Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 5/15 kur. 3-4
  • Jitihada ya Kutafuta Matabiri Yenye Kutegemeka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitihada ya Kutafuta Matabiri Yenye Kutegemeka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Matabiri ya Biblia Ni Yenye Kutegemeka Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kitabu Cha Unabii
    Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote
  • Kwa Nini Kuna Maonyo Mengi Bandia?
    Amkeni!—1993
  • Wakati Ujao Wako Njia Nzuri Zaidi ya Kujifunza Juu Yao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 5/15 kur. 3-4

Jitihada ya Kutafuta Matabiri Yenye Kutegemeka

“YEYE ambaye angeweza kuona mambo siku tatu kimbele angekuwa tajiri kwa maelfu ya miaka.” Ndivyo isemavyo mithali moja ya Kichina.

Watu hutaka kujua yale yatakayoletwa na wakati ujao, na wengi wangelipa fedha nyingi sana kwa utayari ili kupata habari yenye kutegemeka ya aina hiyo. Wanajitahidi kutafuta matabiri yenye kutegemeka. Kama ionwavyo kutokana na matabiri ya halihewa na matabiri ya kiuchumi, sisi tunapendezwa na matukio yaliyoko mbele. Tena zaidi ya hayo, ujuzi wenye kutegemeka wa wakati ujao ungetuwezesha tupange na kuratibu maisha zetu.

Tamaa ya kujua yale yatakayotukia wakati ujao huwachochea wengi wawaendee wapiga-ramli, waguru (viongozi wa kiroho), wanajimu, na walozi. Maduka ya vitabu na rafu za kuwekea magazeti zimejaa maandishi ya kale na ya ki-siku-hizi ya wale wanaodai kuutabiri wakati ujao. Lakini shaka huzunguka namna hizo za utabiri. Mwanatawala Mroma Kato aliripotiwa kuwa alisema hivi: ‘Nashangaa kwamba mpiga bao mmoja hacheki anapomwona mpiga bao mwingine.’

Bila shaka, kuna matabiri ya aina nyingi. Katika 1972 kikundi kimoja cha kimataifa cha wasomi na wafanya biashara kinachoitwa Club of Rome kilitangaza kwa chapa uchunguzi uliotabiri kwamba ulimwengu ungeishiwa karibuni na nyenzo zisizoweza kufanywa upya. Ungekuwa bila dhahabu kufikia 1981, bila zebaki kufikia 1985, bila zinki kufikia 1990, bila mafuta ya kipetroli kufikia 1992, na kadhalika. Tunaona sasa kwamba matabiri hayo hayakutimia.

Matabiri mengi yametegemea maoni ya kidini. Kutoa kielezi: Askofu mmoja wa Sakson Wulfstan aliamini kwamba Denmark kushambulia Uingereza mapema katika karne ya 11 ilikuwa ishara kwamba mwisho wa ulimwengu ulikuwa karibu. Katika 1525, Thomas Münzer aliongoza uasi wa wakaa-mashambani Wajerumani kwa sababu katika njozi aliona malaika wakinoa miundu kwa ajili ya yale aliyofikiria yangekuwa mavuno makubwa. Kwa wazi, matabiri hayo hayakuwa sahihi.

Kama vile huenda ikawa wajua, Biblia ina matabiri. Tena zaidi ya hayo, waandishi wa Biblia walidai kupuliziwa na Mungu. Mtume Mkristo Petro alisema hivi: “Hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW].”—2 Petro 1:20, 21.

Miongoni mwa mambo mengine, Biblia ilitabiri matukio mbalimbali ikitambulisha kile kizazi ambacho kingeona kuwapo kwa Yesu Kristo katika mamlaka ya Ufalme ya kimbingu. Vita isiyotangulia kuonwa, njaa kubwa, matetemeko ya dunia, na mvunjiko wa nguvu za kiadili za binadamu ingekuwa ishara ya zile ambazo Biblia husimuliwa kuwa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5; Mathayo 24:3-14, 34) Kulingana na Biblia, kuondolewa mbali kwa mfumo wa mambo uliopo kungefungulia njia furaha ya ainabinadamu katika ulimwengu mpya wenye baraka zisizo na mwisho.—2 Petro 3:13; Ufunuo 21:1-4.

Wewe huonaje matabiri ya Biblia ya jinsi hiyo? Je! hayo ni makisio-kisio tu, kama yale matabiri mengine mengi? Tunaweza kutahini hali ya kutegemeka ya unabii mwingi wa Biblia ambao haujatimizwa bado kwa kuchunguza kama matabiri ya Biblia kuhusu matukio yaliyopita yalitegemeka. Katika makala ifuatayo, tutachunguza baadhi yayo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Hisani ya National Weather Service

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki