Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 3/15 kur. 29-31
  • Je, Wewe Utamsifu Yehova?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Utamsifu Yehova?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sifu Mungu kwa Kutangaza Habari Njema
  • Msaada Upatikanao
  • Saidia Watoto Wamsifu Yehova
  • Uhusiano wa Milele Pamoja na Yehova
  • Waliotengwa Wawe Wasifaji Wenye Shangwe Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu
    Mwimbieni Yehova
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 3/15 kur. 29-31

Je, Wewe Utamsifu Yehova?

“KAMA lilivyo jina lako, Ee Mungu, ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia.” Haya ni maneno katika wimbo wa kiunabii wa wana wa Kora. (Zaburi 48:10) Leo, korasi kubwa ya mamilioni ya Mashahidi wa Yehova inamsifu Mungu na kujulisha jina lake kwa kuhubiri habari njema za Ufalme wake. Kwa kufanya hivyo katika nchi na visiwa vya bahari 232 na kwa zaidi ya lugha 300, wanafikia kihalisi “miisho ya dunia.”

Ni kitu gani hicho husukuma watu wa malezi mbalimbali wa kitamaduni, kijamii, na lugha kumsifu Yehova? Uthamini wao wa ujuzi sahihi wa Neno la Mungu, Biblia, ndio sababu kubwa. Kweli ya kiroho imewaweka huru kutokana na ushirikina na imani zinazotumikisha kama ile ya mateso ya milele. (Yohana 8:32) Ile kweli pia huwasaidia kuthamini sifa za ajabu za Mungu, kama vile upendo wake, uwezo, hekima, na haki iliyochanganywa na rehema. Kupata kufahamu kutoa kwa Mungu Mwanaye pekee, Yesu Kristo, akiwa dhabihu ya fidia kwa binadamu huchochea watu wenye haki kusifu na kumtumikia Yehova.

Kulingana na kitabu cha Biblia cha Ufunuo, korasi ya kimbingu yasema: “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.” (Ufunuo 4:11) Sifa kama hiyo haitokani na kuhisi tu tukiwa na daraka. Badala ya hivyo, inatokana na staha kwa Yehova.

Sifu Mungu kwa Kutangaza Habari Njema

Katika kumsifu Yehova, mtu huiga kielelezo bora kabisa cha Yesu Kristo, aliye msifaji mkuu wa Mungu. Kufuata katika hatua za Yesu kunatia ndani kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. (Mathayo 4:17, 23; 24:14) Utendaji huu wa kuhubiri umekuwa jitihada kubwa kuliko zote ulimwenguni kote za kumsifu Yehova.

Kazi hii ya kuhubiri ni ya maana sana hivi kwamba Biblia kwa wazi huilinganisha na wokovu. Warumi 10:13-15 lasema: “Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!”

Katika mwaka uliopita pekee, Mashahidi wa Yehova walihubiri zaidi ya saa bilioni moja. Na ni matokeo gani mazuri yaliyopatikana kutokana na huko kumsifu Mungu! Watu karibu 314,000 walijiunga na korasi ya wasifaji hao kwa kuonyesha wakfu wao kwa Yehova kwa ubatizo wa maji.

Hata hivyo, ni jambo gani laweza kusemwa kuhusu wale 12,288,917 waliohudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo mwaka wa 1994? Miongoni mwao mlikuwamo zaidi ya 7,000,000 ambao bado hawamsifu Yehova wakiwa wahubiri wa habari njema. Lakini kuwapo kwao katika tukio hili muhimu kungeweza mwishowe kuleta tokeo la ongezeko la mamilioni mengi zaidi ya korasi ya wasifaji. Ni jambo gani laweza kufanywa ili kusaidia hawa wenye kupendezwa wawe wasifaji wa Yehova?

Msaada Upatikanao

Watu wengi wenye kupendezwa huenda wakawa na tamaa ya kumsifu Yehova lakini wahisi kwamba hawawezi kufikia matakwa. Wao wanafanya vema kukumbuka maneno haya ya mtunga-zaburi: “Nitayainua macho yangu niitazame milima; msaada wangu utatoka wapi? Msaada wangu u katika BWANA, aliyezifanya mbingu na nchi.” (Zaburi 121:1, 2) Inaonekana kwamba mtunga-zaburi aliinua macho yake kuitazama milima ya Yerusalemu mahali hekalu la Yehova na makao ya kidunia ya serikali ya kitheokrasi yalipokuwa. Kutokana na hili twaweza kwa kufaa kukata maneno kwamba msaada unaotakiwa ili kumsifu Mungu na kutangaza ujumbe wa Ufalme hutoka tu kwa Yehova na tengenezo lake.—Zaburi 3:4; Danieli 6:10.

Leo, wale watamanio kumsifu Yehova wanaweza kutazamia msaada wenye upendo kutoka kwa tengenezo lake la kidunia. Kwa kielelezo, Mashahidi wa Yehova hujitolea kusaidia watu wenye kupendezwa kwa kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani bila malipo. Programu hii ya elimu inatia ndani mengi kuliko kujifunza mafundisho ya Biblia tu. Inasaidia mwanafunzi kukuza uthamini kwa yale anayojifunza na kwa tengenezo ambalo Yehova anatumia.

Kupatana na hili, Shahidi anayeongoza funzo la Biblia hujaribu kuhakikisha kwamba kweli mpya anazofundisha zinaingia akilini na moyoni. Na mwalimu asikose kumwonyesha mwanafunzi jinsi Yehova anavyotumia tengenezo Lake kutimiza kusudi Lake hapa duniani. Ile broshua Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote na ile tepu ya vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name mara nyingi vimethibitika kuwa vyenye manufaa katika kutimiza jambo hili.

Mikutano ya Kikristo pia huwa na sehemu kubwa katika kusaidia wale watakaokuwa wasifaji wa Yehova. Kwenye mwanzo-mwanzo wa funzo la Biblia, mwanafunzi aweza kukaribishwa kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Baada ya muda, atajifunza umuhimu wa kuhudhuria na kushiriki kwa ukawaida katika mikutano yote ya kutaniko. (Waebrania 10:24, 25) Waangalizi wanaweza kuandaa msaada ufaao kwa waamini wenzi na kwa wale watakaokuwa wasifaji wa Yehova kwa kutayarisha mikutano yenye kujenga na kutumika kiroho.

Saidia Watoto Wamsifu Yehova

Watoto wamo miongoni mwa wengi ambao wangeweza kuwa wahubiri wa habari njema katika wakati ujao ulio karibu. Hasa akina baba wana daraka la Kibiblia la kulea watoto wao “katika adabu na maonyo ya Bwana.” (Waefeso 6:4) Hata watoto wachanga sana waweza kusitawisha tamaa ya kumsifu Yehova wanapozoezwa vizuri.

Msichana mmoja mchanga katika Argentina aliwaendea mara nyingi wazee wa kutaniko kwa muda wa miezi kadhaa, akiwaomba msaada wao ili astahili kuwa mhubiri wa Ufalme. Baada ya muda, wazazi wake pamoja na wazee wakakubali kumruhusu awe mhubiri asiyebatizwa. Tayari yeye anatoa ujumbe wa Ufalme kwa matokeo kwenye milango. Ingawa msichana huyu mdogo ni mwenye umri wa miaka mitano tu na hajui kusoma, amekariri mahali mistari ya Biblia inapopatikana. Baada ya kupata andiko, yeye humuuliza mwenye nyumba alisome, kisha yeye hutoa maelezo.

Ni wazi kwamba wazee na wazazi wanaweza kutimiza mambo mengi kwa kutia moyo na kusaidia wanaofanya maendeleo kuelekea kuwa wasifaji wa Yehova.—Mithali 3:27.

Uhusiano wa Milele Pamoja na Yehova

Hata hivyo, vipi ikiwa wewe umekuwa ukishirikiana na Mashahidi wa Yehova kwa muda fulani lakini bado hujajiunga nao katika kazi yao ya kuhubiri? Huenda kukawa na manufaa kujiuliza maswali yafuatayo, ‘Je, ninaamini kwamba nimepata kweli na kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli? Je, nimesadiki kwamba Ufalme wa Mungu ndio suluhisho pekee kwa matatizo ya binadamu? Je, nimeacha dini yote ya uongo na mila na mazoea ya kilimwengu yasiyompendeza Yehova? Je, ninao upendo wenye kina kwa Mungu na kwa matakwa yake maadilifu?’ (Zaburi 97:10) Ukiweza kujibu ndiyo kwa unyoofu maswali hayo, nini kinachokuzuia kumsifu Yehova?—Linganisha Matendo 8:36.

Kumsifu Yehova kunatia ndani mengi zaidi ya kuhubiri habari njema tu. Ikiwa umepata ujuzi sahihi, una imani ya kweli, nawe unapatanisha maisha yako na matakwa ya kimungu, unahitaji kuongeza uhusiano wako binafsi pamoja na Mungu. Jinsi gani? Kwa kujiweka wakfu kwake kwa sala halafu kuonyesha hili kwa kubatizwa kwa maji. Uhai wa milele uko hatarini. Hivyo, tenda sasa kulingana na shauri la Yesu: “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.”—Mathayo 7:13, 14.

Mfumo huu wa mambo ukaribiapo mwisho wake wenye msiba, huu si wakati wa kusitasita. Chukua hatua mara moja kuelekea uhusiano wa milele pamoja na Yehova. Kwa kweli huu ndio wakati wa kuitikia ndiyo kwa swali hili, Je, utamsifu Yehova?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki