Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 8/15 kur. 4-7
  • Wokovu—Inachomaanisha kwa Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wokovu—Inachomaanisha kwa Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wokovu—Wapatikana Katika Dini Zote?
  • Ujuzi Sahihi juu ya Yesu Ni wa Maana kwa Wokovu
  • Ujuzi Sahihi juu ya Mungu Ni Muhimu Pia
  • Kwa Roho na Kweli
  • Imani Huchochea Matendo
  • Kile Ambacho Wokovu Waweza Kumaanisha Kwako
  • Dumisha ‘Tumaini Lako la Wokovu’!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Wokovu Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • “Mwamini Yesu”—Je, Kumwamini Yesu Kunatosha Kupata Wokovu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jambo Ambalo Ni Lazima Tufanye Ili Tuokolewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 8/15 kur. 4-7

Wokovu—Inachomaanisha kwa Kweli

‘WEWE umeokoka?’ Mara nyingi, wanaouliza swali hili huhisi kwamba wameokoka kwa sababu ‘wamemkubali Yesu kuwa Mwokozi wao binafsi.’ Hata hivyo wengine huhisi kwamba kuna njia mbalimbali za kufikia wokovu na maadamu ‘Yesu yumo ndani ya moyo wako,’ haidhuru kile unachoamini au hata wewe ni wa kanisa gani.

Biblia husema kwamba ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wa namna zote waokolewe.” (1 Timotheo 2:3, 4) Hivyo wokovu unapatikana kwa wote watakaoukubali. Lakini yamaanisha nini kuokolewa? Je, kwa kweli ni jambo linalotukia kwako tu kwa kufanya bidii kidogo au bila kufanya bidii yoyote?

Neno “wokovu” lamaanisha “kukombolewa katika hatari au uharibifu.” Hivyo ni kweli wokovu wahusisha zaidi ya hali tulivu ya akilini. Wamaanisha kuokolewa katika uharibifu wa huu mfumo wa mambo wa sasa ulio mwovu na hatimaye katika kifo chenyewe! Lakini ni nani ambaye Mungu atamwokoa? Kwa kujibu, acheni tuchunguze yale aliyofunza Yesu Kristo juu ya habari hii. Huenda matokeo ya uchunguzi wetu yakakushangaza.

Wokovu—Wapatikana Katika Dini Zote?

Pindi moja, Yesu alikuwa na mazungumzo na mwanamke Msamaria. Ijapokuwa hakuwa Myahudi, aliamini kwa usahihi kabisa kwamba Mesiya angekuja “aitwaye Kristo.” (Yohana 4:25) Je, itikadi hiyo ilitosha ili aweze kuokolewa? La, kwa maana Yesu alimwambia huyo mwanamke kwa ujasiri hivi: “Nyinyi mwaabudu kile msichojua.” Yesu alijua kwamba ikiwa mwanamke huyo angepata wokovu, angepaswa kurekebisha njia yake ya kuabudu. Kwa hiyo Yesu alieleza hivi: “Hata hivyo, saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati waabudu wa kweli watakapomwabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta wa namna hiyo wamwabudu yeye.”—Yohana 4:22, 23.

Pindi nyingine ambayo Yesu alifunua maoni yake juu ya wokovu ilihusisha Mafarisayo, farakano mashuhuri la Dini ya Kiyahudi. Mafarisayo walikuwa wamefanyiza mfumo wa ibada na waliamini kwamba ulikuwa na kibali cha Mungu. Lakini sikiliza maneno ya Yesu kwa hao Mafarisayo: “Nyinyi wanafiki! Isaya alisema kweli alipotabiri hivi juu yenu: ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wao huniabudu bure; mafundisho yao yakiwa tu sheria zilizofundishwa na wanadamu.’”—Mathayo 15:7-9, New International Version.

Lakini vipi juu ya vikundi vya kidini leo vinavyodai kumwamini Kristo? Je, Yesu angevikubali vyote kuwa njia halali za kupata wokovu? Kwa habari hiyo hatuhitaji kukisia, kwa maana Yesu alisema hivi: “Si kila mtu anayeniambia, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika ufalme wa mbingu, bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye katika mbingu ataingia. Wengi wataniambia katika siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii katika jina lako, na kufukuza roho waovu katika jina lako, na kufanya kazi nyingi zenye nguvu katika jina lako?’ Na bado ndipo hakika nitaungama kwao: Sikuwajua nyinyi kamwe! Ondokeni kwangu, nyinyi wafanyakazi wa uasi-sheria.”—Mathayo 7:21-23.

Ujuzi Sahihi juu ya Yesu Ni wa Maana kwa Wokovu

Maneno haya ya Yesu yana maana yenye kufanya mtu afikiri. Yaonyesha kwamba watu wengi walio wachaji wanashindwa ‘kufanya mapenzi ya Baba.’ Basi, mtu aweza kupataje wokovu wa kweli? Kitabu cha 1 Timotheo 2:3, 4 chajibu hivi: “Mapenzi [ya Mungu] ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.”—Linganisha Wakolosai 1:9, 10.

Ujuzi huo ni wa maana sana ili kupata wokovu. Mlinzi wa jela Mroma alipowauliza mtume Paulo na mwandamani wake, Sila, “Ni nini ambalo lazima nifanye ili nipate kuokolewa?” walimjibu hivi: “Amini juu ya Bwana Yesu nawe utapata kuokolewa, wewe na watu wa nyumbani mwako.” (Matendo 16:30, 31) Je, hilo lilimaanisha kwamba jambo tu ambalo mlinzi wa jela na familia yake walihitaji kufanya ni kuwa na hisia fulani mioyoni mwao? La, kwa sababu, hawangeweza kwa kweli “kuamini juu ya Bwana Yesu” bila kuwa na uelewevu fulani juu ya Yesu alikuwa nani, alifanya nini, na lile alilofunza.

Kwa kielelezo, Yesu alifundisha kuanzishwa kwa serikali ya kimbingu—“ufalme wa Mungu.” (Luka 4:43) Pia alieleza waziwazi kanuni juu ya adili na tabia za Kikristo. (Mathayo, sura ya 5-7) Alieleza kwa muhtasari msimamo ambao wanafunzi wake wangechukua ilipohusu mambo ya kisiasa. (Yohana 15:19) Alianzisha programu ya elimu ya tufeni pote na kuwaagiza wafuasi wake waishiriki. (Mathayo 24:14; Matendo 1:8) Ndiyo, ‘kuamini juu ya Yesu’ kulimaanisha kuelewa mambo mengi! Basi, si ajabu kwamba, Paulo na Sila ‘walimwambia [huyo mlinzi wa jela] neno la Yehova pamoja na wote wale walio katika nyumba yake’ kabla ya waamini hao kubatizwa.—Matendo 16:32, 33.

Ujuzi Sahihi juu ya Mungu Ni Muhimu Pia

Sehemu ya lazima katika kumwamini Yesu kikweli huhusisha kumwabudu Mungu ambaye Yesu mwenyewe humwabudu. Yesu alisali hivi: “Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

Wakati wa huduma yake ya kidunia, Mwana wa Mungu alielekeza uangalifu sikuzote kwa Babake na si kwake mwenyewe. Hakudai kamwe kuwa Mungu Mweza-Yote. (Yohana 12:49, 50) Katika pindi nyingi Yesu alieleza wazi wadhifa wake katika mpango wa Mungu kwa kusema kwamba alikuwa chini ya Babake. (Luka 22:41, 42; Yohana 5:19) Kwani, Yesu alijulisha wazi hivi: “Baba ni mkubwa zaidi kuliko mimi.” (Yohana 14:28) Je, kanisa lako limekufundisha huo uhusiano wa kweli kati ya Mungu na Kristo? Au umeongozwa kuamini kwamba Yesu mwenyewe ni Mungu Mweza-Yote? Wokovu wako wategemea kuwa na uelewevu sahihi.

Katika Sala ya Bwana, Yesu aliwasihi sana wanafunzi wake wasali hivi: “Jina lako na litakaswe.” (Mathayo 6:9) Tafsiri zilizo nyingi zaidi za Biblia zimelificha jina la Mungu, wakilitafsiri “Bwana.” Lakini katika nakala za kale za “Agano la Kale” jina la Mungu lilionekana zaidi ya mara elfu sita! Hivyo andiko la Zaburi 83:18 lasomeka hivi: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.” (Italiki ni zetu.) Je, umefundishwa kulitumia jina la Mungu, Yehova? Ikiwa sivyo, wokovu wako u hatarini, kwa maana “kila mtu aitiaye jina la Yehova ataokolewa”!—Matendo 2:21; linganisha Yoeli 2:32.

Kwa Roho na Kweli

Yesu Kristo pia alielekeza uangalifu kwenye Neno la Mungu, Biblia. Alipokuwa akifafanua maoni ya Mungu juu ya mambo fulani, nyakati nyingi alikuwa akisema hivi: “Imeandikwa.” (Mathayo 4:4, 7, 10; 11:10; 21:13) Usiku uliotangulia kifo chake, Yesu alisali kuhusu wanafunzi wake hivi: “Watakase kwa njia ya ile kweli; neno lako ni kweli.”—Yohana 17:17.

Hivyo, kuwa na uelewevu wa mafundisho ya Neno la Mungu, Biblia, ni takwa jingine la kutimiza ili kupata wokovu. (2 Timotheo 3:16) Biblia tu ndiyo hujibu maswali kama vile: Ni nini kusudi la uhai? Kwa nini Mungu ameruhusu uovu uendelee kwa muda mrefu sana? Inakuwaje kwa mtu anapokufa? Je, Mungu kwa kweli huwatesa watu motoni? Kusudi la Mungu kwa ajili ya dunia ni nini?a Mtu hawezi kumwabudu Mungu ifaavyo bila uelewevu sahihi wa masuala hayo, kwa maana Yesu alisema hivi: ‘Waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho na kweli.’—Yohana 4:23.

Imani Huchochea Matendo

Wokovu huhusisha mengi zaidi ya kupata habari tu. Katika moyo wenye kuitikia, ujuzi sahihi juu ya Mungu hutokeza imani. (Waroma 10:10, 17; Waebrania 11:6) Imani hiyo husukuma mtu atende. Kwa kielelezo, Biblia huonya kwa upole hivi: “Tubuni na mgeuke kabisa ili mpate kufutiwa dhambi zenu, ili majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka kwa utu wa Yehova.”—Matendo 3:19.

Ndiyo, wokovu pia huhusisha kujipatanisha mwenyewe na viwango vya Mungu vya mwenendo na vya adili. Chini ya uvutano wenye kugeuza umbo wa Neno la Mungu, ufuatiaji wa haki na ukweli huchukua mahali pa mazoea ya muda mrefu wa maisha wa kusema uwongo na kudanganya. (Tito 2:10) Mazoea yasiyo ya adili, kama vile ugoni-jinsia-moja, uzinzi, na uasherati, yanaachwa na mahali pake huchukuliwa na mwenendo safi kiadili. (1 Wakorintho 6:9-11) Huko si kujiepusha kwa muda ambako kwategemea hisia-moyo lakini ni badiliko la kudumu litokanalo na funzo na matumizi yenye uangalifu ya Neno la Mungu.—Waefeso 4:22-24.

Baada ya muda, kumpenda na kumthamini Mungu humsukuma mtu mwenye moyo wa haki ajiweke wakfu kabisa kwa Mungu na kuuonyesha kwa ubatizo wa maji. (Mathayo 28:19, 20; Waroma 12:1) Wakristo waliobatizwa wameokolewa machoni pa Mungu. (1 Petro 3:21) Wakati wa uharibifu unaokuja wa ulimwengu huu mwovu, Mungu atawaokoa kabisa kwa kuwahifadhi hadi mwisho wa dhiki hiyo.—Ufunuo 7:9, 14.

Kile Ambacho Wokovu Waweza Kumaanisha Kwako

Ni wazi kutokana na mazungumzo haya mafupi kwamba kupata wokovu kwahusisha mengi zaidi ya ‘kuwa na Bwana Yesu moyoni.’ Kwamaanisha kuendelea kutwaa ujuzi sahihi juu ya Yehova Mungu na Yesu Kristo na kufanya mabadiliko yahitajiwayo maishani mwa mtu. Huenda kufanya hivyo kukasikika kuwa jambo gumu, lakini Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia katika jitihada hiyo. Kupitia funzo la Biblia nyumbani, wanaweza kukusaidia kuanza kutembea katika njia ya wokovu wa kweli.b

Kwa sababu ya ukaribu wa siku ya Mungu ya hukumu inayokuja, kufanya hivyo ni jambo la uharaka zaidi kuliko wakati mwingine wowote uliotangulia! Sasa ndio wakati wa kuyatii maneno haya ya nabii: “Kabla haijawajilia siku ya hasira ya BWANA. Mtafuteni BWANA, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA.”—Sefania 2:2, 3.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa ajili ya mazungumzo juu ya habari hizi, tafadhali ona kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

b Ikiwa ungetaka funzo la Biblia nyumbani, tafadhali pata habari katika kutaniko la Mashahidi wa Yehova la kwenu. Au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Wokovu Hutokana na . . .

◻ Kupata ujuzi sahihi juu ya Mungu na Yesu.—Yohana 17:3.

◻ Kudhihirisha imani.—Waroma 10:17; Waebrania 11:6.

◻ Kutubu na kugeuka kabisa.—Matendo 3:19; Waefeso 4:22-24.

◻ Kujiweka wakfu na kubatizwa.—Mathayo 16:24; 28:19, 20.

◻ Kuendelea kutangaza hadharani.—Mathayo 24:14; Waroma 10:10.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kujifunza Biblia, kutumia unayojifunza, kujiweka wakfu, na kubatizwa ni hatua ziongozazo kwenye wokovu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki