Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 11/1 uku. 3
  • Hadithi Moja ya Uwongo Inatokeza Nyingine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hadithi Moja ya Uwongo Inatokeza Nyingine
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Justin-Mwanafalsafa, Mteteaji, na Shahidi Mfia-Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Watetezi wa Imani—Je, Walikuwa Watetezi wa Imani au Wanafalsafa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Sehemu ya 3-Je! Wateteaji-Ukristo Walifundisha Fundisho la Utatu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Hadithi ya Pili ya Uwongo: Waovu Wanateseka Katika Moto wa Mateso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 11/1 uku. 3

Hadithi Moja ya Uwongo Inatokeza Nyingine

“MJIHADHARI,” ndivyo mtume Paulo alivyowaandikia Wakristo walioishi mwishoni mwa karne ya kwanza W.K. Alikuwa akiwaonya kuhusu nini? “Labda kuna mtu ambaye atawachukua ninyi kama windo lake kupitia falsafa na udanganyifu mtupu kulingana na pokeo la wanadamu.”—Wakolosai 2:8.

Ingawa Paulo alitoa onyo hilo, kuanzia katikati ya karne ya pili W.K., Wakristo fulani walianza kutumia mawazo ya wanafalsafa wa kale ili kueleza imani yao. Kwa nini? Walitaka kukubaliwa na wasomi wa Milki ya Roma na hivyo kupata wafuasi wengi zaidi.

Justin Martyr, mmoja kati ya Wakristo hao waliojulikana sana, aliamini kwamba Msemaji wa Mungu alijionyesha mwenyewe kwa wanafalsafa Wagiriki mapema sana kabla ya Yesu kuja duniani. Kulingana na Justin na walimu waliofundisha mawazo kama hayo, falsafa na hadithi za uwongo zilifanya Ukristo uwe dini ambayo iliwanufaisha sana wanadamu wote.

Ukristo huo wa Justin Martyr ulifanikiwa sana kupata wafuasi wengi wapya. Hata hivyo, kukubaliwa kwa hadithi moja ya uwongo kuliongoza kwenye hadithi nyingine na kukatokeza yale yanayoaminika sasa kuwa mafundisho ya Kikristo. Ili kufunua hadithi hizo za uwongo, linganisha mambo yafuatayo ambayo yanasemwa na wasomi na yale ambayo Biblia inafundisha hasa.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Devil: Barrators—Giampolo/The Doré Illustrations For Dante’s Divine Comedy/Dover Publications Inc.; angels: Art Resource, NY; trinity relief: Museo Bardini, Florence

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki