Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 1/15 uku. 3
  • Malaika—Wao Ni Akina Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika—Wao Ni Akina Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 1/15 uku. 3

Malaika—Wao Ni Akina Nani?

MFALME mmoja wa milki fulani kubwa hakuamini alichoona. Wanaume watatu waliohukumiwa kifo katika tanuru ya moto waliokolewa kutoka motoni! Ni nani aliyewaokoa? Mfalme mwenyewe aliwaambia hivi wanaume hao: “Abarikiwe Mungu [wenu], aliyemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake waliomtegemea.” (Danieli 3:28) Mtawala huyo wa Babiloni aliyeishi zaidi ya miaka elfu mbili iliyopita alishuhudia watu hao wakiokolewa na malaika. Zamani, mamilioni ya watu waliwaamini malaika. Mbali na kuamini kwamba kuna malaika, watu wengi leo huhisi kwamba malaika wanahusika kwa njia fulani katika maisha yao. Malaika ni akina nani, nao walitoka wapi?

Kulingana na Biblia, malaika ni roho, kama vile Mungu ni Roho. (Zaburi 104:4; Yohana 4:24) Familia ya malaika ni kubwa sana, idadi yao inafikia mamilioni. (Ufunuo 5:11) Wote wana “uwezo katika nguvu.” (Zaburi 103:20) Ingawa wana utu na wamepewa uwezo wa kujiamulia kama wanadamu, malaika hawakuanza maisha yao wakiwa wanadamu. Mungu aliwaumba malaika zamani kabla ya wanadamu—hata kabla ya Dunia kuumbwa. Mungu alipoweka “msingi wa dunia,” Biblia inasema kwamba ‘nyota za asubuhi [malaika] zilipiga vigelegele pamoja kwa shangwe, na wana wote wa Mungu wakaanza kupaaza sauti kwa kushangilia.’ (Ayubu 38:4, 7) Kwa kuwa malaika waliumbwa na Mungu, wanaitwa wana wa Mungu.

Mungu aliwaumba malaika kwa kusudi gani? Malaika wamekuwa na wajibu gani katika maisha ya wanadamu? Je, wanahusika katika maisha yetu leo? Kwa kuwa malaika wana uwezo wa kufanya maamuzi, je, kuna wowote ambao wamefuata njia ya Shetani Ibilisi na kujifanya kuwa maadui wa Mungu? Biblia ina majibu yanayofaa kwa maswali hayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki