Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 4/1 uku. 26
  • Kueneza Mbegu za Ufalme Kila Pindi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kueneza Mbegu za Ufalme Kila Pindi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • “Mmebadili Maoni Yangu Juu ya Mashahidi wa Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Nilikuwa Mwanasiasa Lakini Sasa Mimi Ni Mkristo
    Amkeni!—2002
  • Nilikuwa Mhalifu
    Amkeni!—1996
  • Je, Magereza Yanaendeleza Uhalifu?
    Amkeni!—2001
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 4/1 uku. 26

Wapiga-Mbiu wa Ufalme Waripoti

Kueneza Mbegu za Ufalme Kila Pindi

NENO la Mungu, Biblia, hutia moyo kufanya kazi kwa bidii. Mfalme Solomoni alisema hivi: “Asubuhi panda mbegu zako, wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa, kama ni hii au hii, au kama zote zitafaa sawasawa.”—Mhubiri 11:6.

Katika kila pindi ifaayo, Mashahidi wa Yehova hupanda “mbegu” kwa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Katika nchi na vikundi vya visiwa zaidi ya 230, wanaendelea “bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Matendo 5:42) Mambo yaliyoonwa yafuatayo yatoa kielezi juu ya jinsi ambavyo Mashahidi wa Yehova ‘hawazuii mikono yao’ katika kazi ya kuhubiri.

◻ Katika Jamhuri ya Cape Verde, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuwa akitembea karibu na gereza akiwa katika huduma ya shambani. Katika ua la gereza, wafungwa kadhaa walikuwa wamepanda juu ya mti. Walipomwona huyo Shahidi huko chini, hao wafungwa walipaaza sauti wakiomba wapewe magazeti. Huyo Shahidi alifungilia magazeti kadha ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwenye jiwe na kuyarusha juu ya ukuta wa gereza hadi upande ule mwingine. Likiwa tokeo la upendezi huo wa kwanza, mafunzo 12 ya Biblia yalianzishwa. Watatu kati ya hao wafungwa wamejiweka wakfu kwa Mungu na kujitoa kwa ubatizo wa maji. Mmojawapo wa hao wafungwa amekuwa akitumikia akiwa mweneza-evanjeli wa wakati wote, au painia, kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa. Lakini, wao hufanyaje utendaji mbalimbali wa utumishi wao wa shambani wakiwa gerezani? Kwanza gereza hugawanywa katika maeneo. Kisha eneo hilo hugawiwa hao Mashahidi watatu nalo huhubiriwa kutoka seli hadi seli. Hao wapiga-mbiu wa Ufalme hufuatia upendezi katika njia ileile Mashahidi wa Yehova hufanya ulimwenguni pote—kwa kufanya ziara za kurudia. Hata hivyo tofauti moja, ni ukawaida ambao mafunzo ya Biblia huongozwa. Badala ya kujifunza Biblia kwa muda wa saa moja au zaidi mara moja au mbili kwa juma, wafungwa wengine hujifunza kila siku! Kwa kuongezea, Mashahidi wamepewa ruhusa na mkurugenzi mkuu wa hilo gereza kuongoza mikutano yote ya kutaniko humo gerezani.

◻ Mwanamke mmoja katika Ureno alirithi vichapo kadhaa vya Watch Tower nyanya yake alipokufa. Kwa kuwa hakuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, hakuwa na upendezi wa kuhifadhi vitabu hivyo. Hata hivyo, hakutaka kuviharibu. Siku moja alimwambia mmoja wa Mashahidi wa Yehova aliyemtembelea akiwa katika kazi ya kuhubiri nyumba hadi nyumba, juu ya hiyo maktaba. Huyo Shahidi alimwuliza kama alijua thamani halisi ya hiyo maktaba. Huyo mwanamke alijibu hivi: “Kwa hakika, sijui thamani yake halisi, lakini nawezaje kupata kujua?” Huyo mwanamke alikubali funzo la Biblia, na upesi akaja kuthamini maktaba ya nyanya. Sasa yeye pia ni Shahidi wa Yehova aliyebatizwa. Isitoshe, binti yake na rafiki wa karibu wa hiyo familia wanajifunza Biblia. Mkusanyo huo wa vitabu ulithibitika kuwa urithi wenye thamani kama nini!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki