Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 6/15 uku. 3
  • Je, Waweza kwa Kweli Kumpenda Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Waweza kwa Kweli Kumpenda Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwenda Pamoja na Mungu wa Kweli
  • Wewe Unampenda Yehova kwa Shauku?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Iweni na Upendo Mwororo kwa Mtu na Mwenzake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kumpenda Mungu Humaanisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 6/15 uku. 3

Je, Waweza kwa Kweli Kumpenda Mungu?

“MWANADAMU hataniona akaishi,” asema Mungu. (Kutoka 33:20) Hata zaidi, tangu nyakati za Biblia hakujawa na uthibitisho wa binadamu yeyote kuwasiliana naye moja kwa moja. Je, yaonekana kuwa vigumu—hata jambo lisilowezekana—kukuza shauku yenye kina na mtu ambaye hujapata kamwe kumwona au kumsikia moja kwa moja? Je, kwa kweli yawezekana kuwa na uhusiano wenye upendo pamoja na Muumba wa ulimwengu wote mzima?

Hakupaswi kuwa na shaka lolote kwamba yawezekana kukuza shauku changamfu ya kibinafsi na Mungu. Kwenye Kumbukumbu la Torati 6:5, twasoma kwamba taifa la Israeli liliamuriwa hivi: “Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.” Baadaye Yesu Kristo aliithibitisha tena sheria hiyo kwa wafuasi wake, akaongeza hivi: “Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.” (Mathayo 22:37, 38) Je, Biblia ingetuhimiza tumpende Mungu ikiwa uhusiano kama huo hauwezi kupatikana?

Lakini, je, Yehova hututarajia tumpende kwa kuwa tu yeye huamuru hivyo? La. Mungu aliwaumba wenzi wawili wa kibinadamu wa kwanza wakiwa na uwezo wa kumpenda. Adamu na Hawa hawakulazimishwa kuingia katika uhusiano wenye upendo pamoja na Muumba wao. Badala ya hivyo, Mungu aliwaweka katika hali bora ambamo wangekuza shauku yenye kina naye. Chaguo lilikuwa lao—wamkaribie Mungu au wajiondoe kutoka kwake.

Adamu na Hawa walichagua kuasi. (Mwanzo 2:16, 17; 3:6, 7) Hata hivyo, wazao wao wangekuwa na uwezekano wa kukuza uhusiano wenye upendo pamoja na Muumba.

Kwenda Pamoja na Mungu wa Kweli

Kwa kielelezo, katika Biblia, Abrahamu anasemwa kuwa “rafiki” ya Mungu. (Yakobo 2:23) Lakini Abrahamu hakuwa kwa vyovyote mtu pekee aliyefurahia uhusiano wa karibu pamoja na Mungu. Biblia husema juu ya wanadamu wengine wengi wasio wakamilifu walioonyesha shauku ya kutoka moyoni kuelekea Yehova na ‘waliokwenda pamoja na Mungu.’—Mwanzo 5:24; 6:9; Ayubu 29:4; Zaburi 25:14; Mithali 3:32.

Watumishi wa Mungu wa kale hawakuzaliwa wakiwa na upendo na shauku na Mungu. Walihitaji kuzikuza. Jinsi gani? Kwa kupata kumjua kwa jina lake la kibinafsi, Yehova. (Kutoka 3:13-15; 6:2, 3) Kwa kufahamu kuwako kwake na Uungu wake. (Waebrania 11:6) Kwa kutafakari kwa ukawaida juu ya matendo yake ya upendo. (Zaburi 63:6) Kwa kueleza hisia zao za ndani kabisa katika sala kwa Mungu. (Zaburi 39:12) Kwa kujifunza juu ya wema wake. (Zekaria 9:17) Kwa kukuza hofu ifaayo ili wasimchukize.—Mithali 16:6.

Je, wewe waweza kuwa rafiki ya Mungu na kwenda pamoja naye? Ni kweli kwamba, huwezi kumwona Mungu wala kusikia sauti yake. Hata hivyo, Yehova hukualika ‘ukae katika hema yake,’ uwe rafiki yake. (Zaburi 15:1-5) Hivyo, yawezekana kwako kumpenda Mungu. Lakini waweza kukuzaje uhusiano wa karibu na wenye shauku pamoja naye?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki