Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 9/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Iweni Wanafunzi wa Kweli wa Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Dumisha ‘Tumaini Lako la Wokovu’!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Je! Utauitikia Upendo wa Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Hii Ndiyo Siku ya Wokovu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 9/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kwenye Warumi 9:3, mtume Paulo aliandika hivi: “Ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili.” Je! alimaanisha kwamba angedhabihu uhai wake ili kuwaokoa Wayahudi wenzake?

Yesu aliweka kielelezo bora mno cha upendo. Alikuwa tayari kusalimisha nafsi, au uhai wake, kwa ajili ya ainabinadamu yenye dhambi. Wakati wa huduma yake ya hadharani, alitumia nguvu zake kwa ajili ya wananchi wenzake—Wayahudi—ili kwamba wengi wao kadiri iwezekanavyo waweze kuwa miongoni mwa wale ambao wangenufaika kutokana na dhabihu yake ya fidia. (Marko 6:30-34) Kutoitikia kwao na kupinga kwao ujumbe wa wokovu hakukupunguza kamwe hangaiko la Yesu lenye upendo kwa ajili ya watu wa Kiyahudi. (Mathayo 23:37) Naye alituachia ‘kielelezo, tufuate nyayo zake.’—1 Petro 2:21.

Je! yawezekana kwa wanadamu wasio wakamilifu kufuata kielelezo cha Yesu cha upendo? Naam, twaweza kuona kielezi cha hilo katika mtume Paulo. Alihangaikia sana Wayahudi wenzake, hivi kwamba kwa sababu ya kuwapenda, alisema angetamani kwamba yeye mwenyewe ‘aharimishwe na kutengwa na Kristo’ kwa ajili yao.

Hapo Paulo alitumia namna ya chuku, au kutia chumvi, ili kueleza jambo hilo. Yesu alitumia namna iyo hiyo ya kutia chumvi kwenye Mathayo 5:18, aliposema hivi: “Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.” Yesu alijua kwamba mbingu na dunia hazingeondoka. Paulo asingeharimishwa, wala Wayahudi wote wasingekubali Ukristo. Lakini jambo ambalo Paulo alitaka kuonyesha ni kwamba angefanya jambo lolote kabisa ili kuwasaidia Wayahudi wajifaidi wenyewe na njia ya Mungu ya wokovu kupitia Yesu Kristo. Haishangazi kwamba mtume huyo angeweza kuwatia moyo Wakristo wenzake hivi: “Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo”!—1 Wakorintho 11:1.

Leo, Wakristo wanapaswa kuwa na hangaiko lilelile ambalo Yesu na Paulo walikuwa nalo kwa ajili ya wasioamini. Hatupaswi kamwe kuruhusu kutopendezwa au upinzani wa moja kwa moja kutoka kwa watu katika eneo letu la kutoa ushahidi upunguze upendo wetu kwa majirani wetu wala bidii yetu ya kuwasaidia wajifunze njia ya wokovu.—Mathayo 22:39.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki