Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 10/1 kur. 3-4
  • Biblia—Ina Thamani Gani Hasa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia—Ina Thamani Gani Hasa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kila Andiko Ni Lenye Manufaa kwa Kufundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Mafundisho ya Kweli Yanayompendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Zawadi Inayotoka kwa Yehova Mwenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 10/1 kur. 3-4

Biblia—Ina Thamani Gani Hasa?

“BIBLIA ni fumbo, kitabu ambacho hakikukusudiwa kueleweka,” adai mwenye nyumba fulani. Mwingine aeleza hivi: “Najua kwamba Biblia ni kitabu cha maana, lakini sijui mengi kukihusu. Ni vigumu kukifahamu.”

“Wakristo wengi wanajua . . . machache kuhusu Biblia,” laeleza The Toronto Star. Mwanamke mmoja Mkatoliki alieleza hivi: “Kuwa na Biblia hunifanya nihisi vizuri. Huleta amani ya ndani.” “Biblia ni kama dira inayokuongoza ili upite magumu na machafuko ya bahari ya maishani hadi mahali pa usalama,” akasema mvuvi mmoja. Katika maneno ya mmoja aliyekuwa Mhindu, “Biblia ni Neno la Mungu na zawadi kwa binadamu na ni dawa ya mauguzi ya kiroho.”

Maoni kuhusu thamani halisi ya Biblia ni mengi na yanatofautiana. Lakini ina thamani gani hasa?

Biblia ndicho kitabu kilichopo cha maana zaidi na chenye kugawanywa zaidi. Ndani ya kurasa zayo mna majibu ya matatizo yenye kutatanisha sana ambayo mwanadamu amepata au atakuja kupata. Kutumika kwa shauri lake hakulinganiki. Viwango vya adili inavyotetea havina kifani. Habari zake zina nguvu na zenye manufaa. Kitabu hiki cha thamani isiyolinganika chapasa kitolewe maktabani mwetu na kuchunguzwa kwa uangalifu na kwa makini.

Twaweza kufungua Biblia kwa uhakika kabisa kwamba ni sahihi kabisa, inategemeka, na ni asilia. Matukio ya historia yaliyorekodiwa ndani yayo yanathibitishwa na historia ya kilimwengu. Mavumbuzi ya kiakiolojia huthibitisha kwa kurudiarudia kwamba Biblia ni yenye uhakika na kweli. Unyoofu wa waandikaji wa Biblia wapatao 40 hivi huwatambulisha kuwa watu wenye haki na washika uaminifu-maadili. Upatano wa kindani wa Biblia huonyesha kwamba chanzo chayo si cha kibinadamu. Matukio yaliyorekodiwa ndani yamo ni halisi. Watu isemayo juu yao ni halisi. Mahali na sehemu ielezazo ni halisi. Zaidi ya hayo, Biblia ina unabii mbalimbali wenye kutokeza unaotambulisha bila kukana kwamba Yehova Mungu ni Mwandikaji wa Biblia.—2 Petro 1:21.

Mfunzi Mkuu wetu alihakikisha kuwa ujuzi wa mapenzi na makusudi yake ungepatikana kwa wale waliotaka kuyajua. Kwa kweli, Yehova hutueleza kwa lugha iliyo wazi kwamba ni mapenzi yake watu wa aina zote wajifunze Neno lake na “kupata kujua yaliyo kweli.” (1 Timotheo 2:3, 4; Mithali 1:5, 20-33) Hili ni mojapo mambo ya maana zaidi tuwezalo kufanya katika maisha zetu. Ni mwito tunaolazimika kukabili. Wakristo wa mapema walifahamu hili. Mmoja wao alisukumwa kusema: “Na hii ndiyo dua yangu, kwamba pendo lenu lizidi kuwa jingi sana, katika hekima (“ujuzi sahihi,” New World Translation) na ufahamu wote; mpate kuyakubali yaliyo mema.”—Wafilipi 1:9, 10; Wakolosai 1:9, 10.

Biblia ndiyo njia kuu ya Muumba ya kuwasilisha mapenzi na kusudi lake kwa familia ya wanadamu, na yaeleza jinsi sisi mmoja-mmoja tunavyoingia ndani ya kusudi hilo. Ndani yamo kumerekodiwa matukio ya kale, na yanatupa maono ya wazi ya wakati ujao. Biblia ina mafundisho sahihi na yatujulisha mambo tupaswayo au tusiyopaswa kuamini. (Matendo 17:11; 2 Timotheo 3:16, 17) Huandaa kanuni za mwenendo ambazo mtu apaswa kuishi kwazo, na huongoza wanadamu katika njia ya mafanikio na furaha. (Mathayo, sura 5 hadi 7) Inakazia Ufalme wa Mungu kuwa tumaini la pekee kwa wanadamu wote na kuonyesha jinsi serikali yake ilivyo chombo cha kutakasa jina lake na kutetea enzi kuu yake. Biblia hueleza mwendo tupaswao kufuata ili kufurahia uhusiano wa karibu wenye upendo pamoja na Mpaji-Uhai wetu, Yehova.

Zaidi ya hayo, Biblia ndiyo kitabu pekee kitakachokuongoza kwenye zawadi kubwa zaidi awezayo kupata mwanadamu—uhai wa milele katika paradiso duniani wakiwa binadamu wakamilifu. (Warumi 6:23) Mwana wa pekee wa Yehova hutuambia: “Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3, NW) Kwa kweli kitabu chenye thamani kubwa jinsi hii chapasa kutuchochea kujifunza tunayopaswa kufanya ili tupate uhai wa milele. Biblia ni kitabu kilichokusudiwa kueleweka, kama makala ifuatayo itakavyoonyesha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki