Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 5/1 kur. 3-4
  • Uchungu Mwingi na Wenye Kudumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uchungu Mwingi na Wenye Kudumu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Huzuni Nyingi?
  • Msaada Kutoka kwa “Mungu Anayetoa Uvumilivu na Faraja”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wengine Waweza Kusaidiaje?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 5/1 kur. 3-4

Uchungu Mwingi na Wenye Kudumu

HIVI karibuni, mchunguzi mmoja alitaka kujua jinsi wale wanaoomboleza kifo cha wapendwa wao wanavyoumia kihisia kadiri wakati unavyopita. Alituma fomu zenye maswali kwa wazazi ambao walifiwa na watoto miaka kadhaa iliyotangulia. Si wazazi wote waliojibu. Baba mmoja anayeitwa Vladimir, ambaye alifiwa na mwana wake miaka mitano mapema, alisema kwamba bado anahisi uchungu mwingi kuzungumza kuhusu mwana wake.a

Ni jambo la kawaida kwa wazazi waliofiwa kuhisi huzuni kama hiyo yenye kudumu. Miaka kumi iliyopita William alifiwa na mwana wake mwenye umri wa miaka 18 aliyezama katika maji. William anaandika hivi: “Bado ninahisi uchungu wa kifo cha mwana wangu, na nitahisi hivyo maisha yangu yote.” Miaka mitano baada ya Lucy kufiwa na mwana wake kutokana na ugonjwa wa ghafula, aliandika hivi: “Katika siku chache za kwanza, niliendelea kufikiri, ‘Haiwezi kuwa kweli.’ Nilihisi kana kwamba nilikuwa nikiota ndoto mbaya na kwamba ningeamka muda mfupi baadaye . Baada ya muda fulani, nilianza kutambua kuwa ilikuwa kweli, kwamba hakuwa akirudi nyumbani. Mwana wangu alikufa miaka mitano iliyopita, lakini nyakati nyingine, nikiwa peke yangu, bado ninamlilia.”

Kwa nini wazazi waliofiwa, kama Vladimir, William, na Lucy, wanahisi uchungu mwingi sana na wenye kudumu? Acheni tuchunguze sababu fulani.

Kwa Nini Huzuni Nyingi?

Mtoto anapozaliwa katika familia, wazazi wanakuwa na hisia ambazo haziwezi kupatikana katika uhusiano mwingine wowote wa kibinadamu. Kumbeba tu mtoto huyo mikononi mwao, kumtazama akiwa amelala, au kuona jinsi anavyocheka kunawaletea furaha kubwa na uradhi. Wazazi wenye upendo wanawapenda sana watoto wao. Wanawafundisha kujiendesha vizuri na kuwa wenye adabu. (1 Wathesalonike 2:7, 11) Kadiri watoto wanavyoendelea kukua kupatana na jitihada hizo, wazazi wanafurahi na wanaanza kuwa na matumaini makubwa kuhusu watoto wao.

Wazazi wanaojali wanafanya kazi kwa bidii ili kutosheleza mahitaji ya watoto wao. Huenda wakaweka kwa ukawaida akiba ya pesa au vitu vya kimwili ili waweze kuwasaidia watoto wao kuanza familia zao wakati ujao. (2 Wakorintho 12:14) Wakati na pesa nyingi zinazotumiwa, hisia na jitihada zinazohusika zinakazia jambo moja, kwamba wazazi wanawalea watoto wao ili waishi, si wafe. Mtoto anapokufa, kazi ya kumlea inakatizwa, na matumaini ya wazazi yanaharibiwa. Upendo mchangamfu na shauku ya wazazi kwa mtoto wao inakomeshwa na kuzuiliwa na ukuta wa mawe, yaani, kifo. Kwa sasa, nafasi ambayo mwana au binti yao alikuwa nayo mioyoni mwao ni tupu. Wazazi wanahisi huzuni nyingi ambayo haitoweki kwa urahisi.

Biblia inathibitisha kwamba wazazi waliofiwa wana uchungu mwingi na wenye kudumu. Ikieleza yale yaliyotukia wakati mzee wa ukoo Yakobo aliposikia kwamba mwana wake Yosefu alikuwa ameuawa, Biblia inasema hivi: “Yakobo akararua nguo zake za kujitanda, akavaa nguo za magunia viunoni mwake, akamwombolezea mwana wake siku nyingi. Nao wanawe wote na binti zake wote wakawa wakiondoka ili kumfariji, lakini akawa akizidi kukataa kufarijiwa na kusema: ‘Kwa maana nitashuka kuingia katika Kaburi nikimwombolezea mwanangu!’” Miaka mingi baadaye, bado Yakobo alikuwa akimwombolezea mwana wake, ambaye alidhani amekufa. (Mwanzo 37:34, 35; 42:36-38) Mfano mwingine katika Biblia unahusu mwanamke mwaminifu anayeitwa Naomi aliyefiwa na wanawe wawili. Akiwa na huzuni nyingi, alitaka kubadili jina lake Naomi, linalomaanisha “Kupendeza,” na kuitwa Mara, linalomaanisha “Uchungu.”—Ruthu 1:3-5, 20, 21.

Hata hivyo, Biblia haisemi tu kuhusu huzuni ya wazazi. Inasema pia jinsi Yehova anavyowatia nguvu wale wenye huzuni. Katika habari inayofuata, tutachunguza njia mbalimbali ambazo Mungu anatumia kuwafariji wale wanaoomboleza.

[Maelezo ya Chini]

a Baadhi ya majina yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki