Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 6/1 kur. 5-6
  • Siri—Katika Jina la Bwana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siri—Katika Jina la Bwana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hatari za Siri za Kidini
  • Mbona hizo Siri Zote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2018
  • Siri Ambayo Wakristo Hawathubutu Kuweka!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Siri Unayoweza Kuwaambia Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 6/1 kur. 5-6

Siri—Katika Jina la Bwana

MACHI 1995 shambulio la gesi yenye sumu katika njia ya chini kwa chini ya Tokyo, Japani, iliua watu 12, ikafanya maelfu zaidi ya watu kuwa wagonjwa, na ikasaidia kufunua siri fulani. Farakano la kidini lijulikanalo kuwa Aum Shinrikyo (Kweli Kuu Kuliko Zote) lilikuwa limejenga ghala la gesi ya sarin, ili kuitumia katika kufuatia makusudi yenye kushangaza.

Mwezi mmoja baadaye mlipuko wa bomu ulivunja vipande-vipande jengo la serikali katika Oklahoma City, Marekani, na kuua watu 167. Uthibitisho ulionekana kuonyesha kwamba kwa njia fulani hilo shambulio lilihusiana na ule mgogoro kati ya serikali na madhehebu ya dini ya Branch Davidian katika Waco, Texas, miaka miwili kamili mapema. Wakati huo washiriki wapatao 80 wa madhehebu hiyo walikufa. Huo mlipuko wa bomu ulifunua pia jambo lililokuwa siri kwa watu wengi: Sosaiti nyingi za wanamgambo wa kijeshi sasa zinatenda katika Marekani, ambazo angalau baadhi yazo zashukiwa kupanga kwa siri utendaji dhidi ya serikali.

Baadaye, mwaka wa 1995 ulipokaribia kwisha, miili iliyochomwa ya watu 16 ilipatikana msituni karibu na Grenoble, Ufaransa. Walikuwa washiriki wa Jumuiya Ifuatayo Kanuni za Kidini ya Solar Temple, madhehebu ndogo ambayo katika Oktoba 1994 ilikuwa katika habari huko Uswisi na Kanada wakati ambapo 53 kati ya washiriki wayo ama walijiua ama waliuawa kimakusudi. Lakini hata baada ya jambo hilo la huzuni kubwa, farakano hilo liliendelea kufanya kazi. Hata leo nia na makusudio yalo yangali sirini.

Hatari za Siri za Kidini

Kwa sababu ya matukio hayo, je, yashangaza kwamba watu wengi hushuku sosaiti za kidini? Bila shaka hakuna mtu angetaka kutegemeza shirika la siri—la kidini au lisilo la kidini—ambalo latumia vibaya itibari yake na humfanya afuatie makusudio asiyokubaliana nayo. Hata hivyo, watu wanaweza kufanya nini ili kuepuka kutumbukia katika mtego wa kuhusika na sosaiti za siri zenye kushukiwa?

Kwa wazi, lingekuwa jambo la hekima kwa yeyote anayefikiria kwa uangalifu kuwa mshiriki wa sosaiti ya siri kuhakikisha makusudio halisi yayo. Wapaswa kujikinga na msongo kutoka kwa marafiki au wajuani, na maamuzi yapaswa kutegemea mambo ya hakika wala si hisia. Kumbuka kwamba, yamkini ni mtu mwenyewe—wala si wengine—atakayepatwa na matokeo yoyote yawezayo kupatikana.

Kufuata kanuni za Biblia ndiko njia hakika kabisa ya kuepuka sosaiti hatari ambazo nia yazo si nzuri. (Isaya 30:21) Hilo hutia ndani kudumisha kutokuwamo kwa kisiasa, kuwapenda wengine, hata maadui, kuepuka “kazi za mwili,” na kukuza matunda ya roho ya Mungu. Zaidi ya yote, ni lazima Wakristo wa kweli wasiwe sehemu ya ulimwengu, kama vile Yesu alivyokuwa si sehemu ya ulimwengu, na mwendo huo utawazuia kushiriki katika sosaiti za siri za kilimwengu.—Wagalatia 5:19-23; Yohana 17:14, 16; 18:36; Waroma 12:17-21; Yakobo 4:4.

Mashahidi wa Yehova ni wanafunzi wa Biblia wenye bidii wanaoichukua imani yao kwa uzito na ambao hujaribu waziwazi kuishi kupatana nayo. Wanajulikana ulimwenguni pote kuwa sosaiti ya kidini ‘itafutayo sana amani na kuifuatia.’ (1 Petro 3:11) Kitabu chao Jehovah’s Witnesses—Proclaimers of God’s Kingdom chasema hivi kwa usahihi: “Mashahidi wa Yehova si sosaiti ya siri katika maana yoyote. Imani zao zenye msingi wa Biblia huelezwa kikamili katika vichapo vinavyopatikana kwa yeyote. Kwa kuongezea, wao hutia jitihada ya pekee kualika umma uhudhurie mikutano yao wajionee na kusikia wao wenyewe lile litukialo.”

Dini ya kweli haina mazoea ya kisiri hata kidogo. Waabudu wa Mungu wa kweli wameagizwa wasifiche utambulisho wao au kufanya kusudi lao wakiwa Mashahidi wa Yehova lisiwe dhahiri. Wanafunzi wa mapema wa Yesu walijaza Yerusalemu kwa mafundisho yao. Itikadi na utendaji wao zilikuwa za peupe. Ndivyo ilivyo kwa habari ya Mashahidi wa Yehova leo. Kwa kueleweka, serikali za kimabavu zizuiapo kimakosa uhuru wa ibada, Wakristo wapaswa kuendelea na utendaji wao kwa hadhari na wakiwa na moyo-mkuu, wakimtii “Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu,” hali inayolazimishwa juu yao kwa sababu ya kutoa kwao ushahidi wa hadharani kwa moyo mkuu.—Matendo 5:27-29; 8:1; 12:1-14; Mathayo 10:16, 26, 27.

Ikiwa umepata kuwaza kwamba huenda Mashahidi wa Yehova wakawa ni madhehebu au farakano la siri, yamkini hilo lilikuwa kwa sababu ulijua machache mno juu yao. Hali lazima ilikuwa hivyo kwa walio wengi katika karne ya kwanza.

Matendo sura ya 28 hutuambia juu ya mkutano ambao mtume Paulo alifanya Roma pamoja na “watu walio wakubwa wa Wayahudi.” Walimwambia hivi: “Twafikiri yafaa kusikia kutoka kwako fikira zako ni nini, kwa maana kweli kwa habari ya farakano hili yajulikana kwetu kwamba kila mahali huwa lasemwa vibaya.” (Matendo 28:16-22) Kwa kuitikia, Paulo ‘aliwaeleza hilo jambo kwa kutoa ushahidi kamili kuhusiana na ufalme wa Mungu,’ na “wengine wakaanza kuamini.” (Matendo 28:23, 24) Bila shaka ilikuwa ni kwa manufaa yao ya kudumu kupata mambo hakika kuhusu Ukristo wa kweli.

Wakiwa wamejitoa wakfu kwa ajili ya utumishi wa peupe na wa hadharani kwa Mungu, Mashahidi wa Yehova watafurahi kufunua mambo ya hakika yaliyo wazi juu ya utendaji na itikadi zao kwa mtu yeyote yule anayetaka kujua mambo ya hakika. Kwa nini usijichunguzie mwenyewe, ili uweze kupata habari kikamili kuhusu imani yao?

[Picha katika ukurasa wa 6]

Mashahidi wa Yehova wanafurahi kufunua wao ni akina nani na wanafanya nini

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki