Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 12/15 kur. 24-25
  • “Mimi Ni Mwenye Thamani kwa Yehova!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mimi Ni Mwenye Thamani kwa Yehova!”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2005
  • Yehova Anakuthamini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Wewe ni Mwenye Thamani Machoni pa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 12/15 kur. 24-25

“Mimi Ni Mwenye Thamani kwa Yehova!”

KATIKA “nyakati [hizi] zilizo ngumu kushughulika nazo,” watumishi waaminifu wengi wa Yehova huvumilia pigano la daima dhidi ya hisia za kutokufaa kitu. (2 Timotheo 3:1, NW) Hili halishangazi, kwa kuwa mojapo “matendo ya ujanja” ya Shetani ni kutufanya tuhisi kwamba hatupendwi, hata na Muumba wetu! (Waefeso 6:11, NW, kielezi-chini) Kwa kufaa, toleo la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1995, lilikuwa na makala mbili kwa ajili ya funzo la kutaniko zenye kichwa “Wewe Ni Mwenye Thamani Machoni pa Mungu!” na “Kuchochea Kwenye Upendo na Kazi Zilizo Bora—Jinsi Gani?” Makala hizo zilikusudiwa kutukumbusha kwamba Yehova huthamini jitihada zetu. Yafuatayo ni baadhi ya maelezo ya shukrani yaliyopokewa:

“Katika miaka yangu 27 nikiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova gazeti halijapata kamwe kuniathiri sana jinsi hii. Sikuweza kujizuia ila kulia machozi—makala hizi zilinituliza sana. Sasa nahisi kuwa napendwa sana na Yehova. Ni kana kwamba mzigo mkubwa sana wenye kulemea umeondolewa kutoka begani pangu.”—C. H.

“Nilisoma gazeti hili mara nne kwa siku moja. Nilifurahia njia ambayo makala hiyo ilisema kwamba wewe ulifundishwa uwongo ikiwa waamini kwamba hufai kitu. Nitatumia makala hii kwa ziara za uchungaji na kuhubiri nyumba kwa nyumba.”—M. P.

“Shetani amefaulu sana kufanya hata wale wampendao Yehova wahisi kuwa hawafai kitu na hawapendeki. Kukumbushwa na jamii ya ‘mtumwa mwaminifu’ kwamba Yehova hutupenda sana na kwamba yeye huthamini yale mambo yote madogo-madogo tunayomfanyia ni mojapo mambo yenye kutia moyo zaidi ambayo nimepata kusoma. Kwa miaka mingi nimekuwa na hisia mlizosema juu yazo katika makala hizi. Sikuhisi kamwe nastahili upendo wa Yehova, kwa hiyo nilijaribu kufanya mengi zaidi na zaidi katika utumishi wake ikiwa njia ya kustahili upendo huo. Lakini nilichochewa na hisia ya hatia na kuona aibu. Kwa hiyo haidhuru ni muda wa saa ngapi niliotumia katika huduma, au ni watu wangapi niliowasaidia, nilihisi hayo hayakutosha. Niliona upungufu wangu tu. Sasa ninapomtumikia Yehova kwa sababu ya upendo, nawazia kwamba yeye anatabasamu na kwamba ananionea fahari. Hilo lafanya upendo wangu kwake ufurike hata zaidi na lanifanya nitake kufanya zaidi. Sasa nina shangwe nyingi sana kutokana na utumishi wangu kwa Yehova.”—R. M.

“Kwa kweli hizi ni makala bora zaidi, zenye kujenga zaidi, ndiyo, zenye kutokeza zaidi ili kugusa mioyo yetu ambazo nimepata kusoma wakati wowote! Nimekuwa nikisoma Mnara wa Mlinzi kwa miaka 55, na kumekuwa na matoleo mengi yenye kutokeza. Lakini toleo hili lapita lolote lile ambalo tumekuwa nalo wakati wowote kuondosha shaka, wasiwasi, na hofu zetu kwamba sisi ‘hatufai kitu’ na ‘hatupendwi’ na hatuwezi kamwe kufanya vya kutosha ili ‘kustahili’ upendo wa Yehova. Mnara wa Mlinzi hili lina aina ya msaada wa kiroho ambayo ndugu zetu wahitaji sana. Ni azimio langu kutumia makala hizi mara kwa mara ninapofanya uchungaji.”—F. K.

“Kwa wale kati yetu wanaoshindana na hali ya kutojistahi, au hata na hisia za kujikirihi, laweza kuwa jambo gumu sana kukusanya nguvu zetu ili tuendelee katika kweli. Makala hii ilionyesha huruma nyingi na uelewevu mwingi, ilikuwa kama kupakwa marhamu yenye kutuliza, inayoponyesha, moja kwa moja moyoni. Inafariji kama nini kusoma maneno hayo katika Mnara wa Mlinzi na kujua bila shaka kwamba Yehova huelewa kwelikweli! Asanteni kwa kutukumbusha kwamba Yehova huwa hajaribu kuchochea watu wake kupitia hisia za hatia, aibu, au hofu. Hata ingawa sehemu ninayochangia kazi ya kuhubiri imepunguka sana kwa sababu ya taabu za kifedha na matatizo ya afya katika familia yetu, ningali napata uradhi katika kile ambacho naweza kufanya. Naona kwamba nina furaha zaidi katika utumishi ninapojaribu kuacha upendo uwe kani ya kunichochea.”—D. M.

“Nimetoka tu kumaliza kusoma [makala] ‘Wewe Ni Mwenye Thamani Machoni pa Mungu!’ Kila fungu lilileta machozi machoni pangu. Nilitoka familia ambayo haikuonyesha upendo sana. Nilishushwa, nikachokozwa, na kuchekwa. Kwa hiyo, mapema maishani nilihisi sifai kitu. Mimi bado huwa na hisia zenye kina sana kutokana na malezi yangu ambazo hunikandamiza ninapopatwa na msiba. Nilipoacha kutumikia nikiwa mzee wa kutaniko, nilihisi, kama ilivyo kawaida, kuwa mwenye kushindwa—kwa Mungu, familia yangu, na ndugu zangu kutanikoni. Hisia hizo haziondoki haraka, lakini makala hii ya wakati ufaao imenisaidia kupata tena kadiri fulani ya usawaziko. Imefanya mtazamo wangu uwe mwangavu.”—D. L.

“Asanteni kwa makala ‘Wewe Ni Mwenye Thamani Machoni pa Mungu!’ Mimi hukabiliana na hali ya kujichukia sana na hisia zenye kina za kutofaa kitu, ambazo hutokana na kutendewa vibaya utotoni. Yafaa kabisa kuona kufikiri huku kulikopotoka kuwa tendo la ujanja la Shetani mwenyewe. Kwaweza hata kuvunja tamaa ya mtu ya kuishi. Kwa kweli ni lazima nijitahidi kila siku kukinza ule uwongo wa kwamba mimi sipendeki. Makala hii ina maana zaidi kwangu kuliko vile mwezavyo kujua.”—C. F.

“Leo akina ndugu huitikia hasa wazo la kwamba Yehova huthamini matendo yanayochochewa na upendo kuliko yale yanayotokana na kulazimishwa au kuwekewa mkazo. Ufikirio juu ya utu wa Yehova wenye uchangamfu na shauku, kupendezwa kwake na watu wake wakiwa mmoja-mmoja, na njia yenye upendo ambayo yeye hujitoa mwenyewe ni wenye kuburudisha na wenye kuchochea. Kwa sababu hiyo, mara tulipopokea makala ‘Wewe Ni Mwenye Thamani Machoni pa Mungu!’ wengi walionyesha shukrani. Yaonekana kana kwamba yawafungulia wengi njia ya kusitawisha uhusiano wa kibinafsi zaidi na Yehova. Mke wangu nami twataka kuonyesha shukrani kwa namna ya kuandika na ufikirio ambao umeonyeshwa katika magazeti ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi. Tunajitahidi kutumia mengi ya mambo haya tunapoyazuru makutaniko.”—Kutoka kwa mwangalizi asafiriye.

“Nimekuwa msomaji mwaminifu kwa karibu miaka 30, lakini sijapata kamwe kusoma jambo lolote lenye kuchochea sana, na lenye kujenga sana jinsi hii. Maandiko yenye nguvu, yaliyotumiwa kwa ustadi yamenisaidia ning’oe ule uwongo mbalimbali uliojificha katika hisia zangu mwenyewe, hilo likiniruhusu nimkaribie Yehova zaidi. Kwa miaka mingi nilimtumikia Yehova kwa sababu ya kuwa na hisia ya hatia. Nilikuwa na uelewevu wa kiakili tu kuhusu fidia na upendo wa Mungu. Asanteni kwa makala hizo zenye ufahamu wenye kina na zenye ufikirio. Natumaini kusoma nyingi zaidi kama hizo.”—M. S.

“Katika miaka yangu yote 29 ya kuwa katika kweli, siwezi kukumbuka wakati makala iliponifanya niwe na itikio la jinsi hii la kuwa mwenye shukrani na hisiamoyo yenye kina. Ingawa nililelewa kwa upendo mwingi na familia yenye kujali, sijapata kamwe kuhisi nastahili kuwa hai, licha ya kustahili kumtumikia Yehova. Baada ya kusoma makala hii, nilipiga magoti, na nikilia kwi kwi kwi sana nilimshukuru Yehova. Nitathamini sana makala hii milele. Nitajiona kwa njia tofauti kwa sababu sasa nina uelewevu wa kwamba mimi ni mwenye thamani kwa Yehova.”—D. B.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki