Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 7/1 uku. 27
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Mambo ya Walawi—Mwito wa Kuja Kwenye Ibada Takatifu ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Tunachojifunza Kwenye Mambo ya Walawi Kuhusu Jinsi ya Kuwatendea Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kitabu Cha Biblia Namba 3—Mambo Ya Walawi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Utakatifu wa Mungu Unatukuzwa na Mambo ya Walawi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 7/1 uku. 27

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Andiko la Kumbukumbu la Torati 14:21 linasema: “Msile mwili wowote uliokufa tayari.” Je, maneno hayo yanapingana na andiko la Mambo ya Walawi 11:40, linalosema: “Anayekula sehemu yoyote ya mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni”?

Mistari hiyo miwili haipingani. Andiko la Kumbukumbu la Torati 14:21 linarudia sheria iliyokataza kula mnyama aliyepatikana akiwa amekufa, labda baada ya kuuawa na wanyama-mwitu. (Kutoka 22:31; Mambo ya Walawi 22:8) Andiko la Mambo ya Walawi 11:40 linaeleza yale ambayo Mwisraeli angeweza kufanya alipovunja sheria hiyo, labda bila kukusudia.

Sheria ilipokataza jambo fulani, hilo halikumaanisha kwamba haingevunjwa wakati fulani. Kwa mfano, kulikuwa na sheria zilizokataza wizi, uuaji, kutoa ushahidi wa uwongo, na kadhalika. Wakati huohuo, kulikuwa na adhabu fulani zilizotolewa kwa kuvunja sheria hizo zilizotoka kwa Mungu. Adhabu hizo zilionyesha uzito wa sheria hizo.

Mtu aliyevunja sheria iliyokataza kula mwili wa mnyama aliyepatikana akiwa amekufa angekuwa asiye safi mbele za Yehova na ingembidi afuate utaratibu unaofaa ili awe safi. Iwapo hangejisafisha kwa njia inayofaa, ‘angejibu kwa kosa lake.’—Mambo ya Walawi 17:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki