Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w08 7/1 uku. 30
  • Je, Ni Vibaya Kutumia Jina La Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ni Vibaya Kutumia Jina La Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu—Maana na Matumizi
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Je, Ni Kosa Kutamka Jina la Mungu?
    Amkeni!—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
w08 7/1 uku. 30

Je, Ni Vibaya Kutumia Jina La Mungu?

KATIKA Maandiko ya Kiebrania ambayo mara nyingi yanaitwa “Agano la Kale,” jina la Mungu linapatikana karibu mara 7,000 katika muundo huu יהוה (likisomwa kutoka kulia kuelekea kushoto).‏ Hilo linamaanisha kuwa jina la Mungu linawakilishwa na herufi nne za Kiebrania Yohdh, He, Waw, na He, linalotafsiriwa kwa kawaida kuwa YHWH.

Muda mrefu uliopita, Wayahudi walikuja kuwa na wazo la ushirikina kwamba ni vibaya kutumia jina la Mungu. Kwa sababu hiyo, walikataa kulitamka, na katika maandishi yao, walianza kutumia maneno mengine badala yake. Hata hivyo, watafsiri wengi wa Biblia wametumia jina “Yahweh,” au “Yehova.” Kati ya tafsiri zilizofanya hivyo ni Biblia ya Wakatoliki Jerusalem Bible. Kulingana na tafsiri hiyo, Musa alipomwuliza Mungu jinsi alivyopaswa kuwajibu Waisraeli ikiwa wangemwuliza ni nani aliyemtuma kwao, Mungu alimwambia hivi: “Waambie wana wa Israeli, ‘Yahweh, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu.’ Hili ndilo jina langu kwa wakati wote; nitaitwa kwa jina hilo kwa vizazi vyote vijavyo.”—Kutoka 3:15.

Alipokuwa akisali, Yesu alisema hivi kuhusu jinsi alivyotumia jina la kimungu: “Nimewajulisha jina lako nami nitaendelea kulijulisha.” Na katika ile inayoitwa sala ya Baba Yetu, Yesu alisema hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na lionwe kuwa takatifu.”—Yohana 17:26; Mathayo 6:9, JB.

Hivyo basi, inaweza kushangaza kujua kwamba katika kitabu chake cha karibuni (Jesus of Nazareth), Papa Benedict wa 16 alisema hivi kuhusu matumizi ya jina la Mungu: “Waisraeli walikuwa . . . sahihi kabisa kukataa kutaja jina hilo ambalo Mungu analitumia mwenyewe, kama linavyoonyeshwa na herufi YHWH, ili kuepuka kulishusha kwa kiwango cha majina ya miungu ya kipagani. Kwa njia hiyohiyo, tafsiri za Biblia za karibuni zilikosea kwa kuandika jina hilo—ambalo sikuzote Waisraeli waliliona kuwa lisiloeleweka na lisilopaswa kutamkwa—kana kwamba lilikuwa jina la kawaida tu la kale.”

Una maoni gani? Ni vizuri au ni vibaya kutumia jina la Mungu? Ikiwa Yehova mwenyewe anasema: “Hili ndilo jina langu kwa wakati wote; nitaitwa kwa jina hilo kwa vizazi vyote vijavyo,” je, kuna yeyote aliye na haki ya kumpinga?

[Picha katika ukurasa wa 30]

Yesu alitumia jina la Mungu katika sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki