Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 8/1 kur. 3-4
  • Dhamiri—Mzigo Wenye Kulemea au Manufaa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dhamiri—Mzigo Wenye Kulemea au Manufaa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Dhamiri—Maoni ya Biblia
  • Sauti ya Dhamiri Iliyomo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Je, Dhamiri Yako Imezoezwa Vizuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kuendelea Kuwa na Dhamiri Njema
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Dhamiri Njema Mbele za Mungu
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 8/1 kur. 3-4

Dhamiri—Mzigo Wenye Kulemea au Manufaa?

‘DHAMIRI yangu inanisumbua!’ Mara kwa mara, karibu sisi sote hupatwa na maumivu makali ya dhamiri. Huenda hisia hizo zikasambaa kutoka wasiwasi wa kawaida hadi maumivu makali. Dhamiri yenye kusumbuka yaweza hata kuanzisha mshuko-moyo au hali ya kuhisi kushindwa kabisa.

Basi, kwa maoni hayo, je, dhamiri si mzigo wenye kulemea? Huenda wengine wakahisi kwamba ndivyo ilivyo. Kihistoria, tamaduni nyingi ziliifikiria dhamiri kuwa uwezo wa kiasili. Wengi walihisi kwamba ilikuwa mwongozo wa kiadili uliotolewa moja kwa moja na Mungu. Hivyo dhamiri imeitwa “kuwapo kwa Mungu katika mwanadamu,” “asili yetu ya awali,” na hata imeitwa “sauti ya Mungu.”

Hata hivyo, katika miaka ya juzi, limekuwa jambo lenye kupendwa na wengi kusisitiza kwamba dhamiri hasa ni uwezo wa kujipatia—tokeo la uvutano wa wazazi na jamii. Kwa kielelezo, wanasaikolojia fulani hutoa hoja kwamba mtoto hujifunza kuepukana na tabia isiyofaa hasa kwa sababu ya hofu ya kuadhibiwa, wakiamini kwamba kile ambacho sisi hukiita dhamiri tunakipata tu kutokana na kanuni na itikadi za wazazi wetu. Wengine huelekeza kwenye fungu ambalo jamii kwa ujumla hutekeleza katika kupitisha kanuni na viwango. Wengine huyaona maumivu makali ya dhamiri kuwa tu hitilafiano kati ya yale ambayo sisi hupenda kuyafanya na yale ambayo jamii yenye uonevu hutudai tuyafanye!

Licha ya hizo nadharia juu ya dhamiri, mara nyingi watu wamesimama imara kinyume cha wazazi, familia, na jamii nzima-nzima kwa sababu dhamiri zao ziliwaambia wafanye hivyo. Watu fulani hata wamekuwa tayari kudhabihu maisha yao kwa ajili ya dhamiri! Na licha ya tofauti kubwa kati ya tamaduni mbalimbali za ulimwengu, matendo kama uuaji wa kimakusudi, wizi, uzinzi, uwongo, na ngono ya maharimu huonekana kuwa makosa karibu ulimwenguni pote. Je, hilo halitoi uthibitisho kwamba dhamiri ni ya kiasili?

Dhamiri—Maoni ya Biblia

Aliye na mamlaka kikweli juu ya habari hiyo ni Yehova Mungu. Kwa vyovyote, “[Mungu] ndiye aliyetuumba.” (Zaburi 100:3) Yeye anaelewa maumbile yetu kikamili. Neno la Mungu, Biblia, hueleza kwamba mwanadamu aliumbwa kwa “mfano” wa Mungu. (Mwanzo 1:26) Mwanadamu aliumbwa akiwa na hisi za yaliyo sawa na yasiyo sawa; tangu mwanzo, dhamiri ilikuwa ni sehemu ya asili ya hali ya mwanadamu.—Linganisha Mwanzo 2:16, 17.

Mtume Paulo athibitisha hili katika barua yake kwa Waroma, anapoandika hivi: “Wakati wowote ule watu wa mataifa wasio na sheria [ya Mungu] wafanyapo kwa asili mambo ya sheria, watu hawa, ijapokuwa hawana sheria, wao ni sheria kwao wenyewe. Wao ndio walewale waonyeshao kiini cha sheria kuwa imeandikwa katika mioyo yao, huku dhamiri yao ikitoa ushahidi pamoja nao na, kati ya fikira zao wenyewe, wanashtakiwa au hata wanatetewa.” (Waroma 2:14, 15) Ona kwamba watu wengi ambao hawakuwa wamelelewa chini ya Sheria ya kimungu waliyopewa Wayahudi bado walifuata kanuni fulani za sheria ya Mungu, si kwa kusongwa na jamii, bali “kwa asili”!

Basi, dhamiri si mzigo wenye kulemea hata kidogo, bali ni zawadi, manufaa. Ni kweli, inaweza kutuletea msononeko. Lakini tunapoitii ifaavyo, yaweza kututhawabisha kwa hisia za uradhi wenye kina na amani ya ndani. Yaweza kutuongoza, kutulinda, na kutuchochea. Kichapo The Interpreter’s Bible chaeleza hivi: “Afya ya kiakili na kihisia-moyo yaweza kuhifadhiwa tu mtu anapojaribu kupatanisha yale anayofanya na yale ambayo anahisi yampasa kuyafanya.” Mtu anaweza kupatanisha hayo jinsi gani? Yawezekana kufanyiza na kuizoeza dhamiri yetu? Maswali hayo yatafikiriwa katika makala ifuatayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki