Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 8/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Amkweza Mtumishi Wake wa Kimesiya
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Mtumishi wa Yehova—‘Alichomwa kwa Silaha kwa Ajili ya Ukosaji Wetu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ninafurahia Kufanya Mapenzi Yako
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Je, Unabii wa Kimasihi Unathibitisha Kwamba Yesu Alikuwa Ndiye Masihi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 8/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Isaya sura ya 53 ina unabii maarufu wa Kimesiya. Mstari wa 10 wasema hivi: “BWANA aliridhika [“ilipendeza BWANA,” Zaire Swahili Bible] kumchubua; amemhuzunisha.” Hilo lamaanisha nini?

Ni rahisi kuona kwa nini swali laweza kuzuka kuhusu Isaya 53:10. Wakristo wa kweli wanajua kwamba Mungu wetu mwenye huruma na wororo hawezi kupendezwa kumchubua au kumhuzunisha yeyote. Biblia inatupa sababu ya kuamini kwamba Mungu hafurahii kuwatesa wasio na hatia. (Kumbukumbu la Torati 32:4; Yeremia 7:30, 31) Katika karne zilizopita, huenda nyakati fulani Yehova aliruhusu kuteseka kwa sababu zinazopatana na hekima na upendo wake. Lakini kwa hakika yeye hakusababisha Mwana wake mpendwa, Yesu, ateseke. Basi, fungu hilo lamaanisha nini kwa kweli?

Naam, twaweza kufahamu maana kwa kuuchunguza mstari wote, tukizingatia neno ‘pendeza’ linalopatikana mara mbili. Isaya 53:10 lasema hivi: “BWANA aliridhika [“ilipendeza BWANA,” ZSB] kumchubua; amemhuzunisha; utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, na mapenzi ya BWANA [“Yehova,” NW] yatafanikiwa mkononi mwake.”

Kwa jumla, ujumbe wa Biblia waonyesha kwamba “mapenzi ya Yehova,” usemi unaotajwa mwishoni mwa mstari huo, hukazia kutekelezwa kwa makusudi yake kupitia Ufalme. Kwa kufanya hivyo, Yehova atatetea enzi kuu yake naye atafanya iwezekane kwa wanadamu watiifu waondolewe dhambi iliyorithiwa—dhambi zetu. (1 Mambo ya Nyakati 29:11; Zaburi 83:18; Matendo 4:24; Waebrania 2:14, 15; 1 Yohana 3:8) Jambo kuu kuhusu hayo yote ni kwamba Mwana wa Mungu alipaswa kuwa mwanadamu ili atoe dhabihu ya fidia. Kama tujuavyo, Yesu aliteseka alipokuwa akifanya hivyo. Biblia yatuambia kuwa “alijifunza utii kutokana na mambo aliyoteseka.” Basi Yesu alinufaika kutokana na mateso hayo.—Waebrania 5:7-9.

Yesu alijua mapema kwamba mwendo mzuri ambao angeufuata ungehusisha maumivu makali ya aina fulani. Hilo ni wazi kulingana na maneno yake yaliyoandikwa kwenye Yohana 12:23, 24, ambapo twasoma: “Saa imekuja kwa Mwana wa binadamu kutukuzwa. Kwa kweli kabisa mimi nawaambia nyinyi, Punje ya ngano isipoanguka kuingia katika ardhi na kufa, hiyo hubaki punje moja tu; lakini ikifa, ndipo hiyo huzaa matunda mengi.” Naam, Yesu alijua kwamba ingembidi ashike uaminifu-maadili wake hata kufikia kufa. Masimulizi hayo yaendelea hivi: “‘Sasa nafsi yangu yataabika, nami nitasema nini? Baba, niokoe kutoka katika saa hii. Hata hivyo, hii ndiyo sababu nimekuja kwenye saa hii. Baba, tukuza jina lako.’ Kwa hiyo sauti ikaja kutoka mbinguni: ‘Mimi nimelitukuza na pia hakika nitalitukuza tena.’”—Yohana 12:27, 28; Mathayo 26:38, 39.

Twaweza kuelewa Isaya 53:10 katika muktadha huo. Yehova alijua vema kwamba mambo ambayo yangempata Mwana wake yangehusisha kuchubuliwa kwa njia fulani. Ingawa hivyo, huku akizingatia manufaa makubwa sana ambayo yangetokea, Yehova alipendezwa na mambo ambayo yangempata Yesu. Kwa maana hiyo, ‘ilipendeza Yehova kumchubua,’ au Mesiya achubuliwe. Yesu naye alipendezwa na mambo ambayo angeweza kutimiza na ambayo alitimiza. Kwa kweli, kama vile andiko la Isaya 53:10 linavyomalizia, ‘mapenzi ya Yehova yalifanikiwa mkononi mwake.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki