Hutataka Kuukosa!
KUKOSA nini? “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova unaokaribia upesi! Katika sehemu nyingi mkusanyiko utaanza saa 3:30 Ijumaa Asubuhi kwa programu ya muziki. Baada ya kusikiliza mahoji yenye kujenga imani katika ile sehemu “Kusikia Kutoka kwa Wapiga-Mbiu wa Amani Wenye Bidii,” utafurahia hotuba yenye kutia moyo “Mungu Anataka Tufanye Nini?”
Jambo kuu alasiri ya Ijumaa litakuwa hotuba ya msingi yenye kuchochea hisia “Fungu Letu Tukiwa Wajumbe wa Amani ya Kimungu.” Kisha ile sehemu “Kusaidia Wengine Wajifunze Matakwa ya Mungu” itatoa madokezo juu ya kuwafundisha wapya. Hiyo itafuatwa na mfululizo wa wakati ufaao “Jihadharini na Mitego Iliyofichwa ya Vitumbuizo.” Programu ya Ijumaa itamalizika kwa hotuba “Mpinge Ibilisi—Usivumilie Ushindani” na “Kutegemeza Uaminifu wa Neno la Mungu kwa Uaminifu-Mshikamanifu.”
Programu ya Jumamosi asubuhi itakazia umuhimu wa kufanya wanafunzi katika mfululizo wenye sehemu tatu “Wajumbe Wanaoleta Habari Njema ya Amani.” Kipindi hicho kitamalizika kwa zile hotuba “Upaji Mchangamfu Ndani ya Tengenezo la Yehova” na “Uhai na Amani Kupitia Wakfu na Ubatizo,” na baadaye kutakuwa na fursa kwa wanafunzi wapya kubatizwa.
Utoaji wa Jumamosi alasiri “Fikiria Mawazo ya Yehova Juu Ya Mambo” utajibu maswali kama vile ‘Je, Wakristo wanashiriki katika kazi ya kutenganisha leo?’ na ‘Maoni ya Biblia ni nini juu ya adhabu ya kifo?’ Pia utafurahia ule mfululizo wenye sehemu mbili unaochangamsha moyo “Mungu wa Amani Hukujali Wewe” na hasa hotuba ya kumalizia “Fuatia Amani ya Kimungu Katika Maisha ya Familia.”
Programu ya Jumapili asubuhi itatia ndani ule mfululizo wenye sehemu tatu “Kuwatambua Wajumbe wa Aina Inayofaa” na hotuba “Sikiliza na Utii Neno la Mungu.” Programu ya asubuhi itamalizika kwa drama ya mavazi kamili ya drama ambayo itatokeza masomo muhimu kutoka kwa simulizi la Biblia la Mwamuzi Gideoni.
Kipindi cha mwisho cha mkusanyiko Jumapili alasiri kitakuwa na hotuba ya watu wote, yenye kichwa “Amani ya Kweli Hatimaye!—Kutoka Chanzo Gani?” Hatimaye, hotuba yenye kuchochea “Kusonga Mbele Tukiwa Wajumbe wa Amani ya Kimungu” itamalizia mkusanyiko.
Fanya mipango sasa ili ushiriki. Ili kujua mahali pa mkusanyiko karibu zaidi na nyumbani kwako, pata habari katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la kwenu au uwaandikie watangazaji wa gazeti hili. Toleo la Juni 8 la Amkeni! litaorodhesha mahali pa mikusanyiko yote katika Afrika Mashariki na Rwanda.