Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 3/1 uku. 29
  • “Mojawapo Tu ya Maisha Nyingi Ulizoathiri”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mojawapo Tu ya Maisha Nyingi Ulizoathiri”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Wakili Awachunguza Mashahidi wa Yehova
    Amkeni!—2010
  • Kulea Familia Ulimwenguni Pote Kulea Katika Upendo, Nidhamu, Mfano, na Kanuni za Kiroho
    Amkeni!—1992
  • Mungu Hujibu Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Vijana—Imarisheni Tamaa Yenu ya Kumtumikia Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 3/1 uku. 29

“Mojawapo Tu ya Maisha Nyingi Ulizoathiri”

HUKO nyuma katika Januari 1996, Carol alikuwa na uvimbe wa ubongo. Alikuwa katika miaka yake ya 60 na hadi wakati huo alikuwa amekuwa sikuzote mwanamke mwenye furaha, mwenye afya na mwenye neno la kutia moyo kwa kila mtu. Lakini sasa madaktari walikuwa wakijitahidi kushinda huo uvimbe wenye kufisha. Katika kujitahidi kwake, Carol alipokea barua ifuatayo:

“Carol Mpendwa:

“Nasikitika sana juu ya afya yako mbaya. Kwa uzuri, tuna tumaini halisi ambalo Biblia hutusaidia kujua na kupenda. Tumaini hilo ni kwa Ufalme wa Yehova kutawala dunia ili tuweze kuishi katika hali za paradiso, wakati ambao sisi sote twatazamia.

“Nataka ujue kwamba kazi yako binafsi ya kuhubiri iliokoa watu wengi kutoka katika kifo kidumucho milele. Mimi ni mmojawapo wa watu hao. Sina uhakika kama wakumbuka mara ya kwanza tulipokutana. Wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 20. Nilikuwa na nywele ndefu, nilikuwa nikiuza dawa za kulevya, na nilikuwa nikishirikiana na kikundi cha wafanya-jeuri. Sote tulibeba bunduki na hatukuwa wenye upendo kwa yeyote isipokuwa kwetu wenyewe.

“Ulibisha mlango wangu pamoja na Shahidi mwingine na kunitolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Nilijaribu kukupatia dola moja na kusema kwamba sikutaka hayo magazeti. Ulinijulisha ya kwamba hamkuwa mkihubiri ili tu kupata upaji. Uliniambia kwamba mlikuwa mkifanya kazi ya kusaidia watu kuisoma Biblia. Sina uhakika kama niliyachukua hayo magazeti au kuyasoma. Hata hivyo, ulipanda mbegu ya kweli katika maisha yangu.

“Miaka kadhaa baadaye Shahidi mwingine, Gary, alikuja nyumbani kwa mama yangu nikiwapo. Nilimwambia juu ya ziara uliyokuwa umefanya miaka kadhaa iliyopita. Gary alijifunza Biblia pamoja nami kwa muda mrefu hadi nilipobatizwa hatimaye katika mwaka wa 1984. Sasa nawafunza watoto wangu kweli juu ya Ufalme wa Mungu.

“Nina uhakika kwamba mimi ni mojawapo tu ya maisha nyingi ulizoathiri katika miaka yako ya utumishi mwaminifu. Hata hivyo, kupitia fadhili-upendo huo, umeniwezesha mimi na familia yangu kuja kumjua Mungu Mkuu, Yehova, na Mwanaye Kristo Yesu. Natazamia siku nitakapoweza kukuona katika mfumo mpya wa mambo wakati Yehova atakapofuta kabisa kila chozi kutoka macho yetu, na kifo hakitakuwapo tena.—Ufunuo 21:4.

“Kwa habari yangu na ya familia yangu, tu wenye furaha kwamba tulipata nafasi ya kukujua na ya kuwa sehemu ya kazi yako ya kutoa ushahidi. Asante.

“Kwa upendo wa kidugu,

Peter”

Baada ya kuwa mgonjwa kwa miezi sita, Carol alikufa katika Machi 1996, akiwa amepanda mbegu nyingi za kweli katika mwendo wa miaka yake 35 akiwa mweneza-evanjeli mwenye bidii. Alijifunza kwamba mtu hajui kamwe wakati mbegu itakapozaa matunda, hata miaka mingi baadaye.—Mathayo 13:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki