Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 10/1 uku. 3
  • Kwa Nini Kuna Ubishi Mwingi Kuhusu Roho Takatifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Kuna Ubishi Mwingi Kuhusu Roho Takatifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Kuitambua Roho Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Roho Takatifu—Kani ya Utendaji ya Mungu
    Je, Uamini Utatu?
  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Roho Takatifu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 10/1 uku. 3

Kwa Nini Kuna Ubishi Mwingi Kuhusu Roho Takatifu

ROHO takatifu ni nini? Huenda swali hilo likaonekana rahisi lakini huenda ikawa vigumu kupata jibu lake. Papa Benedikto wa 16 aliuambia hivi umati uliokuwa umekusanyika huko Australia: “Ni kana kwamba hatuwezi kuelewa Roho ni nini hasa.”

Bila shaka, watu hawana uhakika na hutoa maoni mengi kuhusu swali, Roho takatifu ni nini? Yafuatayo ni baadhi ya majibu yanayotolewa:

• Ni mtu halisi anayeishi ndani ya wanafunzi wa Kristo.

• Sayansi ya kimungu, sheria ya Mungu ikitenda.

• Mungu akitenda katika ulimwengu.

• Mtu wa tatu katika Utatu.

Kwa nini kuna ubishi mwingi hivyo? Ubishi huo ulianza katika karne ya nne W.K. ambapo wanatheolojia fulani walidai kwamba roho takatifu ni mtu ambaye kwa njia fulani analingana na Mungu. Hata hivyo, jambo hilo halipatikani katika Maandiko wala wafuasi wa mapema wa Kristo hawakufundisha hivyo. Kitabu fulani (New Catholic Encyclopedia) kinaeleza hivi: “Kwa wazi Agano la Kale halionyeshi kuwa roho ya Mungu ni mtu . . . Roho ya Mungu ni nguvu za Mungu.” Kitabu hichohicho kilisema hivi: “Maandiko mengi ya Agano Jipya huonyesha roho ya Mungu kuwa kitu, wala si mtu; jambo hilo linaonekana hasa kutokana na ulinganifu uliopo kati ya roho na nguvu za Mungu.”

Inaeleweka kwamba watu huona vigumu kufikiria nguvu kuwa mtu. Hivyo, uchunguzi uliofanywa karibuni nchini Marekani ulionyesha kwamba watu wengi wanapinga wazo la kwamba roho takatifu ni mtu. Je, wako sahihi? Au je, tunapaswa kuwaamini wanatheolojia ambao husisitiza kwamba “Roho Mtakatifu ni Mtu tofauti na Baba na Mwana”?

Ili kupata jibu linalotegemeka, tunahitaji kuchunguza Neno la Mungu, Biblia, ambalo hufafanua roho takatifu kwa undani. Mtume Paulo aliandika hivi: “Maandiko yote Matakatifu yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, . . . kusahihisha makosa.”—2 Timotheo 3:16, Biblia Habari Njema.

Kwa nini utafute ukweli kuhusu roho takatifu? Kwa sababu kujua kweli kunaweza kukufungulia njia ya kupata msaada kutoka kwa Mungu. Je, nyakati nyingine wewe huona kwamba huna nguvu za kuvumilia hali ngumu? Yesu aliwaahidi wanafunzi wake hivi: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa . . . Ikiwa ninyi . . . mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”—Luka 11:9, 13.

Katika habari zinazofuata, Maandiko yatatufafanulia roho takatifu ni nini. Na tutajifunza jinsi ambavyo inaweza kutunufaisha maishani.

[Blabu katika ukurasa wa 3]

Maandiko yanatufafanulia roho takatifu ni nini

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki