Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 6/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongozwa na Roho ya Mungu Katika Karne ya Kwanza na Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Roho Yenyewe Hutoa Ushahidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Tembea kwa Roho na Uishi Kulingana na Wakfu Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 6/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, twaweza kusema kwamba watumishi wa Mungu leo walio na tumaini la kidunia wana kiasi kilekile cha roho ya Mungu kama walicho nacho Wakristo watiwa-mafuta kwa roho?

Swali hili si jipya. Habari ii hii ilishughulikiwa katika “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1952 (la Kiingereza). Wengi wamekuwa Mashahidi tangu wakati huo, kwa hiyo twaweza kulifikiria hilo swali tena na wakati uleule kupitia yaliyosemwa katika habari hiyo ya awali.

Kimsingi, jibu ni, ndiyo, ndugu na dada waaminifu wa jamii ya kondoo wengine waweza kushiriki kwa kadiri ileile na watiwa-mafuta katika kupokea roho takatifu ya Mungu.—Yohana 10:16.

Bila shaka, hilo halimaanishi kwamba hiyo roho hutenda kazi katika njia ileile juu ya watu wote mmoja-mmoja. Kumbuka watumishi waaminifu katika nyakati za kabla ya Ukristo, ambao bila shaka walipokea roho ya Mungu. Wakiwa na nguvu kutokana na hiyo roho, baadhi yao walichinja wanyama wakali, wakaponya wagonjwa, hata wakafufua wafu. Nao walihitaji hiyo roho ili kuandika vitabu vilivyopuliziwa vya Biblia. (Waamuzi 13:24, 25; 14:5, 6; 1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:17-37; 5:1-14) Hilo Mnara wa Mlinzi lilisema: “Ingawa hawakuwa wa jamii ya watiwa-mafuta, walijazwa roho takatifu.”

Kwa upande mwingine, wafikirie wanaume na wanawake katika karne ya kwanza waliotiwa mafuta kwa roho, na kuwa wana wa kiroho wa Mungu wenye tumaini la kimbingu. Wote walikuwa wametiwa mafuta, lakini hilo halimaanishi kwamba baada ya hilo, hiyo roho ilitenda kazi kwa njia ileile juu yao wote. Hilo ni wazi kutokana na 1 Wakorintho sura ya 12. Hapo mtume Paulo alizungumzia zawadi za roho. Twasoma hivi katika mistari 8, 9, na 11: “Mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja. . . . lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.”

Kwa umaana, huko nyuma si watiwa-mafuta wote waliokuwa na zawadi za roho za kimuujiza. Katika 1 Wakorintho sura ya 14, Paulo alitaja mkutano wa kutaniko ambamo mmoja alikuwa na zawadi ya lugha, lakini miongoni mwa wote waliokuwapo, hakuna aliyekuwa na zawadi ya kutafsiri. Hata hivyo, mapema kidogo, kila mmoja wao alikuwa ametiwa mafuta kwa roho. Je, ingefaa kusema kwamba ndugu aliye na zawadi ya lugha alikuwa na roho zaidi kuliko wengine waliokuwapo? La. Wale watiwa-mafuta wengine hawakuwa na upungufu, kana kwamba hawakuweza kuielewa Biblia vizuri kama huyo au hawakuweza kukabili majaribu kwa kadiri ileile. Roho ilitenda kazi kwa njia ya pekee juu ya yule ndugu aliyeweza kusema kwa lugha. Licha ya hayo, yeye na wao walihitaji kubaki karibu na Yehova na ‘kujazwa roho,’ kama Paulo alivyoandika.—Waefeso 5:18.

Kuhusu wale wa mabaki leo, bila shaka wamepokea roho ya Mungu. Wakati mmoja ilitenda kazi juu yao kwa njia ya pekee—walipotiwa mafuta na kuasilishwa kuwa wana wa kiroho. Baadaye wao ‘hujazwa roho,’ wakiwa na msaada wayo wajitahidipo kuifahamu Biblia kwa wazi zaidi, waongozapo katika kazi ya kuhubiri, au kukabili majaribu—ya kibinafsi au ya kitengenezo.

Washiriki wa “kondoo wengine,” ingawa hawajapata kutiwa mafuta, wao hupokea roho takatifu katika njia nyinginezo. Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1952 (la kiingereza), lilionelea hivi:

“‘Kondoo wengine’ leo hufanya kazi ya kuhubiri ileile sawa na watiwa-mafuta, chini ya hali zilizo ngumu zilezile, nao huonyesha uaminifu na uaminifu-mshikamanifu uleule. Wao hujilisha kwenye meza ileile ya kiroho, wakila chakula kilekile, wakijifunza kweli zilezile. Wakiwa wa jamii ya kidunia, wenye matumaini ya kidunia na upendezi mkubwa wa mambo ya kidunia, huenda wakijifurahisha zaidi na maandiko yahusianayo na hali za kidunia katika ulimwengu mpya; hali mabaki ya watiwa-mafuta, wenye matumaini ya kimbingu na upendezi wa kibinafsi wenye nguvu katika mambo ya roho, huenda wakajifunza kwa bidii zaidi mambo hayo katika neno la Mungu. . . . Hata hivyo mambo ya hakika yabaki kwamba kweli zilezile na uelewevu uleule unapatikana kwa jamii zote mbili, na ufahamu wa mambo ya kimbingu na ya kidunia wapatao hutegemea tu kadiri ambavyo watu mmoja-mmoja hujifunza. Kiasi kilekile cha roho ya Bwana hupatikana kwa kiasi kilekile kwa jamii zote mbili, na kiasi kilekile cha ujuzi na uelewevu hupatikana kwa jamii zote mbili, kukiwa na fursa zilezile za kujifunza.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki