Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 9/15 uku. 3
  • Biblia Inaweza Kusaidia Ndoa Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inaweza Kusaidia Ndoa Yako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Baada ya Siku ya Harusi
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Ilinde Ndoa Yako
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kupata Furaha Katika Zawadi ya Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 9/15 uku. 3

Biblia Inaweza Kusaidia Ndoa Yako

NENO ndoa huwafurahisha watu fulani na kuwaumiza wengine. “Ninahisi kuwa nimetalikiwa kihisia,” asikitika mke mmoja. “Ninahisi kuwa nimepuuzwa na mpweke nyakati zote.”

Ni nini huwafanya watu wawili walioweka nadhiri ya kupendana na kutunzana kwa upendo wakose kufanya hivyo? Sababu moja ni kutojua yale ambayo ndoa huhusisha. “Tunafunga ndoa bila kuwa na ujuzi wowote,” anasema mwandikaji mmoja wa habari za tiba.

Uchunguzi uliofanywa na Mradi wa Ndoa katika Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Rutgers huko New Jersey, Marekani, unaonyesha kwamba leo ni watu wachache walio na ujuzi kuhusu ndoa. “Wengi waliohojiwa katika uchunguzi huo wamelelewa katika ndoa zisizo na furaha au na wazazi waliotalikiana,” wanaandika wasimamizi wa mradi huo. “Wanajua hasa hali ya ndoa zisizo na furaha, lakini hawajui ndoa zenye furaha zinakuwaje. Wengine wanaweza tu kusema kwamba ndoa yenye furaha ni ile ‘iliyo tofauti na ya wazazi wao.’”

Je, ndoa za Wakristo hupatwa na matatizo? Ndiyo. Hata baadhi ya Wakristo wa karne ya kwanza walihitaji kushauriwa moja kwa moja ili ‘wakome kutafuta sana kufunguliwa’ kutoka katika ndoa zao. (1 Wakorintho 7:27) Ni wazi kwamba ndoa yoyote ya watu wawili wasio wakamilifu itakuwa na matatizo mara kwa mara, lakini tuna msaada. Waume na wake wanaweza kuboresha uhusiano wao kwa kufuata kanuni za Biblia.

Kwa kweli, Biblia si kitabu cha maagizo ya ndoa tu. Hata hivyo, tunaweza kutazamia kanuni zake zitusaidie kwa kuwa kiliandikwa kwa roho ya Yule aliyeanzisha mpango wa ndoa. Kupitia nabii Isaya, Yehova Mungu alisema: “Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Laiti ungalisikiliza amri zangu! ndipo amani yako ingalikuwa kama mto wa maji, na haki yako kama mawimbi ya bahari.”—Isaya 48:17, 18.

Je, upendo uliokuwa kati yako na mwenzi wako wa ndoa umeanza kupungua? Je, unahisi umenaswa katika ndoa isiyo na upendo? Mke mmoja ambaye amekuwa katika ndoa kwa miaka 26 alisema: “Ni vigumu kueleza maumivu ambayo mtu hupata katika ndoa ya aina hiyo. Hayaishi, yanaendelea tu.” Badala ya kukaa tu katika ndoa isiyoridhisha, mbona usiazimie kuchukua hatua fulani kuiboresha? Makala ifuatayo itawaonyesha waume na wake jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kusaidia ndoa zao katika eneo moja hususa, yaani, kutimiza wajibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki