Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 1/15 uku. 3
  • Kwa Nini Usitawishe Wema wa Adili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Usitawishe Wema wa Adili?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Tuwezavyo Kusitawisha Wema wa Adili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Wafuatia Wema wa Adili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Tunaweza Kutiaje Wema-adili Katika Imani Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Itikia Ahadi za Mungu kwa Kuzoea Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 1/15 uku. 3

Kwa Nini Usitawishe Wema wa Adili?

MWANAMUME mmoja Mjapani wa makamo aitwaye Kunihito alihamia Marekani hivi majuzi.a Majuma machache baada ya kuwasili huko, alipatwa na hali ambayo nusura imharibie kazi-maisha yake. Kunihito asimulia hivi: “Mkubwa wangu aliponiuliza kama ningefanya kazi fulani, nilikuwa na uhakika kabisa ningeikubali. Lakini kwa kuwa nimelelewa kuona sifa ya kiasi kuwa wema wa adili, nilijibu: ‘Sina hakika kama nitaweza kuifanya, lakini nitajaribu kadiri niwezavyo.’ Mkubwa wangu ambaye ni Mmarekani aliona ni kana kwamba sikuwa na uwezo na uhakika. Nilipotambua jambo hilo, niling’amua kwamba nilihitaji kufanya marekebisho fulani.”

Maria, anayeishi New York City, alikuwa mwanafunzi bora kabisa, ambaye sikuzote alikuwa tayari kuwasaidia wanadarasa wenzake. Juan alikuwa mwanafunzi mwenzi ambaye pindi kwa pindi alimwomba Maria amsaidie. Lakini pia alipendezwa naye kimahaba na kujaribu kumvutia. Ijapokuwa Maria alitamani kudumisha usafi wa kiadili, alikubali kutongozwa na Juan na hatimaye akafanya ngono naye.

Kwa kweli, ni vigumu kudhihirisha wema wa adili katika ulimwengu wa leo ulio na tamaduni tofauti-tofauti na uliopotoka kiadili. Basi kwa nini usitawishe wema wa adili? Kwa sababu mwenendo wenye wema wa adili humpendeza Mungu, na bila shaka wengi wetu tunatamani kupata kibali chake.

Neno la Mungu, Biblia, huhimiza wasomaji wake wasitawishe wema wa adili. Kwa mfano, mtume Paulo aandika hivi: “Wema wa adili wowote ulioko na jambo lolote la kustahili sifa likiwako, endeleeni kufikiria mambo haya.” (Wafilipi 4:8) Naye mtume Petro atuhimiza tufanye ‘jitihada yote yenye bidii kujaza imani yetu wema wa adili.’ (2 Petro 1:5) Lakini wema wa adili ni nini? Je, waweza kufundishwa darasani? Twaweza kuusitawishaje?

[Maelezo ya Chini]

a Baadhi ya majina yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki