Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 9/15 kur. 3-4
  • Je, Wewe ni Mwenye Kusamehe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe ni Mwenye Kusamehe?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Msamaha ni Mwito Mgumu
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Samehe Kutoka Katika Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Msameheane Kwa Hiari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Uwe Mwenye Kusamehe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 9/15 kur. 3-4

Je, Wewe ni Mwenye Kusamehe?

BILL na binti yake mwenye miaka 16, Lisa, hawakuwa wakisikilizana sana. Kutokubaliana kati yao kwa mambo madogo-madogo mara nyingi kulitokeza mifoko mikali. Hatimaye, hali hiyo ya kutosikilizana iliongezeka kufikia hatua ya Lisa kuambiwa aondoke nyumbani.a

Baada ya muda, Lisa alikuja kutambua kwamba alikuwa amekosea naye akatafuta msamaha kwa baba yake. Lakini badala ya kuachilia makosa yaliyopita ya Lisa, baba yake mwenye uchungu mwingi wa moyo alikataa jitihada zake za kufanya amani. Ebu wazia! Alikataa kumwonyesha rehema binti yake mwenyewe!

Karne nyingi zilizopita mtu mmoja asiye na kosa alihukumiwa kifo kwa sababu ya uhalifu ambao hakufanya. Mashahidi walitoa ushuhuda bandia, na maofisa wa kisiasa walikataa kimakusudi kutekeleza haki. Mtu huyo asiye na hatia alikuwa Yesu Kristo. Muda mfupi kabla afe, kwa sala alimwomba Mungu hivi: “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo.”—Luka 23:34.

Yesu alisamehe kabisa, kutoka kwa moyo wake, na wafuasi wake walihimizwa wamwige kwa jambo hilo. (Waefeso 4:32) Hata hivyo, kama Bill, wengi hawataki kusamehe kutoka moyoni. Je, wewe unafanyaje kwa jambo hilo? Je, wewe ni tayari kusamehe wengine wanapokukosea? Na vipi juu ya dhambi zilizo nzito? Je, ni lazima hizo pia zisamehewe?

Msamaha ni Mwito Mgumu

Si rahisi sikuzote kusamehe. Na katika nyakati hizi zilizo ngumu, mahusiano ya kibinadamu yamekuwa yenye matatizo hata zaidi. Mara nyingi maisha ya familia hujawa na mikazo na mibano. Hapo zamani mtume Mkristo Paulo alisema kwamba hali kama hizo zingeenea katika “siku za mwisho.” Yeye alisema hivi: “Watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, . . . wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna.”—2 Timotheo 3:1-4.

Kwa hiyo basi, ni lazima sisi sote tukabili mibano ya nje ijaribuyo uwezo wetu wa kusamehe wengine. Na zaidi, sisi hushindana pia na nguvu zilizo ndani yetu. Paulo aliomboleza: “Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.” (Warumi 7:19, 20) Matokeo ni kwamba wengi wetu si wenye kusamehe kwa jinsi ambavyo tungependa. Kwani, kutokamilika kulikorithiwa na dhambi huwa na uvutano mkubwa sana juu yetu sisi sote, nyakati nyingine ikitufanya tusiwe wenye huruma kwa wanadamu wenzetu.

Mwanamke mmoja alipotiwa moyo amsamehe mwingine kwa sababu ya kosa dogo, yeye alijibu: “Hakuna mtu astahiliye ile jitihada ya kusamehe.” Kijuu-juu maelezo kama hayo yaweza kuonekana kama ni ya kutojali, yasiyo na huruma, na hata yenye madharau. Lakini ukitazama kindani zaidi, twaona kwamba yanafunua mfadhaiko ambao watu wengi huhisi wakabilipo ulimwengu ambao wao waona kuwa wenye uchoyo, usiojali, na ulio mkali. Mtu mmoja alisema hivi: “Watu hukutumia vibaya unapowasamehe. Ni kama kukanyagwa-kanyagwa kama kitambaa cha kupangusia mguu.”

Basi, si ajabu kwamba ni vigumu sana kusitawisha mtazamo wa kusamehe katika siku hizi za mwisho. Bado, Biblia yatutia moyo kusamehe kwa fadhili. (Linganisha 2 Wakorintho 2:7.) Kwa nini tuwe wenye kusamehe?

[Maelezo ya Chini]

a Majina yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki