Njooni Kwenye “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya!
MAMILIONI wengi watakuwapo kwenye mamia ya mahali ulimwenguni kote. Katika Marekani peke yake, mikusanyiko 193 imeratibiwa. Mkusanyiko wa kwanza utakuwa Mei 23-25 na wa mwisho, Septemba 12-14. Yamkini mmojawapo wa mikusanyiko hiyo ya siku tatu—kuanzia Ijumaa hadi Jumapili—utakuwa katika jiji ambalo haliko mbali na nyumbani kwako.
Utanufaika kutokana na wingi wa maagizo ya Biblia yenye kutumika. Katika sehemu zilizo nyingi programu itaanza saa 3:30 kila asubuhi kwa muziki. Programu ya Ijumaa yakazia mahojiano ya dakika 25 pamoja na watu ambao maisha yao yameathiriwa sana na imani yao katika Neno la Mungu. Kipindi cha kwanza kitamalizika kwa hotuba ya msingi “Kutembea kwa Imani, Si kwa Kuona.”
Hotuba ya kwanza Ijumaa alasiri itazungumzia sehemu muhimu waliyo nayo vijana katika kutaniko la Kikristo. Mfululizo wenye sehemu tatu unaofuata wazungumzia viwango vya Biblia kama vinavyohusiana na mwenendo wa Mkristo katika usemi, adabu, na sura ya kibinafsi. Kisha hotuba “Jihadharini na Ukosefu wa Imani” na “Neno la Mungu Liko Hai” zakazia onyo la upole katika Waebrania sura ya 3 na ya 4. Programu ya Ijumaa itamalizika kwa hotuba “Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.”
Hotuba ya kwanza Jumamosi asubuhi ni “Imani Bila Kuwa na Kazi Imekufa.” Hotuba nyingine ya maana asubuhi hiyo, “Pateni Kutia Mizizi na Kuimarishwa Katika Kweli,” yafafanua jinsi ukuzi wa kiroho uwezavyo kutimizwa. Hicho kipindi kitamalizika kwa sehemu ya kawaida ya mkusanyiko, “Imani Katika Neno la Mungu Huongoza Kwenye Ubatizo,” na baadaye kutakuwa uandalizi kwa wanafunzi wapya kubatizwa.
Hotuba ya ufunguzi Jumamosi alasiri, “Fanya Pigano Kali kwa Ajili ya Imani” yazungumzia onyo la upole la kitabu cha Biblia cha Yuda. Mfululizo wa muda wa saa nzima wenye kichwa “Na Twende Nyumbani kwa Yehova” utazungumzia manufaa za mikutano ya Kikristo. Programu siku hiyo yamalizika kwa hotuba “Ubora wa Imani Yako—Watahiniwa Sasa.”
Programu ya Jumapili asubuhi yavuta uangalifu kwenye mfululizo wenye sehemu tatu utakaozungumzia kitabu cha Biblia cha Yoeli, kutia ndani utumizi wacho kwa siku yetu. Kisha yafuata drama ya Biblia yenye kichwa “Weka Jicho Lako Likiwa Sahili.” Jambo kuu la mkusanyiko ni hotuba ya watu wote ya alasiri, “Imani na Wakati Ujao Wako.”
Kwa hakika utatajirishwa kiroho kwa kuwapo. Utakaribishwa kwa moyo mweupe kwenye kila pindi. Fanya mipango sasa uhudhurie. Kwa habari ya mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi na nyumbani kwako, pata habari katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la kwenu au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili.