Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 10/1 uku. 15
  • Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Shetani
    Amkeni!—2013
  • Shetani Ni Nani? Ni Kiumbe Halisi?
    Amkeni!—2007
  • Je, Shetani Ni Alama tu ya Uovu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 10/1 uku. 15

Wasomaji Wetu Wanauliza

Je, Ibilisi Ni Kiumbe Halisi?

Ndiyo, Biblia inafundisha kwamba Shetani Ibilisi ni kiumbe halisi. Hata hivyo, wachambuzi wa Biblia wanapuuza wazo hilo. Wanasema kwamba Shetani ni uovu tu ulio ndani ya wanadamu.

Je, tushangazwe na ubishi uliopo kuhusu Shetani ni nani? Sivyo hata kidogo. Kwa mfano: Mhalifu anaweza kufuta alama zake za vidole baada ya kufanya uhalifu ili asitambuliwe na hivyo aendelee na uhalifu wake. Vivyo hivyo, Shetani ni mhalifu stadi ambaye hufanya matendo yake kwa kujificha na kuendeleza maadili yaliyopotoka. Yesu alimtambulisha waziwazi Shetani kuwa ndiye anayesababisha uovu duniani. Yesu alimwita Shetani “mtawala wa ulimwengu huu.”—Yohana 12:31.

Ibilisi alitoka wapi? Ingawa aliumbwa akiwa kiumbe mkamilifu huko mbinguni, malaika huyo mwasi alijifanya mwenyewe Ibilisi wakati alipotamani sana wanadamu wamwabudu badala ya kumwabudu Mungu. Biblia inataja mazungumzo kati ya Shetani na Yesu alipokuwa hapa duniani akifunua waziwazi nia yake yenye ubinafsi. Shetani alijaribu kumshawishi Yesu ‘aanguke chini na kumfanyia tendo la ibada.’—Mathayo 4:8, 9.

Pia, katika mazungumzo yake na Mungu, yaliyorekodiwa katika kitabu cha Ayubu, Shetani alifunua nia yake. Atatumia njia yoyote ile awafanye wanadamu wamkane Mungu.—Ayubu 1:13-19; 2:7, 8.

Fikiria hili: Ikiwa Shetani alizungumza na Yehova Mungu na Yesu Kristo, anaweza jinsi gani kuwa uovu ulio ndani ya wengine? Kwa kweli, hakuna uovu wowote ndani ya Mungu au Mwana wake! Hivyo, ni wazi kwamba, Shetani ni kiumbe halisi, kiumbe mwovu wa kiroho ambaye hamheshimu Yehova wala Yesu.

Kupotoka kwa wanadamu kunathibitisha kuwepo kwa Ibilisi. Mataifa ya ulimwengu huu huacha chakula kioze huku raia zake wakifa njaa. Pia, mataifa yanajirundikia silaha za maangamizi makubwa, na yanachafua mazingira ya dunia. Hata hivyo, watu wengi hawajui chanzo cha matendo hayo yanayochochewa na chuki yanayowaangamiza wenyewe. Kwa nini?

Biblia inafunua kwamba Shetani “amezipofusha akili za wasioamini.” (2 Wakorintho 4:4) Shetani huwadanganya wanadamu kwa kutumia tengenezo lisiloonekana. Yeye ndiye “mtawala wa roho waovu.” (Mathayo 12:24) Kama vile tu kiongozi wa genge la wahalifu anavyoweza kuliongoza bila kujulikana na washiriki wengine wa hilo genge, ndivyo Shetani anavyotumia kwa hila tengenezo lake la malaika waovu kuongoza watu wengi ambao hawajatambua uvutano wake.

Tunashukuru kama nini kwamba Biblia inamfichua Ibilisi na tengenezo lake! Hivyo, tunaweza kuchukua hatua za kuzuia uvutano wa Ibilisi. Biblia inatuhimiza hivi: “Jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.”—Yakobo 4:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki