Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 6/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Nani Ataongoza Ainabinadamu Kwenye Amani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Acha “Amani Ya Mungu” Ilinde Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 6/1 uku. 16

Majibu ya Maswali ya Biblia

Kwa nini hakuna amani duniani?

[Picha katika ukurasa wa 16]

Serikali inayoweza kubadili mioyo ya watu ndiyo tu inayoweza kuleta amani duniani

Biblia inataja sababu mbili kuu. Kwanza, ingawa wanadamu wametimiza mambo yenye kustaajabisha, hawakuumbwa wakiwa na uwezo wa kujiongoza. Pili, jitihada za wanadamu zimeshindwa kufanikiwa kwa sababu “ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu,” Shetani Ibilisi. Hivyo basi, jitihada za wanadamu zimeshindwa kuleta amani duniani.​—Soma Yeremia 10:23; 1 Yohana 5:19.

Pia, ubinafsi na kujitakia makuu kumefanya amani isipatikane duniani. Serikali ya duniani pote inayowafundisha watu kupenda mema na kuwa wenye kujali ndiyo tu inayoweza kuleta amani duniani.​—Soma Isaya 32:17; 48:18, 22.

Ni nani atakayeleta amani duniani?

Mungu Mweza-Yote ameahidi kuleta serikali moja itakayotawala wanadamu wote. Itachukua mahali pa serikali za kibinadamu. (Danieli 2:44) Yesu, Mwana wa Mungu, atatawala akiwa Mkuu wa Amani. Ataondoa uovu wote duniani na atawafundisha watu kuishi kwa amani.​—Soma Isaya 9:6, 7; 11:4, 9.

Tayari mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanatii mwongozo wa Yesu na wanatumia Neno la Mungu, Biblia, kuwafundisha watu jinsi ya kuishi kwa amani. Hivi karibuni, kutakuwa na amani duniani kote.​—Soma Isaya 2:3, 4; 54:13.

Kwa habari zaidi ona sura ya 3 ya kitabu hiki Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki