Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 11/1 kur. 4-5
  • Swali la 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Swali la 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kufuatia Kusudi Lenye Maana Maishani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kusudi Lenyewe la Uhai
    Amkeni!—1992
  • Ni Nini Maana ya Uhai?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 11/1 kur. 4-5

SWALI LA 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?

ROSALIND, aliyelelewa huko Uingereza, alikuwa na tamaa kubwa ya kupata ujuzi. Pia, alitaka kuwasaidia watu. Baada ya kumaliza shule alipata kazi yenye mshahara mnono ambayo ilihusisha kuwasaidia watu wasio na makao na pia aliwasaidia watu wasiojiweza na wenye matatizo ya kujifunza. Ingawa alikuwa na kazi yenye kuridhisha na alikuwa na vitu vya kimwili, anasema: “Kwa miaka mingi nilijiuliza, ‘Kwa nini tuko hai?’ na ‘Kusudi la maisha ni nini?’”

Kwa nini tuulize swali hilo?

Wanadamu si kama wanyama wasioweza kufikiri. Tuna uwezo wa kujifunza kutokana na mambo yaliyopita, kupanga wakati ujao, na kutafuta kusudi la maisha yetu.

Watu fulani wanafikiri jibu ni nini?

Wengi wanafikiri kwamba kusudi kuu la maisha ni kupata utajiri au umaarufu na hivyo kuwa na furaha.

Jibu hilo linamaanisha nini?

Tunajiamulia mambo ya kutanguliza maishani. Mapenzi ya Mungu si ya maana kuliko tamaa zetu.

Biblia inafundisha nini?

Mfalme Sulemani alijikusanyia utajiri mwingi na kufuatia anasa lakini akatambua kwamba vitu hivyo havikumletea kusudi la kweli maishani. Alitaja jambo linaloleta kusudi la kweli maishani alipoandika: “Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Mwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.” (Mhubiri 12:13) Kushika amri za Mungu kunatia ndani nini?

Mungu anakusudia kwamba tuwe na furaha maishani. Sulemani aliandika: “Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba ale, naam, anywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu. Hilo pia mimi nimeliona, naam mimi, ya kwamba linatoka kwenye mkono wa Mungu wa kweli.”—Mhubiri 2:24.

Mungu pia anataka tupende na kutunza familia zetu. Ona mwongozo rahisi na ulio wazi ambao kila mshiriki wa familia anapewa.

  • “Waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.”—Waefeso 5: 28.

  • “Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.”—Waefeso 5:33.

  • “Enyi watoto, watiini wazazi wenu.”—Waefeso 6:1.

Tukifuata kanuni hizo za Biblia, tutaridhika na kuwa na na furaha ya kadiri. Hata hivyo, jambo muhimu zaidi ambalo tunaweza kufanya ni kujifunza mengi iwezekanavyo kumhusu Muumba na kumkaribia kama Rafiki yetu. Hata Biblia inatualika ‘tumkaribie Mungu.’ Kisha inatoa ahadi hii nzuri ajabu: “Naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Ukikubali mwaliko huo, maisha yako yatakuwa na kusudi halisi.

Rosalind aliyetajwa mapema, sasa anahisi kwamba ametambua kusudi la maisha. Kwenye ukurasa wa 10 wa gazeti hili, unaweza kusoma mambo yaliyomfanya abadili mtazamo wake.

Ili upate habari zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kuishi maisha yanayompendeza Mungu, ona sura ya 12 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Unaweza kukipakua kwenye Tovuti ya www.jw.org/sw

Yesu Alisema Nini Kuhusu Kusudi la Maisha?

Yesu hakuwa na shaka kuhusu kusudi la maisha yake. Alisema: “Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.” (Yohana 18:37) Yesu alitumia maisha yake kuwafundisha watu ukweli kumhusu Mungu na makusudi Yake.

Maisha yetu yatakuwa na kusudi halisi ikiwa tutaiga mfano wa Yesu. Hata Yesu anatualika tujifunze kutoka kwake. (Mathayo 11:29) Hebu fikiria njia mbili zinazoweza kutusaidia kufanya hivyo.

Yesu alifundisha kwamba ili tuwe na furaha, ni lazima ‘tutambue uhitaji wetu wa kiroho.’ (Mathayo 5:3) Tunaweza kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho kwa kupata ujuzi juu ya ‘Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule aliyemtuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.

Yesu aliwaamuru wafuasi wake wawafundishe watu wengine kuhusu mambo waliyojifunza. Alisema: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.”—Mathayo 28:19, 20.

Watu wanaotosheleza uhitaji wao wa kiroho kwa kujifunza Biblia na kufuata yale wanayojifunza, wanatambua kwamba maisha yao yanabadilika na kuwa bora. Wanakuwa na usadikisho wa kwamba maisha yao yana kusudi halisi wanapoanza kuwasaidia wengine kujifunza kumhusu Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki