Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 12/1 uku. 9
  • Kuchukua Msimamo Imara Shuleni Kwathawabishwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuchukua Msimamo Imara Shuleni Kwathawabishwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Chanzo cha Halloween Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Ukweli Kuhusu Halloween
    Amkeni!—2013
  • Ukweli Kuhusu Sherehe Zinazopendwa
    Amkeni!—2001
  • “Hatutaki Kusherehekea ‘Halloween!’”
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 12/1 uku. 9

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

Kuchukua Msimamo Imara Shuleni Kwathawabishwa

BIBLIA hutabiri hivi: “Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.” (Isaya 54:13) Kwa njia iliyopanuliwa, maneno “watoto wako wote” yaweza kutumiwa kuhusu jamii nzima ya watumishi wa Mungu duniani, kutia ndani na wachanga sana. Leo, wazazi Wakristo huhakikisha kwamba watoto wao ‘wanafundishwa na Yehova’ nyumbani na kwenye mikutano ya Kikristo.

Hata hivyo, Wakristo vijana wanapoenda shuleni wanakabiliwa na miito ya ushindani iliyo migumu. Mara nyingi wanapata kwamba ni lazima wachukue msimamo wenye nguvu kwa kutegemea yale ambayo wamejifunza kutoka katika Biblia. Wafanyapo hivyo, matokeo yaweza kunufaisha wanafunzi na walimu vilevile, kama ionyeshwavyo na jambo lililoonwa lifuatalo kutoka Micronesia.

Katika Tol kisiwa kidogo cha magharibi mwa Pasifiki katika visiwa vya Chuuk, walimu katika shule ya huko waliwaambia watoto wote wajitayarishe na kushiriki katika mwadhimisho wa Halowini wa shule. Wanafunzi Mashahidi waling’amua kwamba huo mwadhimisho ungeweza kuhusisha mapambo na mavazi ya kufananisha mizuka, mazimwi, na wachawi—zote zinazohusiana na tamaduni za uwasiliani-roho. Watoto hao wasingeweza kushiriki wakiwa na dhamiri nzuri.a

Kutokana na mazoezi yao yenye kutegemea Biblia, ya nyumbani na kwenye kutaniko la Kikristo, walijua kuwa mazoea hayo hayampendezi Mungu, hata yafanywapo kwa ajili ya vitumbuizo tu. Ili kusaidia kueleza msimamo wao wazi zaidi, hao watoto walimwalika Barak, mmoja wa wamishonari Mashahidi kwenye hicho kisiwa, aseme na walimu wao.

Baada ya kusikia maelezo, hao walimu walipangia mkutano wa pili, ambamo Barak angeweza kusema na wafanyakazi wote wa shule. Kwenye mkutano huo, Barak alitoa mambo ya hakika ili kuonyesha asili ya kweli ya Halowini. Alipata habari yake kutoka kwenye vichapo kadhaa vya Watch Tower na vilevile kutoka vyanzo vingine. Walimu na wasimamizi walishangazwa na yale waliyojifunza juu ya chanzo, historia, na asili ya kidini ya huo mwadhimisho. Waliamua kufanya mkutano wa wafanyakazi ili kuamua jinsi ya kusuluhisha hali hiyo.

Siku chache baadaye, uamuzi usiotazamiwa ulitangazwa. Matayarisho yote kwa ajili ya Halowini yalikuwa yakifutiliwa mbali. Hiyo shule isingeadhimisha Halowini kwa vyovyote mwaka huo. Ni tokeo lenye kupendeza kama nini lililotokana na azimio la kufanya lililo sawa shuleni la Mashahidi hao vijana! Vijana hawapaswi kamwe kuogopa au kuaibika kuchukua msimamo imara kwa ajili ya kweli ya Biblia.

Ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova huwafundisha watoto wao wajifunze kwa bidii shuleni. Pia Mashahidi vijana wanazoezwa kuishi kupatana na kanuni za Biblia na kushiriki tumaini lao na itikadi zao pamoja na wanafunzi wengine kadiri wanavyokuwa na fursa. Hata matokeo yasipokuwa yenye kupendeza au ya mara moja kama yalivyokuwa katika kisa hiki, vijana waweza kuwa na uhakika na uradhi unaotokana na kufanya lililo sawa. Na la maana zaidi, wao waweza kuwa na uhakika kwamba Baba yao wa kimbingu anapendezwa naye atawabariki kwa sababu ya utii wao mwaminifu.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi juu ya Halowini na vyanzo vyayo vya uwasiliani-roho, ona toleo la Amkeni! la Novemba 22, 1993, lililochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki