Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 10/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Ufufuo—wa Nani, na Wapi?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je, Wafu Wana Tumaini Lolote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kuna Tumaini Gani kwa Wafu?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 10/1 uku. 16
[Picha katika ukurasa wa 16]

Majibu ya Maswali ya Biblia

Je, wafu wana tumaini lolote?

Kifo ni kama usingizi katika maana ya kwamba wafu hawajui wala hawawezi kufanya lolote. Hata hivyo, Muumba wa uhai anaweza kuwarudishia wafu uhai kwa kuwafufua. Ili kuthibitisha hilo, Mungu alimpa Yesu nguvu na uwezo wa kuwafufua watu kadhaa.​—Soma Mhubiri 9:5; Yohana 11:11, 43, 44.

Kwa nini kifo kinalinganishwa na usingizi?

Mungu ameahidi kwamba wafu walio katika kumbukumbu lake watafufuliwa ili waishi katika ulimwengu mpya wenye uadilifu. Kwa sasa, wale ambao watafufuliwa bado watabaki wakiwa wafu hadi Mungu atakapowarudishia uhai. Mungu Mweza Yote anatamani kutumia nguvu zake kuwarudishia wafu uhai.​—Soma Ayubu 14:14, 15.

Hali itakuwaje wakati wa ufufuo?

Watu watakaofufuliwa na Mungu hawatapoteza utambulisho wao. Pia, watawatambua marafiki, na familia zao. Ingawa mwili wa mtu huoza, Mungu anaweza kumfufua mtu huyo akiwa na mwili mpya.​—Soma 1 Wakorintho 15:35, 38.

Watu wachache watafufuliwa ili wakaishi mbinguni. (Ufunuo 20:6) Walio wengi watafufuliwa na kuishi kwenye dunia paradiso. Watakuwa na mwanzo mpya wakiwa na tarajio la kuishi milele.​—Soma Zaburi 37:29; Matendo 24:15.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 6 na 7 ya kitabu, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kukipakua kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki