pinnock asema hivi: “Kwa kukiri kutokupendeza kwalo, wao hutumaini kuthibitisha uaminifu wao thabiti kwa Biblia na ushujaa fulani katika kuamini kwao kweli hiyo yenye kuhofisha sana kwa sababu tu andiko hulifundisha. Wanafanya lionekane kwamba kweli ya Biblia imo hatarini. Lakini, je, imo hatarini kwelikweli?

Wewe pia huenda ukataka kujua kama uaminifu kwa Biblia haukupi la kufanya ila kukubali fundisho hilo. Kwa kweli Biblia husema nini kuhusu helo?

[Maelezo ya Chini]

a Eternal Life?—Life After Death as a Medical, Philosophical, and Theological Problem, ukurasa 136.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

MAONI MATATU YALIYOFANANA

Ile imani iitwayo Ungamo la Imani la Westminister, inayokubaliwa na Waprotestanti wengi, hutaarifu kwamba wale wasioenda mbinguni “watatupwa katika mateso ya milele, na kuadhibiwa kwa uangamizo wa milele.” (The Confession of Faith, 33:2) “Katika Ukristo wa Roma Katoliki,” yaeleza The Encyclopedia of Religion, “helo huonwa kuwa hali ya adhabu isiyokoma . . . inayotokezwa hasa . . . na kule kuteseka kwa moto na mateso mengine.” Ensaiklopedia hiyo huongeza kwamba “Ukristo wa Orthodoksi ya Mashariki” hushiriki “lile fundisho kwamba helo ndio mwisho wa moto wa milele na adhabu inayowangojea waliolaaniwa.”—Buku 6, kurasa 238-9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki