Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 4/15 kur. 28-30
  • Je! Wewe Unafanya Yote Kabisa Uwezayo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unafanya Yote Kabisa Uwezayo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Kwaweza Kuongezwa
  • Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Katika Kuwasaidia Wengine
  • Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Katika Kuonyesha Kupendezwa Kibinafsi
  • Wewe Fanya Yote Kabisa Uwezayo
  • “Fanyeni Hata Zaidi Yote Kabisa Mwezayo”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kufanya Yote Yote Tuwezayo Tuzitangaze Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kuishi kwa Kupatana na Wakfu Wetu “Kila Siku”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Aliazimia Aishi Kulingana na Viwango vya Adili za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 4/15 kur. 28-30

Je! Wewe Unafanya Yote Kabisa Uwezayo?

“NITAFANYA kadiri niwezavyo.” Ni mara nyingi kadiri gani maneno hayo hufuatwa na neno “lakini” na orodha ndefu ya udhuru mbalimbali kwa kutokujikakamua! Namna gani wakfu wetu kwa Yehova? Je! tunatimiza ahadi yetu ya kumfanyia yote kabisa tuwezayo?

Kujiweka wakfu humaanisha ‘mtu kujitoa mwenyewe kabisa kwa ajili ya utumishi au ibada ya nafsi ya kimungu au ya matumizi matakatifu.’ Yesu alifanya mengi kuonyesha kile ambacho kujiweka wakfu kwa Yehova kwamaanisha kwa kusema hivi: “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba [mti wa mateso, NW] wake, anifuate.” (Mathayo 16:24) Mtu ambaye amejikana mwenyewe na kujiweka wakfu kwa Mungu hufanya kule kutimiza mapenzi ya kimungu kuwe ufuatiaji wa maana zaidi maishani mwake.

Tukiwa watu waliojiweka wakfu, ni lazima tujichunguze wenyewe kuona kama tunaishi kulingana na wakfu wetu. Petro alionyesha sababu kwa nini tunapaswa kujichunguza wenyewe alipowatia moyo Wakristo wapakwa-mafuta hivi: “Jitahidini zaidi [fanyeni yote kabisa mwezayo, NW] kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.” (2 Petro 1:10) Naam, tukifanya yote kabisa tuwezayo, hatimaye hatutakuja kuwa wenye kutofaulu kiroho.

Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Kwaweza Kuongezwa

Kwa maana pana zaidi, watumishi wote wa Mungu ambao wamejiweka wakfu wanatazamiwa kufanya yote kabisa wawezayo, au kadiri wawezavyo, kumpendeza Yehova. Hata hivyo, kufanya yote kabisa tuwezayo katika kutimiza mapenzi ya Mungu kwaweza kuongezeka. Kwa mvulana wa miaka mitatu, kutimiza kazi ndogo huenda kukawa kadiri awezavyo kufanya kumsaidia mama yake, lakini anapokua kuwa mwenye umri mkubwa zaidi, ataweza kufanya zaidi. Vilevile kwa ukuzi wetu wa kiroho—yale yaliyokuwa yote kabisa tuwezayo kufanya wakati mmoja huenda yasiwe hivyo tena. Tunasukumwa kumfanyia Yehova zaidi.

Uthamini wetu wenye kuongezeka kwa Yehova huchochea nia yetu ya kufanya zaidi. Kuthamini yale ambayo ametufanyia kunaimarishwa kupitia funzo la kibinafsi la neno lake, Biblia. Kwa kielelezo, tunapochunguza kwa uangalifu na kutafakari juu ya jinsi Yehova alivyomtuma Mwana wake asalimishe nafsi yake ili kukomboa ainabinadamu kutoka kwa dhambi, tunasukumwa kumtumikia yule Mwanzilishi wa mpango wa fidia. (Yohana 3:16, 17; 1 Yohana 4:9-11) Kadiri ‘tunavyoonja na kuona ya kuwa Yehova yu mwema,’ ndivyo mioyo yetu inavyosukumwa kumtumikia.—Zaburi 34:8.

Mhudumu mmoja wa wakati wote aitwaye Jetter aling’amua hilo. Ili kuchunguza kwa kina zaidi yale aliyokuwa akijifunza, aliweka kando chumba kidogo katika nyumba yake kwa kusudi hilo. Alikipanga ili aweze kukaza fikira zake alipokuwa akifanya utafiti. Yeye ana Watch Tower Publications Indexes pamoja na mabuku yaliyojalidiwa ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwenye rafu ambayo ni karibu kufikiwa. “Ninapofanya utafiti wa habari yenye kupendeza,” yeye asema, “Nina hamu ya kuishiriki na wengine.”

Hata hivyo, kama vile kula chakula kitamu mara kwa mara hakutoshelezi uhitaji wa mtu wa kila siku wa kula chakula kwa ukawaida, utafiti wenye kina katika Biblia wa wakati mmoja haufuti ule uhitaji wa kila siku wa kutwaa chakula cha kiroho. Ruth huthamini uhitaji huo, kufikia wakati wa nyuma sana kadiri awezavyo kukumbuka, familia yake ilisoma Biblia pamoja kila asubuhi na jioni baada ya milo. Sasa, akiwa na umri wa miaka 81, akiwa ametumia miaka zaidi ya 60 katika huduma ya wakati wote, yeye bado husoma Biblia kwa ukawaida baada ya kuamka saa 12 za asubuhi. Mara anapopokea magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, Ruth hutafuta wakati wa kuyasoma. Yeye hupitia makala angalau mara tatu au nne kabla ya kujifunza makala hiyo kundini. “Kutwaa Neno la Mungu ni jambo unalohitaji hasa ili kuendelea kuwa imara katika imani,” yeye asema. Hilo limemsaidia pia aendelee katika utumishi wa mishonari kwa miaka mingi.

Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Katika Kuwasaidia Wengine

Kwa funzo la Neno la Mungu lenye kina na la kawaida, bidii yetu ya kumtumikia Mungu hukua, na kitu fulani ndani yetu kinatuhimiza tufanye zaidi. (Linganisha Yeremia 20:9.) Bidii ya jinsi hiyo ilimsukuma Hirohisa atimize huduma yake kikamili. (2 Timotheo 4:5) Aliishi katika familia yenye mzazi mmoja pamoja na ndugu na dada wanne wachanga zaidi. Alipokuwa tineja, Hirohisa alitegemeza familia yake kifedha kwa kuamka saa tisa za usiku ili kupeleka magazeti ya habari. Alitaka kufanya zaidi katika kuwaambia wengine kuhusu Yehova, kwa hiyo Hirohisa alipeleka ombi la utumishi wa painia, kama vile huduma ya wakati wote ya Mashahidi wa Yehova inavyoitwa. Akiwa mchanga hivyo, alifurahia kuwasaidia wengine wajiunge na yeye katika kufanya yote kabisa wawezayo kumsifu Yehova.

Kufanya kadiri tuwezavyo katika kuwasaidia wengine kunatia ndani kuwa wenye matokeo katika huduma yetu. Wakati mmoja Yesu aliwatia moyo wanafunzi wake hivi: “Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.” (Yohana 13:17) Naomi ni kielelezo kizuri cha kutumia madokezo yanayotolewa na tengenezo la Yehova ili kufanyia maendeleo huduma yetu. Alikuwa na tatizo la kusema na watu asiowafahamu nyumba kwa nyumba na mara nyingi hakujua la kusema aliposimama mlangoni. Wazee katika kundi walimhimiza atumie madokezo yanayopatikana katika kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, katika sehemu ya “Matangulizi ya Kutumia Katika Huduma ya Shambani.”a Alikariri yale matangulizi chini ya kichwa “Jamaa/Watoto” akajizoeza hayo mara nyingi. Likiwa tokeo, aliweza kuwa na mazungumzo pamoja na mke mmoja wa nyumbani aliyekuwa katika miaka yake ya 30. Hata kabla ya Naomi kuweza kufanya ziara ya kurudia, mwanamke huyo alikuja kwenye Jumba la Ufalme. Funzo la Biblia likaanzishwa. Mke huyo wa nyumbani pamoja na mume wake sasa ni Wakristo ambao wamebatizwa, wanaoonea shangwe maisha ya familia yenye furaha pamoja na watoto wao.

Kufanya Yote Kabisa Tuwezayo Katika Kuonyesha Kupendezwa Kibinafsi

Tunaweza pia kumwiga mtume Paulo, aliyesema hivi: “Nafanya mambo yote kwa ajili ya Injili ili kuishiriki pamoja na wengine.”—1 Wakorintho 9:22, 23.

Hatsumi huonyesha mtazamo huo. Hatsumi alipokuwa katika huduma ya hadharani, mwanamke mmoja alisema kwa adabu kwenye simu inayounganishwa na mlango kwamba yeye alikuwa na shughuli nyingi mno kuweza kuongea. Sauti ya mwenye nyumba huyo ilikuwa yenye uanana, kwa hiyo Hatsumi aliendelea kumtembelea. Mwenye nyumba huyo alijibu tu kupitia simu hiyo, asitoke kamwe kukutana na Hatsumi. Hilo liliendelea kwa muda wa miaka miwili na nusu.

Siku moja Hatsumi alibadili wakati wa ziara yake, alitembelea saa za baadaye za alasiri. Hakuna aliyejibu. Hata hivyo, alipokuwa akiondoka, sauti aliyofahamu kutoka nyuma yake ilimwuliza, “Wewe ni nani?” Mwanamke huyo alikuwa tu akirudi nyumbani. Aliposikia jina la Hatsumi, aliitikia upesi, “Ah, ni wewe ambaye umekuwa ukinitembelea. Asante sana kwa kunijali sikuzote.” Kwa sababu mwanamke huyo alikuwa ameacha kuendelea na funzo lake la Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova katika eneo jingine, alikuwa amekuwa na aibu mno kumfungulia Hatsumi mlango. Funzo la Biblia lilianzishwa tena, na mwenye nyumba huyo anafanya maendeleo vizuri sana. Je! sisi hujali vivyo hivyo wale tunaokutana nao katika huduma ya nyumba kwa nyumba?

Wewe Fanya Yote Kabisa Uwezayo

Yehova huthamini jitihada yetu ya kumtumikia kwa kufanya yote tuwezayo. Yeye ni kama baba ambaye mwana wake humjia na zawadi. Kwa muda wa miaka, zawadi yaweza kuwa tofauti kwa kutegemea umri na uwezo wa mwana huyo. Kama vile baba huyo hufurahi kupokea zawadi zozote za kuhisiwa moyoni ambazo mwana wake humpa, ndivyo ambavyo Yehova hukubali kwa utayari utumishi wetu wa moyo wote kulingana na ukuzi wetu wa kiroho.

Bila shaka, hakuna maana yoyote ya kulinganisha yale yote kabisa tuwezayo kufanya na yale ambayo wengine wawezayo kufanya. Kama vile Paulo asemavyo, tutakuwa na sababu ya kushangilia sana kwa habari yetu wenyewe, “si kwa [kulinganishwa na, NW] mwingine.” (Wagalatia 6:4) Na tuendelee kutii himizo hili la mtume Petro: “Fanyeni bidii [fanyeni yote kabisa mwezayo, NW] ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake.”—2 Petro 3:14.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

[Picha katika ukurasa wa 29]

Je! wewe unafanya yote kabisa uwezayo katika kutumia madokezo kwa ajili ya huduma ya shambani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki