Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 8/1 kur. 3-4
  • Nyakati Zimebadilika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nyakati Zimebadilika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Sulemani Atawala kwa Hekima
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Je, Yeye Ni Mfano Mzuri au Ni Onyo Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wafungwa wa Umaskini
    Amkeni!—1998
  • Jitihada za Kumaliza Umaskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 8/1 kur. 3-4

Nyakati Zimebadilika

NI LAZIMA iwe ilikuwa shangwe kama nini kuishi katika Israeli ya kale chini ya utawala mtukufu wa Mfalme Sulemani mwaminifu! Kilikuwa kipindi cha amani, ufanisi, na furaha. Katika kipindi ambacho Sulemani alitegemeza ibada ya kweli kwa uaminifu-mshikamanifu, Yehova alibariki sana taifa hilo. Kwa Mfalme Sulemani, Mungu alimpa utajiri mwingi sana na pia “moyo wa hekima na wa akili” ili Sulemani atawale katika uadilifu na upendo. (1 Wafalme 3:12) Biblia yasema hivi: “Wafalme wote wa duniani wakamtafuta Sulemani uso wake, ili waisikie hekima yake, Mungu aliyomtia moyoni.”—2 Mambo ya Nyakati 9:23.

Yehova aliwapa watu usalama, amani, na wingi wa vitu vizuri. Neno la Mungu lasema hivi: “Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi.” Kihalisi na kitamathali, watu “wakakaa salama, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, . . . siku zote za Sulemani.”—1 Wafalme 4:20, 25.

Nyakati zimebadilika. Maisha leo ni tofauti sana na siku hizo za furaha za zamani za kale. Tofauti na wakati wa Sulemani, umaskini ni tatizo kuu leo. Hata katika mataifa yenye utajiri, kuna umaskini. Kwa kielelezo, katika Marekani na vilevile Jumuiya ya Ulaya, karibu asilimia 15 ya watu huishi kwa umaskini, lasema shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo.

Kuhusu hali ya ulimwenguni pote, The State of the World’s Children 1994, ambayo ni ripoti ya UNICEF (Hazina ya Watoto ya Umoja wa Mataifa), ilisema kwamba mtu mmoja kati ya watu watano wa wakazi wote ulimwenguni huishi kwa umaskini kabisa, ikiongeza kwamba maisha ya wengi walio maskini ulimwenguni “yanazidi kuwa magumu sana na yenye kutamausha.”

Katika nchi fulani, infleshoni yenye kuongezeka sana inaongezea taabu za maskini. Mwanamke mmoja katika nchi moja ya Afrika alisema hivi: “Unaona kitu sokoni, kisha unasema, ‘Sawa, acha niende nyumbani nichukue pesa nikinunue.’ Unarudi saa moja baadaye unaambiwa kwamba huwezi kukinunua kwa sababu kwa muda mfupi tu bei imepandishwa. Sasa, mtu atafanyaje? Inafadhaisha sana.”

Mwanamke mwingine huko alisema hivi: ‘Ili tuweze kuishi sisi husahau juu ya mahitaji mengine. Namna ya kupata chakula ndilo jambo la kushughulikia.’

Kulingana na Umoja wa Mataifa, wakati ujao hauna tumaini. Kwa kielelezo, UNICEF, inakadiria kwamba idadi ya watu ikiendelea kukua kwa jinsi inavyoendelea, idadi ya maskini ulimwenguni pote itaongezeka mara nne “katika muda wa maisha ya mtu.”

Hata hivyo, ijapokuwa hali za kiuchumi na kijamii zinazozidi kuharibika, watumishi wa Mungu wana sababu ya kuhisi ifaavyo. Ingawa wanaishi miongoni mwa wale waonao wakati ujao kwa maoni yazidiyo kuwa mabaya, watumishi wa Mungu wanatazama wakati ujao kwa shangwe na uhakika. Makala ifuatayo itachanganua sababu kwa nini.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

De Grunne/Sipa Press

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki