Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 5/22 uku. 32
  • Je, Utakuwapo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Utakuwapo?
  • Amkeni!—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Hutataka Kuukosa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Hungependa Kuukosa!
    Amkeni!—2000
  • Je, Uko Tayari Kuhudhuria?
    Amkeni!—2005
  • Njooni Kwenye “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 5/22 uku. 32

Je, Utakuwapo?

Katika mwaka uliopita, zaidi ya watu 8,700,000 kotekote ulimwenguni walihudhuria “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova. Je, utakuwapo katika mmoja wa “Wajumbe wa Amani ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya? Wakaribishwa kwa uchangamfu uhudhurie.

Mahali pengi, mkusanyiko utaanza 3:30 Ijumaa asubuhi kwa programu ya muziki. Kipindi cha kufungua kitakazia hotuba yenye kutia moyo “Mungu Anataka Tufanye Nini?” Hii itatia ndani habari tuwezayo kutumia kusaidia mamilioni ya wengine yafanye kile ambacho Mungu anataka.

Utoaji wa alasiri “Kusaidia Wengine Wajifunze Matakwa ya Mungu” utatayarisha wakusanyikaji kushiriki kwa matokeo zaidi katika kazi ya kufanya wanafunzi. Baadaye, mfululizo wenye sehemu mbili “Jihadharini na Mitego Iliyofichwa ya Vitumbuizo” utaonya juu ya mitego ya roho waovu tupaswayo kuepuka. Programu ya Ijumaa itamalizika kwa hotuba ya maana “Kutegemeza Uaminifu wa Neno la Mungu kwa Uaminifu-Mshikamanifu.”

Kipindi cha Jumamosi asubuhi kitakazia umuhimu wa kazi ya kufanya wanafunzi kikiwa na mfululizo wenye sehemu tatu “Wajumbe Wanaoleta Habari Njema ya Amani.” Hotuba ya mwisho ya kipindi hicho itakuwa juu ya wakfu na ubatizo, kisha ubatizo wa wanafunzi wapya utafuata.

Utoaji wa Jumamosi alasiri “Fikiria Mawazo ya Yehova Juu Ya Mambo” utajibu maswali ambayo wengi wamekuwa nayo juu ya vichwa vya habari za karibuni zaidi. Utafurahia mfululizo wenye sehemu mbili wenye kuchangamsha moyo “Mungu wa Amani Hukujali Wewe.” Kisha kitu fulani cha kipekee kitafurahiwa wakati wa hotuba ya kumalizia kipindi hicho “Fuatia Amani ya Kimungu Katika Maisha ya Familia.”

Mfululizo wenye sehemu tatu wa Jumapili asubuhi, “Kuwatambua Wajumbe wa Aina Inayofaa,” utakazia kichwa cha mkusanyiko kwa kuvuta uangalifu juu ya vielelezo vya manabii wa Biblia. Programu ya asubuhi itamalizika kwa drama yenye mavazi kamili ambayo itatoa masomo yenye thamani kutoka kwa simulizi la Biblia la Mwamuzi Gideoni.—Waamuzi 6:11–8:28.

Kipindi cha mwisho cha mkusanyiko Jumapili alasiri, kitakazia hotuba ya watu wote yenye kichwa “Amani ya Kweli Hatimaye!—Kutoka Chanzo Gani?” Mwishowe, hotuba yenye kuhamasisha “Kusonga Mbele Tukiwa Wajumbe wa Amani ya Kimungu” itamalizia mkusanyiko.

Kwa kuwa mikusanyiko 22 imepangiwa Afrika Mashariki na Rwanda pekee, yamkini kutakuwa na mmoja utakaofanywa karibu na mahali unapoishi. Hakikisha na Mashahidi wa Yehova wa mahali penu ili upate habari juu ya wakati na mahali pa mkusanyiko ulioko karibu nawe. Toleo la Amkeni! la Juni 8, pia litaorodhesha mahali pa mikusanyiko katika Afrika Mashariki.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki