Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 5/1 kur. 30-31
  • Karibuni Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Karibuni Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Usikose Kusudi la Uhuru wa Kupewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Mtumikie Yehova, Mungu wa Uhuru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kukusanyika Pamoja na Wapendao Uhuru wa Kupewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Watu Huru Lakini Wanaotakwa Watoe Hesabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 5/1 kur. 30-31

Karibuni Kwenye “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya!

UHURU! Neno hilo lasikika lenye kupendeza kama nini! Hakuna mtu yeyote anayeonea shangwe kuwa katika ufungwa au utekwa. Miaka ya hivi karibuni imekuwa yenye maendeleo mengi katika uhuru wa kisiasa unaotamaniwa sana, kupita mingineyo yote inayoweza kukumbukwa.

Hata hivyo, ingawa uhuru wa kisiasa unatamaniwa sana, kuna uhuru ambao ni wa maana na wenye kutamaniwa zaidi. Ni uhuru ule ambao Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, alisema juu wayo kwa wanafunzi wake: “Mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:31, 32) Huo ni uhuru kutoka katika imani bandia za kidini, uhuru kutoka katika hofu ya wanadamu, uhuru kutoka katika utumwa wa uzoevu mbalimbali wa dhambi, na mwingine mwingi zaidi.

Ni uhuru huo ambao ndio kichwa cha “Wapendao Uhuru” Mikusanyiko ya Wilaya ambayo itafanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kuanzia kiangazi cha 1991. Tangu mwaka wa 1919, uliotiwa alama kwa kuondolewa kwa vizuizi vya kiserikali juu ya wale waliokuwa wakiongoza miongoni mwao, watu wa Mungu wamekuwa wakionea shangwe uhuru wenye kuongezeka kwa habari ya ibada yao safi.

Ni jambo lenye kufaa sana kwamba, habari ya uhuru imekaziwa muda wa miaka iliyopita kwenye mikusanyiko ya kitheokrasi, na vichwa kama “‘Taifa Huru’ Kusanyiko la Kitheokrasi” na “‘Wana wa Mungu wa Uhuru’ Makusanyiko ya Wilaya.” Uhuru unazungumzwa kwa upana pia katika vichapo kama “The Truth Shall Make You Free” [Kweli Itawaweka Huru] na Uzima wa Milele—Katika Uhuru wa Wana wa Mungu.

Ule uhuru wenye kutolewa na Mungu wa watumishi wa Yehova si kwa ajili ya hali njema na raha yao wenyewe tu. Ni kama vile tunavyosoma kwenye Wagalatia 5:13: “Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.” “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko wa Wilaya utatusaidia tuthamini kusudi la uhuru wetu, utatuwezesha kuushikilia uhuru wetu wenye thamani kubwa, na utatuonyesha jinsi ya kuutumia kwa njia inayofaa kabisa.

Mkusanyiko utaanza Ijumaa saa 4:20 asubuhi kwa programu ya muziki ambayo itatupa hali ya akili inayofaa kwa kile chakula cha kiroho kitakachofuatia. Kichwa cha siku ya kwanza ni “Kujua Kweli Ambayo Hutuweka Huru,” chenye msingi wa Yohana 8:32. Mambo makuu ya pindi kabla ya adhuhuri yatakuwa maneno ya ukaribishaji wa mwenyekiti na hotuba ya msingi, “Kusudi na Utumizi wa Uhuru Wetu Wenye Kutolewa na Mungu.” Hotuba hiyo itakazia tofauti kati ya uhuru wa Mungu ulio kamili na uhuru wa kiasi kinachohusu ambao Yehova hutupa sisi. Itatutia moyo pia kuutumia uhuru tulio nao kwa njia iliyo bora zaidi. Programu ya alasiri itashughulikia sehemu mbalimbali za uhuru wetu na huduma yetu na kumalizia kwa drama, Kuwekwa Huru Ili Kuendeleza Ibada ya Kweli.

Kichwa cha siku ya pili ni “Kusimama Imara Katika Uhuru Wetu Wenye Kutolewa na Mungu,” chenye msingi wa Waga-latia 5:1. Jambo kuu katika programu ya asubuhi litakuwa mfululizo wa hotuba utakaoonyesha jinsi washirika mmoja mmoja wa familia wanavyoweza kuonea shangwe uhuru katika familia. Wale ambao watakuwa tayari kubatizwa watathamini hasa maneno kuhusu jinsi ambavyo uhuru unapatikana kwa wakfu na ubatizo. Yenye kuhusishwa pia katika programu ya alasiri, ni mazungumzo ya kuvutia juu ya kama ndoa ndiyo au siyo ufunguo wa kupata furaha. Kutakuwa pia na mfululizo wa hotuba juu ya sehemu tofauti za uhuru halafu hotuba ya kumalizia itakayokazia Wakili Mkuu wa Mungu wa kuandaa uhuru na uhai wa milele.

Jumapili ina kichwa “Kutumia Uhuru Wetu Kupatana na Roho ya Mungu,” chenye msingi wa 2 Wakorintho 3:17. Mambo makuu ya programu hiyo yatakuwa mfululizo wa hotuba wenye kupendeza sana juu ya mfano wa Yesu uliorekodiwa kwenye Mathayo 13:47-50, unaofunua jinsi Mashahidi wa Yehova hutumikia wakiwa wavuvi wa watu. Hotuba ya watu wote alasiri ni “Kupokea kwa Shangwe Ulimwengu Mpya wa Mungu wa Uhuru!” Itafuatwa na jambo jipya la kutokeza kwa mkusanyiko wa wilaya: muhtasari wa somo la Mnara wa Mlinzi wa juma hilo. Na programu itamalizika na himizo la Kimaandiko kwa sisi sote kuzidi kuendelea katika kutumia vizuri uhuru wetu wenye kutolewa na Mungu katika mwenendo wetu na katika kutoa kwetu ushuhuda.

Kwa wapendao uhuru wote, tunasema katika maneno ya mtunga zaburi Daudi hivi: “Onjeni mwone ya kuwa BWANA [Yehova, NW] yu mwema.” (Zaburi 34:8) Jaribu uwezavyo kabisa kufika kwenye mkusanyiko huo. Ifanye iwe shughuli yako kuwapo kutoka kipindi cha kufungua Ijumaa asubuhi hadi hotuba ya kumalizia Jumapili alasiri. Ukija na hamu yenye afya ya kiroho, ukiwa na ufahamu kamili wa uhitaji wako wa kiroho, utakuwa mwenye furaha kweli kweli! (Mathayo 5:3) Na tusisahau kanuni hii, “Apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.” Hiyo pia inatumika kwa jinsi tunavyoweka bidii katika kutayarisha kimbele ili kuhudhuria, jinsi tunavyoweka bidii-nyendelevu katika kusikiliza programu kwa kadiri inavyotolewa, na kwa jinsi tunavyotimiza kwa shauku mapendeleo yoyote ya utumishi wa hiari yaliyo wazi kwetu kuhusiana na “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko wa Wilaya wetu.—2 Wakorintho 9:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki