Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 2/15 uku. 29
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Utaokolewa Mungu Atendapo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • “Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Waokolewa Wakiwa Hai Kupitia Dhiki Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 2/15 uku. 29

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

“Mnara wa Mlinzi” la Agosti 15, 1996, lilisema hivi: “Katika sehemu ya mwisho ya dhiki, ‘mwili’ ambao umekimbilia upande wa Yehova utaokolewa.” Je, hilo ladokeza kwamba baada ya sehemu ya kwanza ya dhiki kubwa, wapya wengi watakuja kwenye upande wa Mungu?

Hiyo haikuwa hoja iliyokuwa inatokezwa.

Maneno ya Yesu yanayopatikana kwenye Mathayo 24:22 yatatimizwa wakati ujao kwa msingi, kwa kuokoka kwa njia fulani sehemu ya kwanza ya dhiki kubwa inayokuja, shambulio dhidi ya dini. Hiyo makala ilisema hivi: “Kumbuka kwamba ‘mwili,’ wa mabaki ya watiwa-mafuta na pia wa ‘umati mkubwa,’ utakuwa tayari umeokolewa wakati Babiloni Mkubwa utakapoangamia upesi na kikamili katika sehemu ya kwanza ya dhiki.”

Waaminifu hao hawatakuwa katika hatari yoyote Yesu na jeshi lake la kimbingu watendapo katika sehemu ya mwisho ya ile dhiki. Lakini ni nani watakaookoka sehemu hiyo ya dhiki? Ufunuo 7:9, 14 huonyesha kwamba umati mkubwa wenye tumaini la kidunia utaokoka. Namna gani Wakristo watiwa-mafuta kwa roho? Makala “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1990, ilizungumzia sababu ya kutoweza kwetu kushikilia kauli juu ya wakati ambapo baki la watiwa-mafuta litachukuliwa kwenda mbinguni. Kwa hiyo makala ya majuzi (Agosti 15, 1996) iliacha habari hiyo bila kutaja mambo dhahiri, ikitoa elezo hili la ujumla: “Vilevile katika sehemu ya mwisho ya dhiki, ‘mwili’ ambao umekimbilia upande wa Yehova utaokolewa.”

Kuhusu ikiwa wapya wowote wataweza kujifunza kweli na kuja kwenye upande wa Mungu baada ya dhiki kubwa kuanza, ona maneno ya Yesu yaliyorekodiwa kwenye Mathayo 24:29-31. Baada ya kuanza kwa dhiki, ishara ya Mwana wa binadamu itatokea. Yesu alisema kwamba makabila yote ya dunia yatajipiga na kuomboleza. Hakusema lolote juu ya watu kutambua hali iliyopo, kutubu, kuchukua msimamo wao kwenye upande wa Mungu, na kuwa wanafunzi wa kweli.

Vivyo hivyo, katika mfano wa kondoo na mbuzi, Mwana wa binadamu atokea na kutenganisha watu kihukumu kwa msingi wa yale waliyokuwa wamefanya au yale ambayo hawakuwa wamefanya wakati uliopita. Yesu hakusema lolote juu ya watu walioonyesha kwa muda mrefu sifa za kuwa wenye mfano wa mbuzi wakibadilika mara moja na kuwa kama kondoo. Anakuja kuhukumu kwa msingi wa yale ambayo watu tayari walikuwa wamethibitika kuwa.—Mathayo 25:31-46.

Lakini, pia, hakuna sababu yoyote ya kushikilia kauli katika hoja hii. Watu wa Mungu, watiwa-mafuta na pia umati mkubwa, wanajua wanalopaswa kufanya sasa—kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20; Marko 13:10) Huu ni wakati wetu wa kukumbuka na kutenda kulingana na himizo hili: “Tukiwa tunafanya kazi pamoja naye, twawasihi sana nyinyi pia msiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi layo. Kwa maana yeye asema: ‘Wakati wenye kukubalika nilikusikia, na siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.”—2 Wakorintho 6:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki