Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 11/15 kur. 8-9
  • Jinsi Tunavyoweza Kuwasaidia Wenye Uhitaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Tunavyoweza Kuwasaidia Wenye Uhitaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Ziada Yao Ilijazia Upungufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Thamini Ukarimu wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Yehova Huwabariki Sana Wenye Nia ya Kutoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 11/15 kur. 8-9
[Picha katika ukurasa wa 8]

Jinsi Tunavyoweza Kuwasaidia Wenye Uhitaji

“MAPIGANO yalianza baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa, na hivyo maelfu ya Mashahidi wa Yehova walilazimika kukimbia. Kulikuwa na upungufu wa dawa na chakula. Na vitu hivyo vilikuwa ghali mno. Benki zilifungwa na mashine za kutoa pesa hazikuwa zikifanya kazi,” akasema François, mzee wa kutaniko katika nchi moja inayoendelea.

Bila kukawia, ndugu kutoka katika ofisi ya tawi walianza kupeleka pesa na vitu vingine ili kuwasaidia Mashahidi waliokimbilia kwenye Majumba ya Ufalme kote nchini. Vikundi vilivyokuwa vikipigana viliweka vizuizi barabarani, lakini magari ya ofisi ya tawi yaliruhusiwa kupita kwa kuwa vikundi vyote vilijua kwamba Mashahidi hawaungi mkono upande wowote.

François anasema: “Tulipokuwa tukielekea kwenye Jumba moja la Ufalme, gari letu lilimiminiwa risasi. Hata hivyo, hatukujeruhiwa. Tulipomwona mwanajeshi mwenye silaha akikimbia kutuelekea, tulirudisha gari nyuma kwa kasi, tukageuka, na kurudi haraka kwenye ofisi ya tawi. Tulimshukuru Yehova kwamba tulikuwa hai. Siku iliyofuata, ndugu 130 waliokuwa katika Jumba hilo la Ufalme walikimbilia eneo lingine. Baadhi yao walikuja kwenye ofisi ya tawi, na tuliwaandalia mahitaji ya kiroho na ya kimwili hadi mapigano yalipokwisha.”

François anasema hivi: “Baadaye, ofisi ya tawi ilipokea barua nyingi kutoka kwa ndugu kote nchini wakishukuru sana kwa msaada waliopata. Uhakika wao kumwelekea Yehova uliimarika sana walipoona jinsi ndugu zao walivyowasaidia.”

Wakati wa misiba ya asili na ile inayosababishwa na wanadamu, hatuwaambii ndugu na dada zetu wenye uhitaji ‘wajipashe moto na kula vizuri.’ (Yak. 2:15, 16) Badala yake, tunajitahidi kuwaandalia mahitaji yao ya kimwili. Vivyo hivyo, baada ya Wakristo wa karne ya kwanza kuonywa kuhusu njaa kali iliyokuwa ikija, “wanafunzi wakaamua, kila mmoja kwa kadiri ambayo yeyote angeweza kutoa, wafanye huduma ya kupeleka misaada kwa akina ndugu waliokuwa wakikaa Yudea.”​—Mdo.11:28-30.

Tukiwa watumishi wa Yehova, tuko tayari kuwasaidia wenzetu walio na uhitaji wa kimwili. Hata hivyo, watu wana uhitaji wa kiroho pia. (Mt. 5:3) Ili kuwasaidia waone uhitaji huo na kuchukua hatua za kuutosheleza, Yesu aliwaamuru wafuasi wake wafanye wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Kila mmoja wetu hutumia mali, nguvu, na wakati mwingi kutimiza kazi hiyo. Tukiwa tengenezo, tunatumia kiasi fulani cha michango kuwasaidia wengine kimwili, lakini michango inayotolewa hutumiwa hasa kuendeleza kazi ya Ufalme na kueneza habari njema. Kwa njia hiyo, tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu na jirani.​—Mt. 22:37-39.

Wale wanaotegemeza kazi ya ulimwenguni pote ya Mashahidi wa Yehova wana hakika kwamba michango yao inatumiwa ifaavyo. Je, unaweza kuwasaidia ndugu zako wenye uhitaji? Je, ungependa kutegemeza kazi ya kufanya wanafunzi? Ikiwa ndivyo, “usiwanyime watu mema wanayostahili, mkono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.”​—Met. 3:27.

JINSI AMBAVYO WENGINE WANATOA MICHANGO KWA AJILI YA KAZI YA ULIMWENGUNI POTE

Kama ilivyokuwa katika siku za mtume Paulo, wengi leo ‘huweka kando kitu fulani,’ au kiasi fulani cha pesa ambacho wanatumbukiza katika masanduku ya michango ya “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma pesa hizo kwenye ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yao. Unaweza pia kutuma michango moja kwa moja kwa shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu. Ili kujua jina la shirika la kisheria linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika nchi yenu, tafadhali wasiliana na ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi yenu. Anwani za ofisi za tawi zinaweza kupatikana katika tovuti ya www.jw.org. Unaweza kutuma michango ifuatayo moja kwa moja:

  • MICHANGO YA MOJA KWA MOJA

    • Michango ya pesa taslimu, vito, au mali yoyote ya kibinafsi iliyo na thamani.

    • Tia ndani barua inayoonyesha kwamba pesa taslimu au mali hizo ni michango ya moja kwa moja.

  • MPANGO WA MICHANGO YENYE MASHARTI

    • Michango ya pesa taslimu ikiwa na masharti kwamba inaweza kurudishwa ikihitajiwa na aliyechangia.

    • Tia ndani barua inayoonyesha kwamba mchango una masharti.

  • UTOAJI ULIOPANGWA

    Mbali na zawadi za pesa na mali za kibinafsi zenye thamani, kuna njia nyingine za kutoa kwa ajili ya kazi ya Ufalme ya ulimwenguni pote. Njia hizo zimeorodheshwa hapa chini. Haidhuru ni njia gani ambayo ungependa kutumia, tafadhali wasiliana kwanza na ofisi ya tawi inayosimamia kazi nchini mwenu ili kuona ni njia zipi zinazokubaliwa katika nchi yenu. Kwa kuwa matakwa ya kisheria na sheria za kodi zinatofautiana, ni muhimu kuwaona washauri wanaostahili wa mambo ya kodi na wa sheria kabla ya kuchagua njia bora ya kutoa mchango.

    Bima: Mchango unaotolewa kwa kutaja kihususa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova kwamba ndilo litakalofaidika na bima ya maisha au mpango wa malipo ya uzeeni au ya kustaafu.

    Akaunti za Benki: Akaunti za benki, hati za amana, au akiba za pesa za kustaafu za mtu mmoja-mmoja zinaweza kuwekwa zikiwa amana, au kulipwa wakati wa kifo kwa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova kulingana na matakwa ya benki za kwenu.

    Hisa na Dhamana: Hisa na dhamana zinaweza kuchangwa kwa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova zikiwa zawadi ya moja kwa moja au kama shirika ambalo litafaidika na hisa au dhamana hiyo kifo kikitokea.

    Ardhi na Nyumba: Ardhi au nyumba zinazotolewa kama mchango kwa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova, zinaweza kutolewa zikiwa zawadi ya moja kwa moja au zawadi yenye masharti, yaani, mtoaji anaweza kuendelea kuishi humo hadi kifo chake.

    Malipo ya Mwaka: Pesa au amana zinazotolewa kama mchango kwa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova chini ya makubaliano kwamba anayetoa mchango huo, au mtu fulani aliyechaguliwa na mtoaji, anapata kiasi fulani cha pesa kila mwaka katika maisha yake yote. Mtoaji anapunguziwa kodi ya serikali katika mwaka ambao mpango huo unaanzishwa.

    Wasia na Amana: Mali au pesa zinaweza kuachiwa jina la shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova kama urithi kwa njia ya wasia halali, au linaweza kutajwa kuwa shirika ambalo litafaidika na mkataba wa amana. Chini ya mpango huu, kodi fulani zinaweza kupunguzwa.

Kama usemi “utoaji uliopangwa” unavyoonyesha, ili mtu atoe michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango hususa. Broshua ya Kiingereza na Kihispania yenye kichwa Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotaka kutegemeza kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kupitia utoaji uliopangwa. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa au baadaye kama urithi mtu anapokufa. Huenda habari zilizo katika broshua hiyo zisifae kabisa hali yako kwa sababu ya sheria za kodi au sheria nyingine nchini mwenu. Baada ya kusoma broshua hiyo, zungumza na washauri wako wa mambo ya kisheria au kodi. Kwa kutumia njia za utoaji uliopangwa, watu wengi wametegemeza utendaji wetu wa kidini na wa kutoa misaada ulimwenguni pote, na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Unaweza kupata broshua hiyo kwa kuomba nakala kutoka kwa mwandishi wa kutaniko ikiwa inapatikana nchini mwenu.

Kwa habari zaidi, unaweza kuandika barua au kupiga simu kwa ofisi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi katika nchi yenu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki