Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 2/1 kur. 3-4
  • Uhuru wa Kidini Wamaanisha Nini Kwako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uhuru wa Kidini Wamaanisha Nini Kwako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Namna Gani Uhuru wa Kidini?
  • Uhuru wa Kidini wa Aina Nyingine
  • Usikose Kusudi la Uhuru wa Kupewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Watu Huru Lakini Wanaotakwa Watoe Hesabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Mtumikie Yehova, Mungu wa Uhuru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Karibuni Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 2/1 kur. 3-4

Uhuru wa Kidini Wamaanisha Nini Kwako?

Ingawa uhuru wa dini huonwa kuwa haki ya msingi Marekani, msukosuko wa ujeuri wa vikundi vya wafanya-ghasia dhidi ya Mashahidi wa Yehova ulienea nchini humo katika miaka ya 1940

MAMILIONI ya watu wameupigania. Watu fulani hata wameufia. Kwa kweli huo ni mojawapo ya mali za wanadamu zenye thamani zaidi. Huo ni nini? Ni uhuru! Kichapo The World Book Encyclopedia chafasili uhuru kuwa “uwezo wa kufanya machaguo na kuyafikiliza.” Chaendelea hivi: “Kulingana na maoni ya kisheria, watu wako huru ikiwa jamii haiwawekei mipaka yoyote yenye kudhulumu, isiyohitajiwa, au isiyo na kiasi. Lazima jamii pia ihami haki zao—yaani, uhuru wao mbalimbali, uwezo wao mbalimbali wa kutenda, na mapendeleo yao ya msingi.”

Hiyo dhana yasikika kuwa sahili. Hata hivyo kwa kweli, yaonekana kuwa karibu haiwezekani kwa watu kuafikiana juu ya ni wapi barabara mipaka ya uhuru yapasa kuwekwa. Kwa kielelezo, watu fulani huamini kwamba serikali yapaswa kuweka sheria ili kuhami uhuru wa raia wayo. Lakini wengine watajadili kwamba sheria hizo ndizo vizuizi hasa ambavyo raia wapaswa kuwekwa huru navyo! Kwa wazi, uhuru humaanisha mambo tofauti kwa watu tofauti.

Namna Gani Uhuru wa Kidini?

Labda ule uhuru unaoshindaniwa zaidi sana ni uhuru wa dini, ambao umefasiliwa kuwa “haki ya mtu ya kuamini na kuzoea imani anayochagua.” Kulingana na Azimio la Ulimwengu Wote la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa, “kila mtu ana haki ya uhuru wa wazo, dhamiri na dini.” Hilo latia ndani haki ya mtu ya “kubadili dini au itikadi yake,” pamoja na uhuru wa “kudhihirisha dini au itikadi yake katika mafundisho, zoea, ibada, na desturi.”—Makala 18.

Kwa hakika, twatazamia taifa lolote linalojali raia walo kikweli liwape uhuru wa aina hiyo. Kwa kuhuzunisha, hilo halitendeki sikuzote. “Dini huathiri hisia za ndani kabisa za watu wengi,” chaeleza The World Book Encyclopedia. “Serikali fulani zina uhusiano wa karibu na dini moja na huona watu wa dini nyingine kuwa tisho kwa mamlaka ya kisiasa. Pia huenda serikali ikaona dini kuwa hatari kisiasa kwa sababu huenda dini zikaweka uaminifu kwa Mungu juu ya utii kwa serikali.”

Kwa sababu hizo serikali fulani huweka vizuizi dhidi ya njia za kuabudu za dini. Serikali chache hukataza kabisa kuzoezwa kwa imani yoyote. Nyingine, ingawa zinadai kuunga mkono uhuru wa ibada, hizo hudhibiti sana utendaji wote wa kidini.

Kwa kielelezo, fikiria hali iliyodumu kwa miaka mingi Mexico. Ingawa Katiba ilihakikisha uhuru wa kidini, iliweka masharti haya: “Makanisa yanayotumiwa kwa ibada ya umma ni mali ya Taifa, liwakilishwalo na Serikali ya Muungano, ambalo litaamua ni yapi yawezayo kuendelea kutumiwa hivyo.” Mwaka wa 1991 Katiba ilifanyiwa mabadiliko ili kukomesha kizuizi hicho. Hata hivyo, kielelezo hicho chaonyesha kwamba uhuru wa kidini waweza kufasiriwa tofauti katika nchi mbalimbali.

Uhuru wa Kidini wa Aina Nyingine

Je, nchi unamoishi ina uhuru wa kidini? Ikiwa ndivyo, huo unafasiliwaje? Je, wewe waweza kumwabudu Mungu kwa njia unayochagua, au unashurutishwa kuwa mshiriki wa dini ya Serikali? Je, unaruhusiwa kusoma na kugawanya fasihi za kidini, au habari hiyo iliyochapwa imekatazwa na serikali? Je, waweza kuzungumza na wengine kuhusu imani yako, au hilo huonwa kuwa kuingilia haki zao za kidini?

Majibu ya maswali hayo yanategemea unakoishi. Hata hivyo kwa kupendeza, kuna aina ya uhuru wa kidini ambayo haitegemei mahali hususa hata kidogo. Alipokuwa Yerusalemu mwaka wa 32 W.K., Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Ikiwa nyinyi mwakaa katika neno langu, nyinyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mtajua kweli, na kweli itawaweka nyinyi huru.”—Yohana 8:31, 32.

Yesu alimaanisha nini kwa taarifa hiyo? Wasikilizaji wake Wayahudi walitamani kuwekwa huru na utawala wa Kiroma. Lakini Yesu hakuwa akizungumza kuhusu kuwekwa huru na uonevu wa kisiasa. Badala ya hivyo, alikuwa akiahidi wanafunzi wake jambo bora zaidi, kama tutakavyoona katika makala ifuatayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki